SOMO LA 4
Kutoa Utangulizi Mzuri wa Maandiko
Mathayo 22:41-45
MUHTASARI: Tayarisha akili za wasikilizaji wako kabla ya kusoma andiko.
JINSI YA KUFANYA HIVYO:
Fikiria lengo lako la kusoma andiko. Toa utangulizi wa kila andiko kwa njia itakayowafanya wasikilizaji wako wakazie fikira jambo kuu katika mstari unaosoma.
Tumia Biblia kuwa mamlaka yako. Unapozungumza na watu wanaomwamini Mungu, wasaidie waikazie fikira Biblia kuwa Neno la Mungu. Unapofanya hivyo utawaonyesha kwamba unawafundisha mawazo ya Mungu.
Chochea upendezi wa wasikilizaji wako. Uliza swali ambalo litajibiwa katika andiko, taja tatizo ambalo litatatuliwa na andiko, au taja kanuni ambayo itafafanuliwa na simulizi la Biblia.