Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • th somo la 2 uku. 5
  • Kutoa Hotuba kwa Njia ya Maongezi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kutoa Hotuba kwa Njia ya Maongezi
  • Boresha Uwezo Wako wa Kusoma na Kufundisha
  • Habari Zinazolingana
  • Shauku
    Boresha Uwezo Wako wa Kusoma na Kufundisha
  • Kuzungumza kwa njia ya kawaida
    Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
  • Kuzungumza kwa Usadikisho
    Boresha Uwezo Wako wa Kusoma na Kufundisha
  • Kuzungumza kwa Hisia
    Boresha Uwezo Wako wa Kusoma na Kufundisha
Pata Habari Zaidi
Boresha Uwezo Wako wa Kusoma na Kufundisha
th somo la 2 uku. 5

SOMO LA 2

Kutoa Hotuba kwa Njia ya Maongezi

Andiko lililotajwa

2 Wakorintho 2:17

MUHTASARI: Zungumza kwa njia ya kawaida inayoonyesha jinsi unavyohisi kuhusu habari unayozungumzia na kuwahusu wasikilizaji wako.

JINSI YA KUFANYA HIVYO:

  • Sali na ujitayarishe vizuri. Sali ili upate msaada wa kukazia fikira ujumbe wako, si kuhusu wasiwasi unaohisi. Hakikisha mambo makuu unayohitaji kuwasilisha yako wazi akilini mwako. Eleza mawazo kwa maneno yako mwenyewe; usirudie tu kusema maneno yaliyochapishwa.

    Dokezo linalofaa

    Ikiwa utasoma Biblia au chapisho lingine kwa sauti, fahamu vizuri simulizi utakalosoma ili usomaji wako utiririke. Ikiwa kuna watu walionukuliwa, soma maneno yao kwa hisia, lakini usipite kiasi.

  • Zungumza kutoka moyoni. Fikiria kwa nini wasikilizaji wanahitaji kusikia ujumbe wako. Wakazie fikira. Kisha kupitia njia yako ya kusimama, ishara zako, na uso wako utaonyesha uchangamfu na urafiki.

    Dokezo linalofaa

    Usifikiri kwamba kuzungumza kwa njia ya kawaida kunamaanisha kuzungumza kizembe. Dumisha heshima ya ujumbe wako kwa kuzungumza kwa njia inayoeleweka na iliyo sahihi kisarufi.

  • Watazame wasikilizaji wako. Watazame wale unaoongea nao ikiwa desturi za kwenu zinaruhusu. Unapotoa hotuba, usipitishe tu macho kutoka upande mmoja hadi mwingine ukiwatazama watu wote wa ujumla, bali mtazame mtu mmoja, kisha mtazame mwingine.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki