Faraja
Faraja katika Maandiko inayotusaidia kushinda baadhi ya mambo yanayosababisha tuvunjike moyo
Hisia kali za kuwa na hatia
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
2Fa 22:8-13; 23:1-3—Baada ya Sheria ya Musa kusomwa kwa sauti, Mfalme Yosia na raia wake wanatambua kwamba wana hatia kubwa
Ezr 9:10-15; 10:1-4—Kuhani Ezra na watu wengine wana hisia kali za hatia kwa sababu baadhi yao wamekosa kumtii Yehova na kuoa wanawake wa kigeni
Lu 22:54-62—Mtume Petro anahisi hatia na kuhuzunika sana baada ya kukana mara tatu kwamba hamjui Yesu
Maandiko yenye kufariji:
Tazama pia Isa 38:17; Mik 7:18, 19
Masimulizi ya Biblia yenye kufariji:
2Nya 33:9-13, 15, 16—Manase ni miongoni mwa wafalme wabaya zaidi wa Yuda; hata hivyo, anatubu na kupata rehema
Lu 15:11-32—Yesu anasimulia mfano wa mwana mpotevu kuonyesha jinsi Yehova alivyo tayari kusamehe kabisa
Kuhisi hatufai tunapokabili tatizo tunaloshindwa kusuluhisha au mgawo mgumu
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
Kut 3:11; 4:10—Nabii Musa anahisi hafai au hastahili anapoambiwa aende kukutana na Farao ili awatoe watu wa Mungu kutoka Misri
Yer 1:4-6—Yeremia anahisi yeye ni kijana sana na hana uzoefu wa kutumikia akiwa nabii wa Yehova kwa watu wenye kiburi
Maandiko yenye kufariji:
Masimulizi ya Biblia yenye kufariji:
Kut 3:12; 4:11, 12—Kwa subira, Yehova anamhakikishia nabii Musa kwamba atamsaidia katika mgawo wake
Yer 1:7-10—Yehova anamhakikishia nabii Yeremia kwamba atamsaidia kukabiliana na changamoto zitakazotokea
Kukata tamaa kwa sababu ya udhaifu na dhambi zetu
Tazama “Kukata Tamaa”
Kukata tamaa wengine wanapotuvunja moyo, wanapotuumiza, au hata kutusaliti
Tazama “Kukata Tamaa”
Kutoweza kufanya mengi kwa sababu ya ugonjwa au umri mkubwa
-
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
2Fa 20:1-3—Mfalme Hezekia analia sana kwa sababu amepata ugonjwa mbaya ambao ungemsababishia kifo
Flp 2:25-30—Epafrodito ameshuka moyo kwa sababu kutaniko limesikia kwamba anaumwa na ana wasiwasi kuwa wanaweza kuhisi ameshindwa kutimiza mgawo wake
Maandiko yenye kufariji:
Masimulizi ya Biblia yenye kufariji:
2Sa 17:27-29; 19:31-38—Mzee mshikamanifu Barzilai anapewa mgawo wa heshima kubwa, lakini kwa kuwa ana sifa ya kiasi anaukataa kwa sababu anahisi kwamba ana umri mkubwa na hawezi kutimiza mgawo huo
Zb 41:1-3, 12—Mfalme Daudi alipokuwa mgonjwa sana, alikuwa na uhakika kwamba Yehova angemtegemeza
Mk 12:41-44—Yesu anamsifu mjane maskini kwa mchango wake kwa sababu alitoa kila kitu alichokuwa nacho
Mahangaiko
Tazama “Mahangaiko”
Mateso
Tazama “Mateso”
Maumivu ya kihisia ya muda mrefu kwa sababu ya kutendewa kwa njia isiyofaa na wengine
Tazama “Kutendewa kwa Njia Isiyofaa”
Shaka kuhusu thamani yetu
Tazama “Shaka”
Uchungu; kuweka kinyongo
Baadhi ya watu wana uchungu kwa sababu ya matatizo mengi wanayokabili au ukosefu wa haki
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
Maandiko yenye kufariji:
Masimulizi ya Biblia yenye kufariji:
Ru 1:6, 7, 16-18; 2:2, 19, 20; 3:1; 4:14-16—Naomi anakuwa na furaha tena baada ya kurudi kwa watu wa Mungu, kukubali msaada wao, na kuwasaidia wengine
Ayu 42:7-16; Yak 5:11—Ayubu anavumilia kwa imani, na Yehova anambariki sana
Wengine wanakuwa na uchungu kwa sababu ya matendo yasiyo ya fadhili ya watu wengine
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
1Sa 1:6, 7, 10, 13-16—Hana anaumia sana moyoni kwa sababu ya matendo yasiyo ya fadhili ya Penina na kuhukumiwa vibaya na Kuhani Mkuu Eli
Ayu 8:3-6; 16:1-5; 19:2, 3—Wafariji watatu wa uwongo wa Ayubu ni waadilifu kupita kiasi na wanamshutumu isivyo haki, na kufanya Ayubu ahisi vibaya zaidi
Maandiko yenye kufariji:
Masimulizi ya Biblia yenye kufariji:
1Sa 1:9-11, 18—Hana alihisi vizuri baada ya kummiminia Yehova moyo wake
Ayu 42:7, 8, 10, 17—Baada ya Ayubu kuonyesha roho ya kusamehe, Yehova anamrudishia afya nzuri na furaha yake
Wivu; husuda
Tazama “Wivu”
Woga usiofaa; Hofu
Tazama “Woga”