Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g24 Na. 1 kur. 10-12
  • Kwa Nini Hakuna Heshima Katika Familia?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kwa Nini Hakuna Heshima Katika Familia?
  • Amkeni!—2024
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • KWA NINI NI MUHIMU KUWA NA HESHIMA KATIKA FAMILIA
  • JAMBO UNALOWEZA KUFANYA
  • MAMBO TUNAYOFANYA
  • Unaweza Kupata Msaada
    Amkeni!—2020
  • Msaada Zaidi Kwa Ajili ya Familia
    Amkeni!—2018
  • Jipatie Hekima ya Kukabiliana na Changamoto za Kila Siku Kwenye JW.ORG
    Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2022
  • Dokezo la Kujifunza
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2023
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—2024
g24 Na. 1 kur. 10-12
Mume aliyeudhika anatumia simu yake huku mke wake akijaribu kuongea naye. Mtoto wao anawatazama.

Kwa Nini Hakuna Heshima Katika Familia?

KWA NINI NI MUHIMU KUWA NA HESHIMA KATIKA FAMILIA

Familia inakuwa na amani washiriki wake wanapoheshimiana.

  • Kitabu The Seven Principles for Making Marriage Work kinasema kwamba wenzi wa ndoa wanapoheshimiana, wanaonyeshana upendo “si katika mambo makubwa tu bali pia katika mambo madogo-madogo kila siku.”

  • Utafiti unaonyesha kwamba watoto wanaofundishwa kuwaheshimu wengine hujiamini, hufurahia uhusiano mzuri zaidi na wazazi wao, na hawana matatizo mengi ya kihisia.

JAMBO UNALOWEZA KUFANYA

Fanyeni mipango mkiwa familia. Kwanza, hakikisha kwamba kila mtu katika familia anaelewa jinsi ya kuonyesha heshima. Pili, andikeni mambo ambayo kila mtu katika familia anapaswa kufanya na mambo ambayo anapaswa kuepuka. Tatu, mkiwa familia, fanyeni mipango na mzungumzie kile ambacho ninyi na watoto wenu mnapaswa kufanya ili kuonyeshana heshima.

“Mipango ya wenye bidii hakika huleta mafanikio.”—Methali 21:5.

Weka mfano mzuri. Je, wewe huwachambua watu wa familia yako kwa sababu ya makosa yao, unawakejeli kwa sababu ya maoni yao, au unawapuuza au kukatiza mazungumzo wanapoongea na wewe?

Dokezo: Ona heshima kuwa jambo ambalo unapaswa kumwonyesha mwenzi wako na watoto wako, na si jambo ambalo wanahitaji kufanyia kazi ili wastahili kupata.

“Katika kuonyeshana heshima, iweni wa kwanza.”—Waroma 12:10.

Waonyeshe wengine heshima hata kama hukubaliani na maoni yao. Unapojieleza, epuka kutumia maneno kama “ni kawaida yako” au “haujawahi.” Maneno kama hayo yatamuumiza sana mshiriki wa familia yako na yatasababisha tatizo dogo liwe kubwa.

“Jibu la upole hutuliza hasira, lakini neno kali huchochea hasira.”—Methali 15:1.

Msichana akitazama video katika tovuti ya jw.org.

MAMBO TUNAYOFANYA

Mashahidi wa Yehova huwatia moyo washiriki wa familia watendeane kwa heshima, wakifanya hivyo mara nyingi kupitia makala, vitabu, broshua, na video wanazotoa bila malipo.

KWA AJILI YA WENZI WA NDOA: Mfululizo wa makala Msaada kwa Ajili ya Familia unaweza kuwasaidia waume na wake kuwa . . .

  • wasilikilizaji wazuri

  • kukomesha tabia ya kunyamaziana

  • kuacha kugombana

(Tafuta “Msaada kwa Ajili ya Familia” kwenye jw.org/sw)

KWA AJILI YA WAZAZI: Mfululizo wa makala Msaada kwa Ajili ya Familia unaweza kuwasaidia wazazi kuwazoeza watoto wao . . .

  • wawe watiifu

  • wasaidie kazi za nyumbani

  • waseme “tafadhali” na “asante”

(Tafuta “Kulea Watoto” na “Kulea Matineja” kwenye jw.org/sw)

Ona pia nyongeza, “Maswali Ambayo Wazazi Huuliza,” kwenye kitabu Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 1. (Tafuta “Maswali Ambayo Wazazi Huuliza” kwenye jw.org/sw)

KWA AJILI YA VIJANA: Sehemu ya Matineja kwenye jw.org ina makala, video, na daftari ambazo zinaweza kuwasaidia vijana . . .

  • kupatana na wazazi wao na ndugu zao

  • kuzungumza na wazazi wao kwa heshima kuhusu sheria walizoweka

  • kuaminiwa na wazazi wao

(Tafuta “Matineja” kwenye jw.org/sw)

Unaweza kutumia tovuti ya jw.org bila malipo. Hautahitaji kujisajili, kutoa ada, au kulipia gharama, na hautaombwa kutoa taarifa zako za kibinafsi.

Joseph Ehrenbogen.

JIFUNZE MENGI ZAIDI

Joseph Ehrenbogen alikuwa mjeuri na alitumia dawa za kulevya. Aliendelea na tabia hizo hata baada ya kufunga ndoa. Ili kuona jinsi kujifunza Biblia na Mashahidi wa Yehova kuliboresha maisha ya familia yake, tafuta makala yenye kichwa, “Nilijifunza Kujiheshimu na Kuwaheshimu Wanawake” kwenye jw.org/sw.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki