Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lff somo la 38
  • Thamini Zawadi ya Uhai

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Thamini Zawadi ya Uhai
  • Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • CHIMBA ZAIDI
  • MUHTASARI
  • CHUNGUZA ZAIDI
  • Biblia Inasema Nini Kuhusu Kutoa Mimba?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Kutoa Mimba
    Amkeni!—2017
  • Je, Utoaji-Mimba—Ndio Suluhisho?
    Amkeni!—1995
  • Kutoa Mimba—Si Suluhisho Lisilo na Madhara
    Amkeni!—2009
Pata Habari Zaidi
Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
lff somo la 38
Somo la 38. Mume na mke wakimpakata mtoto wao.

SOMO LA 38

Thamini Zawadi ya Uhai

Makala Iliyochapishwa
Makala Iliyochapishwa
Makala Iliyochapishwa

Tunaweza kufurahia kufanya mambo mengi kwa sababu tuko hai. Hata tunapokabili matatizo, bado kuna mambo tunayoweza kufurahia maishani. Tunawezaje kumwonyesha Yehova kwamba tunathamini zawadi ya uhai? Na ni sababu gani muhimu zaidi inayotuchochea kufanya hivyo?

1. Kwa nini tunapaswa kuuthamini uhai?

Tunapaswa kuuthamini uhai kwa sababu ni zawadi kutoka kwa Baba yetu mwenye upendo, Yehova. Yeye “ndiye chanzo cha uhai,” yaani, aliumba kila kitu kilicho hai. (Zaburi 36:9) “Yeye mwenyewe huwapa watu wote uhai na pumzi na vitu vyote.” (Matendo 17:25, 28) Yehova anatupatia vitu tunavyohitaji ili kuendelea kuwa hai. Zaidi ya hilo, amehakikisha kwamba tunaweza kufurahia maisha.​—Soma Matendo 14:17.

2. Tunawezaje kumwonyesha Yehova kwamba tunathamini zawadi ya uhai?

Tangu ulipokuwa tumboni kabla hujazaliwa, Yehova alikutunza. Katika Biblia, Daudi mtumishi wa Yehova alisali hivi: “Macho yako hata yaliniona nikiwa kiinitete.” (Zaburi 139:16) Uhai wako ni wenye thamani kubwa machoni pa Yehova. (Soma Mathayo 10:29-31.) Yehova huhuzunika sana mtu anaposababisha kimakusudi kifo cha mtu mwingine, au hata kifo chake mwenyewe.a (Kutoka 20:13) Yehova huhuzunika pia tunapohatarisha uhai wetu isivyo lazima au tunapokosa kuchukua tahadhari ili kulinda uhai wa wengine. Tunapolinda uhai wetu na kuheshimu uhai wa watu wengine, tunaonyesha kwamba tunathamini zawadi bora ya uhai.

CHIMBA ZAIDI

Jifunze baadhi ya njia unazoweza kuonyesha kwamba unathamini zawadi ya uhai.

3. Tunza afya yako

Wakristo waliojiweka wakfu hutumia maisha yao yote kumtumikia Yehova. Ni kana kwamba wameitoa miili yao iwe dhabihu kwa Mungu. Soma Waroma 12:1, 2, kisha mzungumzie maswali haya:

  • Ni nini kinachopaswa kukuchochea utunze afya yako?

  • Unaweza kufanya hivyo kwa njia gani?

Mwanamke mjamzito akizungumza na daktari.

4. Chukua tahadhari ili kuwalinda wengine wasijeruhiwe au kufa

Biblia inatutia moyo tuepuke kufanya mambo ambayo ni hatari. Onyesha VIDEO ili ujifunze baadhi ya njia za kudumisha usalama.

VIDEO: Zingatia Usalama (8:34)

Soma Methali 22:3, kisha mzungumzie jinsi unavyoweza kulinda usalama wako na wa watu wengine . . .

  • unapokuwa nyumbani.

  • unapokuwa kazini.

  • wakati wa michezo.

  • unapoendesha au kusafiri katika chombo cha usafiri.

Mwanamume akijifunga mkanda kwenye gari.

5. Heshimu uhai wa mtoto ambaye hajazaliwa

Mwanamke mjamzito anashika tumbo lake.

Daudi alifafanua jinsi Yehova anavyopendezwa na ukuzi wa mtoto katika tumbo la mama yake. Soma Zaburi 139:13-17, kisha mzungumzie swali hili:

  • Kulingana na maoni ya Yehova, je, uhai wa mtu huanza mimba inapotungwa au mtoto anapozaliwa?

Sheria ambazo Yehova aliwapa Waisraeli wa kale ziliwalinda akina mama na watoto wao ambao hawajazaliwa. Soma Kutoka 21:22, 23, kisha mzungumzie maswali haya:

  • Yehova alimwonaje mtu aliyesababisha bila kukusudia kifo cha mtoto ambaye hajazaliwa?

  • Yehova atahisije ikiwa mtu atafanya hivyo kimakusudi?b

  • Unaonaje maoni ya Mungu kuhusu jambo hilo?

Onyesha VIDEO.

VIDEO: Thamini Uhai Kama Yehova Anavyouthamini (5:00)

Hata mwanamke anayethamini uhai huenda akahisi kwamba hali zinamlazimu kutoa mimba. Soma Isaya 41:10, kisha mzungumzie maswali haya:

  • Ikiwa mwanamke anakabili mkazo wa kutoa mimba anapaswa kutafuta msaada kwa nani? Kwa nini?

WATU FULANI HUSEMA: “Mwanamke ana haki ya kutoa mimba kwa sababu ni mwili wake.”

  • Ni nini kinachokusadikishia kwamba Yehova anathamini uhai wa mama na mtoto ambaye bado hajazaliwa?

MUHTASARI

Biblia inatufundisha kwamba tunapaswa kupenda, kuheshimu, na kulinda zawadi ya uhai ambayo Yehova ametupatia. Hilo linatia ndani uhai wetu na uhai wa watu wengine.

Ungejibuje?

  • Kwa nini uhai wa mwanadamu ni wenye thamani machoni pa Yehova?

  • Yehova anahisije mtu anaposababisha kimakusudi kifo cha mwanadamu?

  • Ni nini ambacho unathamini kuhusu zawadi ya uhai?

Lengo

CHUNGUZA ZAIDI

Tunawezaje kumshukuru Yehova kwa zawadi ya uhai?

Wimbo 141​—Muujiza wa Uhai (2:41)

Ona jibu la swali hili, Je, Mungu anaweza kumsamehe mwanamke ambaye amewahi kutoa mimba?

“Biblia Inasema Nini Kuhusu Kutoa Mimba?” (Makala iliyo kwenye mtandao)

Jifunze jinsi maoni ya Mungu kuhusu uhai yanavyopaswa kutuongoza tunapochagua burudani.

“‘Michezo Hatari’​—Je, Ujihatarishe?” (Amkeni!, Oktoba 8, 2000)

Namna gani ikiwa mtu anafikiria kujiua? Ona jinsi Biblia inavyoweza kumsaidia.

“Ninataka Kufa​—Je, Biblia Inaweza Kunisaidia Ikiwa Ninawazia Kujiua?” (Makala iliyo kwenye mtandao)

a Yehova anawajali sana watu waliovunjika moyo. (Zaburi 34:18) Anaelewa hisia zenye kuhuzunisha ambazo hufanya watu fulani watamani kujiua, na anataka kuwasaidia. Ili kuona jinsi anavyowasaidia watu washinde hisia hizo, soma makala “Ninataka Kufa​—Je, Biblia Inaweza Kunisaidia Ikiwa Ninawazia Kujiua?” iliyo kwenye sehemu ya Chunguza Zaidi katika somo hili.

b Wale ambao wamewahi kutoa mimba hawapaswi kulemewa na hisia za hatia, Yehova anaweza kuwasamehe. Ili kupata habari zaidi, soma makala “Biblia Inasema Nini Kuhusu Kutoa Mimba?” iliyo kwenye sehemu ya Chunguza Zaidi katika somo hili.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki