Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w12 12/1 uku. 6
  • Kuwasaidia Watu Wenye Uhitaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kuwasaidia Watu Wenye Uhitaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Habari Zinazolingana
  • Kinachowachochea Watu Washerehekee Krismasi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Fuata Kielelezo Cha Yesu Kwa Kuwahangaikia Maskini
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
  • Uwe Mwenye Furaha Waonyeshe Kibali Walio na Shida
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • ‘Wakumbuke Maskini’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
w12 12/1 uku. 6

Kuwasaidia Watu Wenye Uhitaji

“Mwenye jicho la ukarimu atabarikiwa, kwa maana amempa mtu wa hali ya chini chakula chake.”​—METHALI 22:9.

Kwa nini watu fulani husherehekea Krismasi?

Kwa kuwa Yesu aliwasaidia maskini, wagonjwa, na wenye kuteseka, watu fulani wanataka kumwiga. Wanahisi kwamba wakati bora wa kufanya hivyo ni Krismasi, ambapo mashirika ya kutoa misaada hujitahidi sana kukusanya michango.

Kwa nini ni vigumu kufanya hivyo?

Wakati wa Krismasi, watu wengi huhangaikia sana kununua vitu, tafrija, na kuwatembelea marafiki na watu wa ukoo. Mambo hayo huwamalizia wakati, nguvu, pesa za kuwapa maskini na wenye uhitaji, pia za kuchangia mashirika yanayotoa misaada.

Ni kanuni gani za Biblia zinazoweza kutusaidia?

“Usiwanyime watu mema wanayostahili, mkono wako ukiwa na uwezo wa kuyafanya.” (Methali 3:27) Maskini,wenye njaa, na wanaoteseka hawapatwi na matatizo wakati wa Krismasi tu. Ikiwa unatambua kwamba mtu fulani anahitaji msaada na ‘mkono wako una uwezo’ wa kumsaidia, kwa nini usubiri mpaka wakati wa Krismasi ili umsaidie? Utabarikiwa kwa kuwa na matendo ya fadhili na huruma.

“Kila siku ya kwanza ya juma acheni kila mmoja wenu kwenye nyumba yake mwenyewe aweke kando kitu fulani katika akiba kulingana na anavyofanikiwa.” (1 Wakorintho 16:2) Mtume Paulo alitoa shauri hilo kwa Wakristo wa mapema waliotaka kuwasaidia maskini. Je, unaweza ‘kuweka kando’ au kutenga kiasi fulani cha pesa ili uwape kwa ukawaida watu au shirika linalotoa misaada yake kwa hekima? Kwa kufanya hivyo, utakuwa na hakika kwamba unawajali watu wenye uhitaji huku ukitoa kulingana na uwezo wako.

“Msisahau kutenda mema na kushiriki vitu pamoja na wengine, kwa maana Mungu hupendezwa vema na dhabihu za namna hiyo.” (Waebrania 13:16) Ona kwamba licha ya “kushiriki vitu pamoja na wengine” ni lazima pia tukumbuke “kutenda mema” au kuwasaidia wengine. Kwa mfano, wazazi wenye hekima huwazoeza watoto wao kuwasaidia wazee-wazee kufanya kazi za nyumbani za kila siku; kuwatia moyo wagonjwa kwa kuwapa kadi, kuwatembelea, au kuwapigia simu; na kupendezwa kibinafsi na watoto wengine walio maskini au wanaoteseka kutokana na ulemavu. Matokeo ni kwamba watoto wanajifunza kuwa wenye fadhili na ukarimu wakati wote.

Wazazi wenye hekima huwazoeza watoto wao kuwasaidia wazee wazee, wagonjwa na watu wenye uhitaji. Matokeo ni kwamba watoto wanajifunza kuwa wenye fadhili na ukarimu wakati wote

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki