Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w14 12/1 uku. 5
  • Je, Unawasiliana na Mungu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Unawasiliana na Mungu?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Habari Zinazolingana
  • Jinsi Unavyoweza Kumkaribia Mungu
    Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele
  • Mkaribie Mungu Katika Sala
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
  • Uhusiano Wako na Yehova Ni Halisi Kadiri Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Jinsi ya Kusali na Kusikiwa na Mungu
    Kweli Iongozayo Kwenye Uzima wa Milele
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
w14 12/1 uku. 5
Mwanamume akiwasiliana kwa simu na rafiki yake

HABARI KUU | UNAWEZA KUMKARIBIA MUNGU

Je, Unawasiliana na Mungu?

Marafiki hufanya yote wawezayo ili kuwasiliana, iwe ni kwa simu, barua-pepe, video, au barua, nao huwasiliana mara nyingi iwezekanavyo. Kwa hiyo, ili tuwe karibu na Mungu, tunahitaji kuwasiliana naye kwa ukawaida. Lakini, tunawezaje kufanya hivyo?

Tunaweza kuwasiliana na Mungu kupitia sala. Hata hivyo, kusali kwa Mungu ni tofauti na kuzungumza na mwanadamu mwenzako. Tunahitaji kutambua kwamba tunaposali tunazungumza na Muumba wetu, Mwenye Enzi Kuu ya ulimwengu mzima. Kutambua hilo kutatuchochea tusali kwa heshima kubwa na staha. Ili Mungu asikilize sala zetu, tunapaswa kutimiza mambo fulani. Acheni tuchunguze baadhi ya mambo hayo.

Kwanza, tunapaswa kusali kwa Yehova Mungu tu—si kwa Yesu, “mtakatifu fulani,” au sanamu. (Kutoka 20:4, 5) Biblia inasema hivi waziwazi: “Katika kila jambo kwa sala na dua pamoja na kutoa shukrani maombi yenu na yajulishwe Mungu.” (Wafilipi 4:6) Pili, tunapaswa kusali kupitia jina la Mwana wa Mungu, Yesu Kristo. Yesu mwenyewe alisema hivi: “Hakuna anayekuja kwa Baba ila kupitia kwangu.” (Yohana 14:6) Tatu, tunapaswa kusali kuhusu mambo yanayopatana na mapenzi ya Mungu. Biblia inasema hivi: “Hata tukiomba nini kulingana na mapenzi yake, yeye hutusikia.”a—1 Yohana 5:14.

Marafiki wanaopendana huwasiliana mara nyingi iwezekanavyo

Ni kweli kwamba uhusiano hauwezi kusitawi ikiwa mtu mmoja ndiye anayezungumza nyakati zote. Kama marafiki wanavyofurahia kila mmoja wao anapochangia mazungumzo, tunapaswa kumruhusu Mungu azungumze nasi na kumsikiliza anapofanya hivyo. Je, unajua jinsi Mungu anavyozungumza nasi?

Leo, Yehova Mungu huzungumza nasi kupitia Neno lake lililoandikwa, Biblia. (2 Timotheo 3:16, 17) Kwa nini tunasema hivyo? Fikiria mfano huu: Tuseme umepokea barua kutoka kwa rafiki yako mpendwa. Baada ya kuisoma, huenda ukafurahi kuwaeleza hivi wengine, “Nimezungumza na rafiki yangu!” Unasema hivyo hata ingawa ulisoma tu barua, hukuzungumza naye ana kwa ana. Vivyo hivyo, unaposoma Biblia, unamruhusu Yehova azungumze nawe. Hiyo ndio sababu, Gina, aliyetajwa kwenye makala iliyopita, anasema hivi: “Nafikiri kwamba ikiwa ninataka Mungu awe rafiki yangu, ninapaswa kuisoma ‘barua’ yake, yaani, Biblia.” Anaendelea kusema hivi, “Kusoma Biblia kila siku kumenifanya nimkaribie Mungu.” Je, unamruhusu Yehova azungumze nawe kwa kusoma Neno lake, Biblia, kila siku? Kufanya hivyo kutakusaidia umkaribie Mungu.

a Kwa habari zaidi kuhusu jinsi unavyoweza kumkaribia Mungu kupitia sala, ona sura ya 17 ya kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki