“Njia za Kutoa Magazeti Katika Mwezi wa . . .”
Kwa kawaida, kila mwezi katika Mkutano wa Utumishi tuna sehemu inayozungumzia njia za kutoa magazeti. Kusudi la sehemu hiyo si kupitia mambo yaliyomo katika magazeti. Badala yake, sehemu hiyo imekusudiwa kuzungumzia njia za kutoa magazeti hayo. Hivyo, kulingana na maagizo, ndugu atakayeshughulikia sehemu hiyo atatoa utangulizi mfupi sana wenye kuchochea wa magazeti hayo. Kisha, atawaomba wahubiri watoe mapendekezo yao kuhusu makala (au makala kadhaa), moja baada ya nyingine, ili wote waweze kufuatana na habari hiyo na waweze kuona mambo watakayotumia. Badala ya kuwaomba wasikilizaji waeleze kwa ujumla jinsi watakavyotoa magazeti, ndugu anayeshughulikia sehemu hiyo ataomba wasikilizaji kadhaa wapendekeze maswali yatakayoamsha upendezi ambayo watauliza, na baada ya hapo ataomba maelezo ya maandiko ambayo watasoma. Atamalizia sehemu hiyo kwa kuonyesha jinsi kila gazeti linavyoweza kutolewa. Tunatiwa moyo kupitia magazeti hayo mapema kabla ya kufika mkutanoni na kuwa tayari kutoa mapendekezo yetu. Ikiwa wote watajitayarisha vizuri, sehemu hii itatusaidia kunoa uso wa mmoja na mwingine.—Met. 27:17.