Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • g18 na. 2 uku. 4
  • 1 Kuwa na Azimio

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • 1 Kuwa na Azimio
  • Amuka!—2018
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • MAANA YAKE NINI?
  • SABABU GANI NI JAMBO LA MAANA
  • MAMBO YENYE UNAWEZA KUFANYA
  • Namna ya Kutia Nguvu Mapatano ya Ndoa
    Amuka!—2015
  • “Ndoa na Iheshimiwe”
    Mubaki “Katika Upendo wa Mungu”
  • 3 Kuheshimiana
    Amuka!—2018
  • Wakati Urafiki Unakuwa wa Nguvu Sana
    Amuka!—2013
Ona Habari Zaidi
Amuka!—2018
g18 na. 2 uku. 4
Nanga inafanya mashua ibakie fasi moja wakati wa upepo mukali

Azimio ni kama nanga yenye inafanya ndoa yako iendelee kuwa yenye nguvu wakati wa magumu

KWA AJILI YA BIBI NA BWANA

1 Kuwa Na Azimio

MAANA YAKE NINI?

Bibi na bwana wenye wameazimia kushikamana na mupango wa ndoa yao wanaona ndoa kuwa kifungo chenye kuendelea, na hilo linafanya kukuwe hali ya usalama kati yao. Kila mumoja wao iko hakika kama bibi ao bwana yake ataheshimia naziri ya ndoa, hata wakati wa magumu.

Bibi na bwana fulani wanalazimika kubakia pamoja kwa sababu wanaogopa mambo yenye marafiki, wafanyakazi wenzao ao watu wa familia yao wanaweza kusema ikiwa wanaamua kuvunja ndoa. Lakini, jambo la muzuri zaidi ni kuwa na azimio la kushikamana na mupango wa ndoa, azimio lenye kutegemea upendo na heshima yenye bibi na bwana wanaonyeshana.

KANUNI YA BIBLIA: ‘Mume [ao, bwana] hapaswe kumuacha muke [ao, bibi] wake.’​—1 Wakorintho 7:11.

“Ikiwa unaazimia kubakia katika ndoa yako, usikuwe mwepesi kukasirika. Ukuwe mwepesi kusamehe na mwepesi kuomba musamaha. Uone matatizo kama vizuizi, hapana kama magumu yenye haiwezi kumalizika yenye kuongoza mutu avunje ndoa.”​—Micah.

SABABU GANI NI JAMBO LA MAANA

Wakati magumu yanawapata, bibi na bwana wenye hawana azimio la kushikamana na ndoa yao wanaweza kufikia kusema, ‘Tulidanganyika kuoana’ na wanaweza kutafuta njia za kuvunja ndoa.

“Watu wengi wanafunga ndoa wakijua kama ikiwa mambo hayaendeke, wanaweza tu kuivunja. Wakati watu wanafunga ndoa wakifikiri tayari kama kutakuwa nafasi ya kuivunja, wanakosa kuwa na azimio tangu tu mwanzo.”​—Jean.

MAMBO YENYE UNAWEZA KUFANYA

UJICHUNGUZE

Wakati muko munabishana . . .

  • Unafikia kuhuzunika juu ulifunga ndoa na bibi ao bwana yako?

  • Unajiwazia kuishi na mutu mwingine?

  • Unasema maneno kama vile “Nitakuacha” ao “Nitapata mutu mwingine mwenye anapendezwa na mimi”?

Ikiwa ulijibu ndiyo kwenye moja ya maulizo hayo, sasa huu ndio wakati wa kutia nguvu azimio lako la kushikamana na mupango wa ndoa.

ZUNGUMUZA NA BIBI AO BWANA YAKO

  • Kiasi cha azimio letu la kushikamana na mupango wa ndoa kimepunguka? Ikiwa ni hivyo, juu ya nini?

  • Ni hatua gani tunaweza kuchukua sasa ili kutia nguvu azimio letu?

MASHAURI

  • Mara fulani, andikia bibi ao bwana yako ujumbe mufupi wa kimapenzi

  • Onyesha azimio lako la kushikamana na mupango wa ndoa kwa kutia picha za bibi ao bwana yako mahali penye zinaweza kuonekana kwenye kazi

  • Kila siku, ita bibi ao bwana yako kwenye telefone wakati uko kwenye kazi ao mahali pengine

KANUNI YA BIBLIA: ‘Kile ambacho Mungu ameunganisha mutu yeyote asikitenganishe.’​—Mathayo 19:6.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine