Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w14 15/12 uku. 4-5
  • Yehova Anabariki Roho ya Kujitolea

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Yehova Anabariki Roho ya Kujitolea
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Habari za Kufanana na Zile
  • “Kazi Ni Kubwa”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2016
  • Michango Yao ya Zaidi Ilijaza Upungufu wa Wengine
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Tuwasaidie Wale Walio Katika Uhitaji
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Mutu Mwenye Kuonyesha “Ukarimu Atabarikiwa”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2017
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
w14 15/12 uku. 4-5
Mutu fulani anatia muchango katika kisanduku cha feza

Yehova Anabariki Roho ya Kujitolea

MUUMBAJI wetu amewapa wanadamu zawadi ya lazima sana, ni kusema, uhuru wa kuchagua. Tena, anabariki sana wale wenye wanatumia uhuru wao wa kuchagua ili kutegemeza ibada ya kweli na ambao wanatimiza sehemu yao katika kutakasa jina lake na kuunga mukono kusudi lake kubwa. Yehova hapendi tumutii kwa sababu tu tunaona kwamba tunapaswa kufanya hivyo ili tusipatwe na jambo fulani mbaya. Lakini, anafurahi sana kuona watu wanajitoa kwake kwa sababu wanamupenda kwa moyo wote na wanataka kumuonyesha shukrani.

Kwa mufano, wakati Waisraeli walikuwa katika jangwa la Sinai, Yehova aliwaambia wajenge mahali pa ibada. Alisema hivi: ‘Kutoka katikati yenu mutoe muchango kwa ajili ya Yehova. Kila mutu mwenye moyo wenye nia na aulete ukiwa muchango wa Yehova.’ (Kut. 35:5) Kila Muisraeli alipaswa kuleta kile angeweza kutoa. Kila muchango wa kujipendea, iwe ni muchango gani, iwe ni mukubwa ao mudogo, ungeweza kutumiwa kwa njia yenye kufaa ili kutimiza kusudi la Mungu. Waisraeli walitenda namna gani?

‘Kila mutu ambaye moyo wake ulimusukuma’ na ‘kila mutu ambaye roho yake ilimuchochea’ alitoa zawadi ya kujipendea, ‘kila mutu mwenye moyo wenye nia.’ Wanaume na wanawake walitoa kwa kujipendea vitu mbalimbali kwa ajili ya kazi ya Yehova. Walitoa vipini, pete za masikio, pete, zahabu, feza, shaba, uzi ya rangi ya bluu (bleu), manyoya ya wanyama yenye rangi ya zambarau, kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili, kitani bora, manyoya ya mbuzi, ngozi za kondoo-dume zenye zilitiwa rangi nyekundu, ngozi ya sili, mbao za mushita (ao acacia), majiwe yenye bei kubwa, zeri, na mafuta. Mwishowe, ‘vitu hivyo vikakuwa vya kutosha kwa ajili ya kazi yote iliyopaswa kufanywa, na kuzidi.’—Kut. 35:21-24, 27-29; 36:7.

Jambo lenye Yehova alifurahia sana, haikuwa tu vitu vyenye watu walitoa, lakini roho ya kujitolea ya wale wenye walitegemeza ibada safi. Walikuwa pia tayari kutoa wakati wao na nguvu yao. Biblia inasema kwamba ‘wanawake wote waliokuwa wenye hekima ya moyo walisokota (ao walisuka) kwa mikono yao.’ Kwa kweli, ‘wanawake wote ambao mioyo yao iliwasukuma kwa hekima walisokota manyoya ya mbuzi.’ Zaidi ya hilo, Yehova alimupatia Bezaleli “hekima katika uelewaji na katika ujuzi na katika kila aina ya ufundi.” Mungu aliwapatia Bezaleli na Oholiabu uwezo wenye walihitaji ili kufanya kazi yote yenye aliwaomba.—Kut. 35:25, 26, 30-35.

Wakati Yehova aliwaomba Waisraeli watoe michango, alijua kabisa kwamba ‘kila mutu mwenye moyo wenye nia’ atategemeza ibada ya kweli. Kisha, Yehova alibariki sana wale wenye walikuwa tayari kutoa; aliwatolea muongozo na aliwasaidia kupata furaha kubwa sana. Kwa njia hiyo, Yehova alionyesha kwamba wakati anabariki watumishi wake wenye kuonyesha roho ya kujitolea, anaweza kuhakikisha kwamba hakuna kitu kinakosa ili kutimiza mapenzi yake. (Zab. 34:9) Yehova hatakosa kubariki roho yako ya kujitolea ambayo unaonyesha kwa kumutumikia kwa moyo wote.

NJIA MBALIMBALI ZA KUTOA MICHANGO

Kama ilivyokuwa katika siku za Paulo, leo wengi ‘wanaweka kando kitu fulani,’ ao kiasi fulani cha feza ambazo watatia katika kisanduku chenye maandishi “Kazi ya Ulimwenguni Pote.” (1 Kor. 16:2) Kila mwezi, makutaniko yanatuma feza hizo kwenye biro ya tawi ya Mashahidi wa Yehova inayosimamia kazi ya kuhubiri katika inchi yao. Unaweza pia kutuma wewe mwenyewe michango yako kwa shirika linalotumiwa na Mashahidi wa Yehova katika inchi yenu. Ukitaka kujua shirika linalokubaliwa kisheria ambalo Mashahidi wa Yehova wanatumia katika inchi yenu, andikia biro ya tawi ya inchi yenu. Unaweza kupata adresi ya biro ya tawi kwenye www.jw.org.

KUKOPESHA BIRO YA TAWI FEZA

  • Unaweza kukopesha “Association Les Témoins de Jéhovah” feza kwa ajili ya kazi ya kuhubiri ulimwenguni pote. Wakati utahitaji feza zako, biro ya tawi itakurudishia feza hizo bila kukuongezea faida yoyote. Ili kupata habari zaidi unaweza kutumia namba hii ya

  • telefone: 0998189791 ao 0815551000.

MIPANGO MINGINE INAYOHUSU MICHANGO

  • Kuna njia nyingine za kutoa michango kwa ajili ya kazi ya kuhubiri ulimwenguni pote. Njia hizo zinatia ndani:

  • Bima ao Asiranse: Unaweza kuandika kwamba “Association Les Témoins de Jéhovah” ndiyo itachukua feza zako za asiranse ao za pansio. Ili kufanya hivyo mutu anapaswa kwanza kuzungumuza na biro ya tawi ili ajue namna ya kufanya.

Akaunti za Benki

Mutu anaweza kutuma zawadi yake kwa kutia feza katika akaunti ya benki ya “Association Les Témoins de Jéhovah.” Ili kufanya hivyo mutu anapaswa kwanza kuzungumuza na biro ya tawi ili ajue namba ya akaunti ambayo kupitia hiyo atatuma zawadi yake.

Nyumba ao Parsele: Unaweza kuitoa kuwa zawadi. Unaweza kuendelea kuishi katika nyumba hiyo mupaka utakapokufa. Mbele ya kutoa zawadi kama hiyo unapaswa kwanza kuzungumuza na biro ya tawi ya inchi yenu.

Zawadi: Ni mupango wa kutoa feza ao vitu vingine ili viwe mali ya shirika fulani linalotumiwa na Mashahidi wa Yehova. Yule anayependa kutoa zawadi ili kutegemeza kazi ya Ufalme, anapaswa kwanza kuzungumuza na biro ya tawi ili kupata habari zaidi na pia muongozo wa kisheria kuhusiana na zawadi ambayo anapenda kutolea “Association Les Témoins de Jéhovah.”

Wasia ao testama: Shirika la “Association Les Témoins de Jéhovah” linaweza, kupitia testama, kuachiwa uriti wa mali ao feza. Mbele ya kufanya testama hiyo mutu anapaswa kwanza kuzungumuza na biro ya tawi ili kupata habari zaidi na pia muongozo wa kisheria.

Usemi “mipango mingine inayohusu michango” unaonyesha kwamba ili mutu afanye michango ya aina hiyo anapaswa kufanya mipango fulani kamili. Broshua Charitable Planning to Benefit Kingdom Service Worldwide katika Kihispania na Kiingereza imetayarishwa ili kuwasaidia watu wanaotamani kutoa michango ili kazi ya Mashahidi wa Yehova ya kuhubiri ulimwenguni pote iendelee. Broshua hiyo iliandikwa ili kutoa habari kuhusu njia mbalimbali za kutoa zawadi sasa ao kama uriti mutu anapokufa. Kisha kusoma broshua hiyo na kushauriana na washauri wao wa mambo ya kisheria ao kodi, watu wengi wamesaidia kutegemeza kazi yetu ya kuhubiri na wanatoa misaada ulimwenguni pote na kupunguziwa kodi wanapofanya hivyo. Ikiwa unapenda kupata broshua hiyo unaweza kuiomba kwenye biro ya tawi.

Ili kupata habari zaidi, unaweza kuzungumuza na biro ya tawi. Unaweza pia kutuma barua kwenye adresi ya B.P. 634, Limete-Kinshasa, ao kuita namba zilizo hapa chini.

“Association Les Témoins de Jéhovah” no 75, 13ème Rue, Industriel, Limete-Kinshasa, République Démocratique du Congo.

Telefone: 0998189791 ao 0815551000.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine