Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w18 Mwezi wa 7 uku. 30-31
  • Namna ya Kufanya Funzo Lako la Biblia Likuwe Lenye Matokeo na Lenye Kufurahisha Zaidi

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Namna ya Kufanya Funzo Lako la Biblia Likuwe Lenye Matokeo na Lenye Kufurahisha Zaidi
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2018
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Unapata Faida Kabisa Katika Chakula cha Kiroho Chenye Yehova Anatupatia?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2016
  • Unaweza Kufanya Nini Juu Upate Faida Wakati Uko Nasoma Biblia
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
  • Je, Kweli Unapendezwa na Neno la Mungu?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Fanya Namna Yako ya Kujifunza Ikuwe Muzuri Zaidi!
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2019
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2018
w18 Mwezi wa 7 uku. 30-31
Yoshua anasoma Sheria kwa kutumia mwangaza wa mushumaa

Namna ya Kufanya Funzo Lako la Biblia Likuwe Lenye Matokeo na Lenye Kufurahisha Zaidi

Yoshua anasoma Sheria; kuta za Yeriko zinaanguka na nyumba ya Rahabu inabakia yenye kusimama; Yoshua anainua mikono yake kuelekea mbinguni wakati anasali

YOSHUA anapewa magao wenye kuogopesha sana. Anapaswa kuongoza taifa la Israeli katika Inchi ya Ahadi hata kama kuko vizuizi vikubwa. Lakini, Yehova anamuhakikishia kama atapata matokeo ya muzuri, na anamutia moyo hivi: ‘Ukuwe hodari na mwenye nguvu sana. Ufuate Sheria yangu. Uisome muchana na usiku, ili ufuate kwa uangalifu mambo yote yenye kuandikwa ndani. Ukifanya vile, utakuwa na matokeo ya muzuri na utatenda kwa hekima.’​—Yos. 1:7, 8.

Katika hizi “nyakati za hatari zenye kuwa ngumu kuvumilia,” sisi pia tunaweza kupata magumu mengi. (2 Ti. 3:1) Kama Yoshua, tunaweza kupata matokeo ya muzuri kama tunafuata mashauri yenye Yehova alimupatia. Tunapaswa kusoma Biblia kwa ukawaida na kufuata kwa uangalifu kanuni zenye kuwa ndani wakati tunapata magumu.

Lakini pengine watu wengi kati yetu hawajue kujifunza ao hawafurahie kujifunza. Hata hivyo, kwa sababu ni jambo la maana sana kujifunza Biblia, chunguza kisanduku chenye kichwa “Jaribu Kufanya Mambo Haya.” Katika kisanduku hicho utapata mashauri yenye yanaweza kukusaidia kufanya funzo lako likuwe na matokeo ya muzuri na lenye kufurahisha zaidi.

Muandikaji mumoja wa Zaburi aliimba hivi: “Uniongoze katika njia ya amri zako, kwa maana ninaifurahia.” (Zb. 119:35) Unaweza kufurahia sana kujifunza Neno la Mungu. Utavumbua mawazo mengi ya muzuri kadiri unaendelea kujifunza Biblia.

Hata kama hauombwe kuongoza taifa kama vile Yoshua, uko na magumu yako yenye unapaswa kupiganisha. Kwa hiyo, kama Yoshua, ujifunze na kutii mambo yenye yaliandikwa kwa faida yako. Ukifanya vile, wewe pia utapata matokeo ya muzuri na utatenda kwa hekima.

JARIBU KUFANYA MAMBO HAYA:

  • Mwanaume mumoja anaweka mikono yake pamoja wakati anasali

    Usali mbele ya kujifunza. Biblia iko na mawazo ya Mungu mweza-yote yenye aliandikisha kwa faida yako. Kwa hiyo, wakati unasoma Biblia, umuombe akusaidie ili uelewe mambo yenye unasoma, uyakumbuke, na kuyatumikisha katika maisha yako.​—Ezr. 7:10.

  • Mwanaume mumoja anajiuliza ulizo

    Ujiulize maulizo wakati unasoma Biblia ao vichapo vyenye kutegemea Biblia. Ujiulize hivi: ‘Andiko hili linanifundisha nini juu ya Yehova? Namna gani linaunga mukono ujumbe mukubwa wa Biblia? Namna gani ninaweza kutumia mawazo haya ili kusaidia wengine?’

  • Mwanaume mumoja anafikiri sana

    Ufikiri sana juu ya mambo yenye unajifunza. Uache kwanza kusoma na ufikiri hivi: ‘Habari hii inanifanya nijisikie namna gani? Sababu gani inanifanya nijisikie hivi? Namna gani inahusu mambo yenye nimepambana nayo, hali yangu ya sasa, ao mambo yenye yanaweza kutokea wakati wenye kuja? Namna gani ninaweza kutumikisha kanuni hizi za Biblia na mashauri haya katika maisha yangu?’ (Yob. 23:5; Zb. 49:3) Ona ikiwa unaweza kufasiria sababu gani Yehova anaomba watu wake waepuke mazoea fulani ao matokeo yanaweza kuwa nini kama mutu anatenda kwa njia tofauti.​—Kum. 32:28, 29.

  • Mwanaume mumoja anaona picha za habari fulani za Biblia katika akili yake

    Utumie uwezo wako wa kuona picha katika akili wakati unasoma maandiko yenye kueleza habari fulani. Kwa mufano, je, unaweza kuona katika akili picha ya namna mambo yalikuwa wakati ndugu za Yosefu walimuuzisha kwa Waishmaeli? (Mwa. 37:18-28) Unaona nini, unasikia nini, na unasikia harufu gani? Ujitie pa nafasi ya watu wenye kuzungumuziwa. Wanawaza nini na kujisikia namna gani? Kutumia uwezo wako wa kuona picha katika akili kutafanya mambo yenye unajifunza yakuwe wazi na yakuletee faida.

  • Mwanaume mumoja anatumia vyombo vya kusaidia kujifunza

    Utumie vyombo vya kusaidia kujifunza vyenye vimetayarishwa ili kukusaidia kutafuta habari zaidi. Ujifunze kutumikisha vyombo vyenye vinapatikana katika luga yako, vyenye kuwa kwenye Enternete ao vyenye kuchapishwa. Usisite kuomba wengine wakusaidie kujua namna ya kutumikisha muzuri vyombo hivyo. Kwa mufano, kitabu Index des publications des Témoins de Jéhovah ao kitabu Musaada wa Kutafuta Habari kwa Ajili ya Mashahidi wa Yehova, vitakusaidia ujue mambo yenye yamekwisha kuandikwa juu ya habari mbalimbali na kupata mafasirio ya maandiko mengi ya Biblia. Tumia nyongeza zenye kuwa katika Biblia​—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya, kama inapatikana katika luga yenye unajua. Nyongeza hizo zinatoa habari zenye kufaa juu ya jeografia, juu ya namna matukio yalifuatana, juu ya uzito na vipimo, na mambo mengine.

  • Mwanaume mumoja anafanya kifupi cha mawazo makubwa

    Ufanye kifupi cha mawazo makubwa. Kufanya vile kutakusaidia ukumbuke mambo yenye umetoka kujifunza. Na jambo la maana zaidi, uyaelezee wengine. Kuko wazo fulani lenye unaweza kutumikisha katika kazi ya kuhubiri? Kama unafanya mambo hayo, utaweka mawazo makubwa katika akili yako na pia utatumikisha mambo yenye umejifunza ili kusaidia wengine.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine