Mikutano Ya Utumishi Ya Aprili
Juma Toka Aprili 1
Wimbo 1
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyochaguliwa katika Huduma Yetu ya Ufalme.
Dak. 15 : “Tubariki Yehova ‘Mchana Kutwa.’ ” Kwa maulizo na majibu. Someni mafungu 2-5, ikiwa wakati unaruhusu hivyo. Sema juu ya utumishi wa painia, msaidizi na wa kawaida, kwa namna yenye kujenga na kutia moyo.
Dak. 20: “Tutolee Magazeti kwa Wakati Wowote.” Mazungumzo ya mawazo makuu. Kisha sema juu ya makala fulani fulani ambazo zingeweza kutumiwa ili kutolea magazeti ya sasa zaidi ambayo kutaniko limepokea. Maonyesho mawili au matatu kutokana na utoaji mbalimbali unaodokezwa kwenye ukurasa wa 4.
Wimbo 78 na sala ya mwisho.
Juma Toka Aprili 8
Wimbo 164
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Hali ya akaunti.
Dak. 20: “Kufaidika na Shule ya Huduma ya Kitheokrasi Katika 1996—Sehemu ya 3.” Hotuba inayotolewa na mwangalizi wa shule. Watie moyo wale wote wanaoweza kujiandikisha kwenye shule, kisha kutayarisha kiaminifu vipindi wanavyopewa. Fasiria kanuni za kutamka majina ya kibiblia zinazotolewa katika makala. Ili kutoa mfano wa kanuni hizo, tutaweza kusoma Luka 3:23-38 katika tafsiri iliyorudiliwa upya [ikiwa tayari inapatikana] na kusoma majina fulani fulani yanayoandikwa moja kwa moja kutokana na Kiebrania, kama vile Yoanân, Salmôn, Qosam, Seroug, n.k.
Dak. 15: “Kusanyiko la Wilaya 1996—Marekebisho.” Nyongeza. Hotuba inayotolewa na mwangalizi-msimamizi inayotegemea mafungu 1-5. Tilia mkazo juu ya faida zinazotokana na kukomeshwa kwa utumishi wa chakula.
Wimbo 211 na sala ya mwisho.
Juma Toka Aprili 15
Wimbo 6
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Wale wanaoongoza mafunzo ya Biblia wanapaswa kuwatia moyo wanafunzi wanaofanya maendeleo mazuri kujiwekea mradi wa kuwa wahubiri wasiobatizwa. Wazazi wanaweza kuwasaidia watoto wao kwa upande huo. Kumbusha utaratibu wa kufuata unaofasiriwa katika kitabu Tumefanywa Tengenezo Tutimize Huduma Yetu, kurasa 97-99.
Dak. 15: “Kusanyiko la Wilaya 1996—Marekebisho.” Nyongeza. Mafungu 6-15. Kwa maulizo na majibu. Itolewe na mwandishi. Wakati wa kumalizia, vutia uangalifu wa wahudhuriaji juu ya kisanduku “Taarifa” Tia mkazo juu ya ulazima wa kuonyesha usawaziko ili kuleta tu kwenye kusanyiko chakula na vitu vingine vya lazima.
Dak. 20: “Tuwe na Mradi Wakati wa Ziara Zetu za Kurudia.” Mazungumzo yanayoonyesha miradi ya kuwa nayo tunapofanya ziara za kurudia. Maonyesho mawili yanayofanywa na wahubiri wenye uwezo.
Wimbo 100 na sala ya mwisho.
Juma Toka Aprili 22
Wimbo 131
Dak. 5: Matangazo ya kwenu.
Dak. 20: Mahitaji ya kutaniko au hotuba inayotolewa na mzee yenye msingi wa makala ‘Kutenga: Mpango Wenye Kujaa Upendo’ iliyotolewa katika Mnara wa Mlinzi wa Julai 15, 1995, kurasa 25-7.
Dak. 20: Tuongoze Watu Walio na Nia Nzuri Kwenye Tengenezo. Kitegemee broshua Mashahidi wa Yehova—Wanafanya Mapenzi ya Mungu Ulimwenguni Pote, mwangalizi wa utumishi anaongoza mazungumzo kati yake na wahubiri wengine wawili au watatu. Fasiria kwa nini ni jambo lenye manufaa kufundisha wanafunzi jinsi tengenezo linavyotenda kazi, jinsi utendaji walo mbalimbali unavyopangwa kitengenezo na jinsi wanavyoweza kufaidika nao. Chunguzeni habari za kurasa 14 na 15 chini ya kichwa cha habari “Mikutano ya Kuhimizana Ili Kupenda na Kufanya Kazi Nzuri.” Onyesho fupi ndani yalo kikundi kinaonyesha jinsi mawazo hayo yanavyoweza kuingizwa katika mazungumzo wakati wa ziara ya kurudia au wa funzo la Biblia, na hilo katika kusudi la kumsaidia mtu anayeonyesha nia nzuri kuelewa ulazima wa kuhudhuria kwenye mikutano.
Wimbo 126 na sala ya mwisho.
Juma Toka Aprili 29
Wimbo 130
Dak. 5: Matangazo ya kwenu.
Dak. 20: “Tumheshimu Yehova kwa Michango Yetu ya Kujipendea.” Kwa maulizo na majibu, ikitolewa na mzee. Onyesha shauku kwa kuchunguza sehemu hiyo. Wakati wa uchunguzi wa fungu la 6, mzee na mtumishi wa huduma wanazungumza mawazo juu ya zaka, yanayotokana na Mnara wa Mlinzi wa Desemba 1, 1992, kurasa 8 na 9, mafungu 8 mpaka 10 na ukurasa 16, mafungu 16 na 17. Tia ndugu moyo kulinda moyoni ulizo hilo la michango ya kujipendea kwa faida ya kazi ya Ufalme.
Dak. 20: Fanyeni Mambo Katika Familia. Kwa msaada wa Mnara wa Mlinzi wa Septemba 1, 1993, kurasa 16-19, na katika hali changamfu, baba anazungumza na familia yake juu ya umuhimu wa kufanya mambo pamoja. Kazia uangalifu wako juu ya funzo na mahubiri katika familia. Tia mkazo juu ya wazo la kwamba familia ya “kisasa” inagawanyika kwa sababu washiriki wayo wanapitisha wakati mdogo pamoja na hawana tena hivi mambo mengi wanayofanya pamoja. Washiriki wa familia ya Kikristo wananufaika na faida fulani: kuweza kujifunza Neno la Mungu na kushiriki katika huduma pamoja. Kazia ulazima kwa baba kupanga utendaji huo mbalimbali vizuri na kwa mama kushirikiana naye. Watoto wanapaswa kupendezwa na mambo ya kiroho na kushirikiana kwa ukaribu sana na wazazi wao. Familia itakuwa yenye kuungana zaidi na imara zaidi ili kutupilia mbali vishawishi vyenye nguvu zaidi na zaidi ambavyo kusudi yavyo ni kufanya familia iige namna ya kuishi ya ulimwengu.
Wimbo 7 na sala ya mwisho.