Kufaidika Na Shule Ya Huduma Ya Kitheokrasi Katika 1996—Sehemu Ya 3
1 Mtume Paulo alitaka kwamba ndugu zake wasali kwa ajili yake ili apate uwezo wa kusema juu ya habari njema kwa uhodari. (Efe. 6:18-20) Tamaa yetu ni ya kupata uwezo huohuo. Ni kwa sababu hiyo tunathamini msaada ambao Shule ya Huduma ya Kitheokrasi inatutolea. Wale wanaohudhuria kwenye mikutano na wanaotimiza matakwa yanayoombwa wanatiwa moyo kujiandikisha kwayo.
2 Wanafunzi wanapokea mashauri ya kibinafsi yanayowasaidia kutengeneza ufundi wao wa kusema na kufundisha. (Mit. 9:9) Tunaweza pia kufaidika na shule kwa kusikiliza mashauri yanayotolewa kwa wanafunzi wengine na kwa kutumikisha sisi wenyewe yale tunayojifunza. Tunapotayarisha kipindi chetu, imetupasa kujifunza kwa makini habari zinazokusudiwa ili kuwa hakika kwamba tunazitoa kwa usahihi. Mambo makuu na maandiko tunayotumia yanapaswa kuwa yenye kuambatana na utoaji wenye kushikamana wa kichwa cha habari. Ikiwa mtu fulani anapaswa kushiriki kwenye kipindi, itafaa kukitayarisha vizuri kwa kukirudilia pamoja naye kabla ya kukitoa kwenye shule. Kwa kadiri tunavyofanya maendeleo, tungepaswa kujikaza kusema kwa namna ya kutotazamia, tukitumia maandishi mafupi badala ya hotuba iliyoandikwa.
3 Wale wote walio na kipindi kwenye shule wangepaswa kufika mapema, na kutoa fomu zao za Shauri la Usemi kwa mwangalizi wa shule na kukaa nafasi ya mbele ya jumba. Akina dada wangepaswa kumjulisha mapema mwangalizi wa shule nini kitakuwa kikao chao na ikiwa wanapanga kutoa kipindi chao wakiwa wima au wenye kukaa. Kwa kushirikiana katika hali hizo zote, tutachangia kwa uendeshaji mzuri wa programu na tutawasaidia wale wanaoshughulikia jukwa kutayarisha mambo yote mbele ya wakati.
4 Kutayarisha Kipindi Na. 2: Mojawapo ya kusudi la usomaji wa Biblia ni kumsaidia mwanafunzi kutengeneza namna yake ya kusoma. Jinsi gani kufikia hilo vizuri? Njia nzuri ni kusoma mara nyingi sehemu kwa sauti kubwa. Ili kujua maana na kutamka vizuri maneno asiyoyazoea, mwanafunzi atayatafuta katika kamusi inayoonyesha matamshi yayo kwa njia ya maandishi ya sauti (fonetiki), kwa mfano Le Petit Robert. Itampasa bila shaka kufahamiana na alama za maandishi ya sauti zinazotumiwa katika kamusi hiyo.
5 Katika Traduction de monde nouveau, mengi ya majina ya pekee yaliandikwa moja kwa moja kutokana na Kiebrania na yanaandikwa kwa namna ya kuwezesha matamshi yaliyo karibu zaidi na yale ya kwanza. Hivyo, alama ya tamko la sauti ya nguvu (accent circonflexe) juu ya herufi za mwisho-mwisho ân, în au ôn inaonyesha kwamba inafaa kutamka n ikiwa yenye kuachana (kwa mfano, “Salmôn” inatamkwa Salmone). Ikiwa e (bila alama ya tamko la sauti) inapatikana katika silabu mwanzoni au katikati ya jina, kwa kawaida inatamkwa e kama katika “petit” au “parvenir”. Ndivyo, kwa mfano, kuhusu majina Nehémia, Tsephania na Seroug. Katika majina yanayoandikwa moja kwa moja kutokana na Kiebrania, s sikuzote ni yenye kukaziwa kama katika “soleil” (kwa mfano, “Yosek, Qosam”). Bila shaka, hakuna badiliko fulani katika matamshi ya majina yanayojulikana sana ambayo tulilinda mtindo wa Kifaransa (kwa mfano, “Isaac, Jérusalem”).
6 Wazazi wanaweza kuwasaidia watoto kutayarisha usomaji wa namna hiyo. Wanaweza kuwasikiliza wakati wanapojizoeza na kuwatolea mashauri yatakayowasaidia kujiboresha. Wakati unaotolewa unawezesha kutoa utangulizi mfupi na umalizio unaofaa katika huo mwanafunzi atafanya matumizi ya mambo makuu. Anaweza hivyo kukuza uwezo wake wa kusema kwa namna isiyo ya kutazamia.
7 Mtunga zaburi alifanya ombi hili kwa Yehova: “Ee [Yehova], ufungue midomo yangu, na kinywa changu kitaonyesha sifa zako.” (Zab. 51:15) Hivyo basi kushiriki kwetu Shule ya Huduma ya Kitheokrasi na kutusaidie kuonyesha tamaa ileile!