Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 4/96 uku. 1
  • Tubariki Yehova “Mchana Kutwa”

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Tubariki Yehova “Mchana Kutwa”
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Tumsifu Yehova Kila Siku
    Huduma Yetu ya Ufalme—2009
  • Vutia Uangalifu wa Watu Kwenye “Nuru ya Ulimwengu”
    Huduma Yetu ya Ufalme—2006
  • Yehova Anastahili Kusifiwa Sana
    Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • ‘Hubiri Neno la Mungu Kikamili’
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1996
km 4/96 uku. 1

Tubariki Yehova “Mchana Kutwa”

1 Katika Zaburi 145:2, tunakuta ahadi ambayo mfalme Daudi alifanya kwa Yehova: “Nitakubariki [mchana kutwa], na nitasifu jina lako milele na milele.” Sisi pia tuna sababu za kumbariki na kumsifu Baba yetu wa mbinguni. Lakini jinsi gani tunaweza kumwiga Daudi na kutukuza Enzi Kuu ya Yehova “mchana kutwa”?

2 Tujaze Moyo Yetu na Shukrani kwa Yehova: Funzo la kawaida la Neno la Mungu linatia nguvu shukrani yetu kwa yale Yehova amefanya, yale anayofanya na yale atakayofanya tena kwa ajili yetu. Kwa kadiri tutakavyotambua matendo ya ajabu ya Yehova, tutafurika kwa shukrani na tutasema juu ya wema wake. (Zab. 145:7) Tutasukumwa kumsifu Yehova kila wakati.

3 Tumsifu Yehova Katika Mazungumzo Yetu ya Kila Siku: Tunapozungumza na majirani zetu, marafiki zetu, wafanya-kazi wenzetu na watu wengine ambao tunakutana nao kila siku, tunaweza kuchukua nafasi za kuwatangazia tumaini letu. Labda jirani atatujulisha wasiwasi yake kuhusu jeuri katika mtaa; inawezekana kwamba rafiki fulani anafazaishwa sababu ya dawa za kulevya au ufisadi; mfanya-kazi mwenzetu atatoa labda wazo fulani juu ya swala la kisiasa. Tunaweza kuvuta uangalifu wao juu ya kanuni na ahadi mbalimbali zilizomo katika Neno la Mungu na kuwaonyesha msimamo mzuri wa kuwa nao tangu sasa, na pia iwezekanavyo utatuzi kwa magumu yao. Maneno kama hayo yanayotamkwa kwa ‘wakati wake’ yanaweza kuonekana kuwa baraka.—Mit. 15:23.

4 Tuzungumze juu ya Yehova kwa Wakati Wote: Yule aliye na shukrani ya kina kirefu kwa Yehova anatamani kutangaza habari njema kwa watu wengi zaidi iwezekanavyo. (Zab. 40: 8-10) Kwa hiyo tujiulize: ‘Je! mimi nafanya yote niwezayo kulingana na hali yangu?’ Wengi walikuja kutambua kwamba kwa kubadilisha kidogo matumizi yao ya wakati, wangeweza kuwa mapainia wa kawaida. Ikiwa hali yetu ya sasa haituruhusu, je! hatuwezi kuwa mapainia wasaidizi? Ukumbusho unakaribia, na ni wakati wa kuongeza utendaji wetu. Miezi ya Machi na Aprili itakuwa yenye kufaa ili sisi kujitoa zaidi katika utumishi kama vile mapainia wasaidizi.

5 Tuwasaidie Wapya Wajiunge Nasi ili Kumbariki Yehova: Mwadhimisho wa Ukumbusho wa kifo cha Yesu unatukumbusha mwaka baada ya mwaka sababu tulizo nazo za kumshukuru Yehova na kulisifu jina Lake. Ni wakati hasa wenye kufaa ili kuwatia moyo watu wanaojifunza Biblia kujiunga nasi ili kusema hadharani juu ya mamlaka ya kifalme ya Yehova. Tuwatie moyo kufikiri katika sala kwa yale yanayosemwa katika kitabu Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele, kurasa 173-5, mafungu 7-9. Ikiwa wanatimiza matakwa yanayoombwa, hawana sababu yoyote ya kungoja, ati tu kwa sababu wanakosa ujuzi. Wahubiri wenye uwezo wanaweza kuwaonyesha jinsi tunahubiri Ufalme. Ikiwa wapya wanapata uhodari wa lazima ili kusema juu ya habari njema, wanaweza kupata uhakika wa kwamba Yehova atawasaidia.—Mdo. 4:31; 1 Thes. 2:2.

6 Ikiwa tunajikaza kumbariki Yehova mchana kutwa, matokeo yatakuwa faida za milele kwetu wenyewe na kwa majirani.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine