Mafunzo Ya Biblia Yanayotokeza Wanafunzi
1 “Ni nini chenye kunizuia nisibatizwe?” aliuliza towashi Mwethiopia kwa Filipo ‘aliyemtangazia habari njema kuhusu Yesu.’ (Mdo. 8:27-39) Towashi alikuwa tayari mwenye kuonyesha upendo kwa maandishi yaliyoongozwa na Mungu na, kisha kupokea msaada wa kiroho wa Filipo, alikuwa tayari kugeuka kuwa mwanafunzi. Lakini watu wote hawasadiki kwamba wana uhitaji wa kuchunguza Maandiko wenyewe.
2 Jambo la kupendeza ni kwamba, tengenezo la Yehova lilitutolea broshua mpya, yenye kichwa Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote, inayowaalika watu kuchunguza ujumbe wa Biblia kwa wakati wetu. Mambo yaliyomo yangepaswa kuwavutia watu wanyofu, walio labda na elimu, lakini wasiojua mengi juu ya Biblia. Chombo hicho bora kimetayarishwa ili kuwapa tamaa ya kuchunguza kitabu hicho.
3 Wakati tunapoanza funzo la Biblia, lingekuwa jambo lenye manufaa kuchunguza upya madokezo bora yaliyotangazwa katika nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Julai 1996, yanayoonyesha jinsi ya kuongoza mafunzo yenye kuzaa matunda kwa msaada wa kitabu Ujuzi. Funzo linapoendelea, tutoe uangalifu kwa maendeleo ya mtu ili kutambua sehemu zinazostahili uangalifu zaidi. Tumtie moyo kujitayarisha mapema na kuchunguza maandiko ya Biblia. Majibu anayotoa katika maneno yake mwenyewe yanaweza kuonyesha shukrani ya kina kirefu kwa ajili ya ukweli. Kwa ujumla, wale wanaosoma vichapo vingine vya Sosaiti na wanaohudhuria kikawaida kwenye mikutano wanafanya maendeleo ya haraka. Tumtie mtu moyo kusema kandokando yake yale anayojifunza. Kwa wema, tumuonyeshe yale anayopaswa kufanya ili kufanya maendeleo kwa upande wa kiroho. Hatungepaswa kujifunza bila mwisho na watu wasiochukua uamuzi. Wanafunzi wangepaswa kuchukua hatua ya kujifunza, ya kuwa na msimamo ulio imara kuelekea ukweli na kufanya maendeleo kuelekea kujiweka wakfu kwa Mungu na kubatizwa.
4 Katika nyumba fulani, kuna zaidi ya funzo moja la Biblia, kwani washiriki wengi wa familia wanajifunza kila mtu siku yake mwenyewe. Hata hivyo, katika visa vingi, ingekuwa vema kuongoza funzo la familia, kwa kuwa hilo linaunganisha familia kiroho.
5 Yesu anatuamuru kufanya wanafunzi. (Mt. 28:19) Kwa hiyo, tunapaswa kuongoza mafunzo yanayochochea watu kufanya maendeleo hata wafikie kuuliza: “Ni nini chenye kunizuia nisibatizwe?”