Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 4/98 uku. 8
  • Tuingize Katika Wengine Tumaini La Uhai Wa Milele

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Tuingize Katika Wengine Tumaini La Uhai Wa Milele
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Ujuzi Utokao Kwa Mungu Unajibu Kwa Maulizo Mengi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • “Hii Yamaanisha Uhai Udumuo Milele”
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Utoaji Mbalimbali Uliopendekezwa kwa Ajili ya Utumishi wa Shambani
    Huduma Yetu ya Ufalme—2005
  • Utoaji Uliopendekezwa kwa Ajili ya Utumishi wa Shambani
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1998
km 4/98 uku. 8

Tuingize Katika Wengine Tumaini La Uhai Wa Milele

1 Ingawa mwanadamu ametafuta njia za kupunguza mwendo wa hatua za uzee na kuzidisha urefu wa maisha yake, uzee na kifo ni mambo yasiyoweza kuepukika. Sisi ni wenye shukrani kama nini kwamba Biblia inafasiria kwa nini wanadamu huzeeka na kufa, vilevile namna gani hasara za uzee zitakavyopinduliwa na kifo kuondolewa. Kweli hizi zinatolewa kwa kusadikisha katika kitabu Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Kitabu hicho kinajibu kwa wazi maswali yenye kutatanisha juu ya uhai na kifo, kikiongoza wasomaji kwenye wakati Paradiso itakaporudishwa.

2 Mnamo Aprili, tutatolea kitabu Ujuzi tukiwa na mradi wa kuanzisha mafunzo ya Biblia ya nyumbani. (Mt. 28:19, 20) Baadaye, tutafanya ziara za kurudia kwa wale wote wanaoonyesha kupendezwa na ujumbe wa Ufalme. Katika njia hiyo tutaingiza katika wengine tumaini la uhai wa milele. (Tito 1:2) Ili kutimiza hilo, utaona bila shaka madokezo yafuatayo kuwa yenye kusaidia.

 3 Wakati wa ziara ya kwanza, unaweza kuuliza swali lifuatalo:

◼ “Je! umekwisha kujiuliza kwa nini watu wanatamani maisha marefu zaidi? [Tuache mtu ajibu.] Wabudha, Wakristo, Wahindu, Waislamu, na wengine wote wana tumaini la kuishi baada ya kifo.” Tufungue kitabu Ujuzi kwenye sura 6, “Sababu Gani Tunazeeka na Kufa?” na tusome fungu 3. Tutafakari juu ya maandiko yaliyotajwa. Kwa kurejezea kwenye maswali mwishoni mwa fungu, tuulize msikilizaji ikiwa angependa kuona majibu yeye mwenyewe. Ikiwa anataka hilo, tuendelee kuzungumza juu ya mafungu machache yafuatayo. Funzo ni lenye kuanzishwa! Ikiwa sivyo, tuache kitabu kwake ili akisome na tuchukue mipango ya kurudi kuzungumza juu ya majibu, vema zaidi kisha siku moja au mbili.

 4 Wakati tunaporudi kuona mtu tuliyeachia kitabu “Ujuzi,” tungeweza kusema:

◼ “Nimerudi kuchunguza yale maswali mawili juu ya kifo ambayo tuliacha bila majibu.” Tukumbushe msikilizaji maswali yenyewe. Ndipo tuzungumzie habari katika sura 6, chini ya kichwa kidogo “Njama Yenye Uovu.” Kuhusiana na hali, labda tuendelee na funzo au tutumie swali la mwisho mwishoni mwa fungu 7 ili kuweka msingi kwa ajili ya ziara itakayofuata. Tuchukue mipango halisi ya kurudia. Tutolee msikilizaji mwaliko, na tumwelezee kwa kifupi namna mikutano inavyoendeshwa. Tumwalike kwa shauku kuhudhuria.

 5 Iwe katika mahubiri ya nyumba kwa nyumba au ushuhuda wa vivi hivi, tunaweza kuanzisha mazungumzo kwa kusema:

◼ “Je! umekwisha kujiuliza wakati ujao utakuwa nini kwetu na kwa dunia? [Tuache mtu ajibu.] Biblia inajumlisha wakati ujao katika neno moja​—Paradiso! Inafasiria kwamba mwanzoni, Mungu alifanya sehemu moja ya dunia kuwa paradiso nzuri ambamo aliweka mwanamume na mwanamke wa kwanza aliokuwa amewaumba. Ilikuwa kwamba wajaze dunia yote watu, wakiigeuza hatua kwa hatua kuwa paradiso. Ona maelezo ya jinsi ingalipaswa kufanana.” Tufungue kitabu Ujuzi kwenye ukurasa 8, na tusome fungu 9 chini ya kichwa kidogo “Uhai Katika Paradiso.” Baadaye tuzungumzie habari katika fungu 10, na tusome andiko lililotajwa, Isaya 55:​10, 11. Tupendekeze kuendeleza mazungumzo juu ya namna uhai utakavyokuwa katika Paradiso na kumaliza mafungu 11-16 pamoja. Au tumtie mtu moyo kuyasoma yeye mwenyewe, na tuchukue mipango ili kukutana tena.

 6 Ikiwa funzo halikuanzishwa wakati wa ziara ya kwanza, tungeweza kujaribu kufanya hivyo wakati wa ziara ya kurudia kwa kusema:

◼ “Kama tulivyosema wakati wa mazungumzo yetu ya nyuma, ni kusudi la Mungu kwamba dunia yote igeuzwe kuwa paradiso. Hilo linatokeza ulizo, ‘Paradiso itakuwaje?’ ” Tufungue kitabu Ujuzi kwenye sura 1, na tujifunze mafungu 11-16 chini ya kichwa kidogo “Uhai Katika Paradiso Itakayorudishwa.” Baadaye tuonyeshe picha kwenye kurasa 4-5, na tuulize mtu ikiwa angetaka kuishi katika mazingira mazuri kama hayo. Ndipo tusome sentensi ya kwanza ya fungu 17 kwenye ukurasa 10. Kulingana na hali, labda tuendelee na funzo au tuseme kwamba wakati wa ziara yetu ijayo tutafasiria yale yanayoombwa ili mtu aishi katika Paradiso itakayorudishwa. Tumwachie mwaliko, tufasirie programu ya mikutano, na tualike mtu huyo kwa shauku kuhudhuria kwenye Jumba la Ufalme.

 7  Kitabu Ujuzi ni kifaa bora cha kutumia katika kujulisha wengine juu ya “uhai udumuo milele” ulioahidiwa na Mungu. Kuongoza kwako mafunzo ya Biblia ya nyumbani pamoja na watu kunaweza kuingiza katika wengine tumaini hili tukufu lililopuliziwa na Mungu “asiyeweza kusema uwongo.”

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine