Tufaidike Na Programu Ya Shule Ya Huduma Ya Kitheokrasi Ya 1999
1 Yesu alikuwa Mwalimu Mkuu. Watu walikuwa “wenye kustaajabishwa na njia yake ya kufundisha.” (Mk. 1:22) Ingawa hakuna mmoja wetu anayeweza kusema na kufundisha kama alivyofanya Yesu, tunaweza kujitahidi kumwiga. (Mdo. 4:13) Ili kufikia mradi huo, kushiriki kwetu programu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi kutatusaidia tuendelee kufanya ustadi wetu wa kusema na kufundisha uwe bora.
2 Mnamo 1999, Hotuba Na. 1 itakuwa zaidi na msingi juu ya makala kutoka magazeti Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Uelewevu wetu wa mambo ya kiroho utaongezwa sana ikiwa tunasoma habari hiyo kimbele na kisha tuisikilize kwenye programu ya shule. Wale wanaogawiwa hotuba hizo za maagizo wanapaswa kufanya matumizi yenye manufaa ya habari, wakiitoa kwa namna yenye kupendeza na yenye uchangamfu. Kipindi Na. 3 kitakuwa na msingi juu ya kitabu Furaha ya Familia na Hotuba Na. 4 itakuwa na msingi juu ya mtu fulani wa kibiblia, ingawa chanzo kimoja cha habari chaweza kutumiwa badala ya kingine kwenye hotuba hizio. Mwangalizi wa shule anapaswa kufikiria habari kwa makini kabla ya kugawa vipindi. Wanafunzi wote wanaogawiwa kutoa habari kutoka kitabu Furaha ya Familia wanapaswa kuwa wenye mfano wa kuigwa katika maisha ya familia zao binafsi.
3 Tutumie Shauri, na Tujitayarishe Vema: Kila mmoja anaweza kufanya maendeleo zaidi katika ustadi wa kusema na kufundisha. (1 Tim. 4:13) Hivyo, tunapaswa kutafuta mashauri na tusiyaone kamwe kuwa mambo ya kuepuka. (Mez. 12:15; 19:20) Kutoa kweli kwa matokeo kwenye mikutano na katika huduma ya shambani kwaomba zaidi ya kueleza tu matukio na kusoma maandiko kijuujuu. Tunahitaji kugusa mioyo na kuchochea wale wanaotusikiliza. Tunaweza kufanya hivyo kwa kusema kweli kwa njia yenye kusadikisha kutoka moyoni mwetu. (Linganisha Matendo 2:37.) Mashauri tunayopata katika shule yatatusaidia kutimiza hilo.
4 Baada tu ya kupewa mgawo, fikiria sifa za usemi unazopaswa kuzitumika kama zinavyofasiriwa katika Kiongozi cha Shule. Fikiria yale unayohitaji kufanya ili utumie mashauri uliyopewa siku zilizopita. Tafakari kichwa cha habari yako, kikao utakachotumia ikiwa kimeombwa kwako, na jinsi utakavyotumia maandiko yanayopatikana katika habari uliyogawiwa. Fikiri juu ya jinsi ya kutumia vizuri zaidi habari ili kufundisha na kuchochea.—1 Tim. 4:15, 16.
5 Ikiwa unaogopa kujiandikisha katika shule, sali kuhusu jambo hilo na kisha uzungumze juu ya hisia zako pamoja na mwangalizi wa shule. Kila mmoja anaweza kunufaika kwa kufuata programu itakayotolewa katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi ya 1999.