Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 11/99 uku. 1
  • Mahubiri hututofautisha sisi

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Mahubiri hututofautisha sisi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Je, Una “Bidii kwa Ajili ya Kazi Njema”?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • ‘Muende Mufanye Wanafunzi Kutoka kwa Watu wa Mataifa Yote’
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2016
  • Umuige Yesu, Ukuwe na Bidii kwa Ajili ya Mahubiri
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
  • Uendelee Kuwa na Bidii Katika Kazi ya Kuhubiri
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1999
km 11/99 uku. 1

Mahubiri hututofautisha sisi

1 Watu wengi huuliza, “Ni nini kinachofanya Mashahidi wa Yehova kuwa tofauti na dini nyinginezo?” Wewe ungejibu namna gani? Ungeweza kufasiria imani zetu fulani zenye msingi juu ya Biblia. Lakini je, umefikiria pia kuonyesha kadiri ambavyo huduma yetu ya peupe hututofautisha na dini nyinginezo?​​—Mt. 24:14; 28:​19, 20.

2 Leo, watu wachache wa kidini hujisikia wenye kuchochewa kushiriki imani zao na wengine. Wanaweza kufikiri kwamba inatosha kutii sheria za Kaisari, kuishi maisha yaliyo safi kiadili, au kufanyia wengine matendo yenye wema. Walakini, hawasikii wajibu wowote wa kusaidia wengine wajifunze yale ambayo Biblia inasema kuhusu ku­pata wokovu. Sisi ni tofauti jinsi gani?

3 Huduma yetu yenye bidii ni tofauti sana na utendaji mbalimbali wa dini nyinginezo. Kwa zaidi ya miaka 100, Mashahidi wa ki-siku-hizi wamehubiri kwa bidii habari njema hadi mii­sho ya dunia, kwa kuiga Wakristo wa mapema. Kusudi letu katika kufanya hivyo ni kusaidia watu wengi iwezekanavyo wapatanishe maisha yao na mapenzi ya Mungu.​​—1 Tim. 2:4; 2 Pet. 3:9.

4 Wewe unajifanyia sifa gani? Je, wewe unajulikana kuwa mhubiri mwenye bidii wa Neno la Mungu? (Mdo. 17:​2, 3; 18:25) Kwa sababu ya utendaji wako wa kuhubiri, je, majirani wako wanaona kwa urahisi tofauti kati ya dini yao na yako? Je, unajulikana kuwa mtu aliye na hamu ya kushiriki tumaini lake pamoja na wengine? Je, unayo programu ya kawaida ya kushiriki katika huduma? Kumbuka kwamba sisi tunajitofautisha kupitia jina letu, na pia kwa kufanya kile ambacho jina hilo linamaanisha​—kwa kutoa ushahidi kuhusu Yehova.​—Isa. 43:10.

5 Upendo kwa Mungu na kwa jirani unatuchochea tujitoe katika utendaji wa kuhubiri. (Mt. 22:​37-​39) Ndiyo sababu, kama Yesu na mitume wake, sisi tunataka kufaidika na kila nafasi ili kushiriki ujumbe wa Ufalme na wengine. Acheni tuendelee kuhubiri habari njema kwa bidii kwa wale wanaotaka kusikiliza. Kufanya hivyo kutasaidia wale wenye unyofu wa moyo ‘watambue . . . katikati ya mwenye kutumikia Mungu na mutu asiyemutumikia.’​​—Mal. 3:​18.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine