Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 1/00 uku. 4
  • Tumieni trakti ili kuanzisha mazungumzo

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Tumieni trakti ili kuanzisha mazungumzo
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Tumia Trakte ili Kueneza Habari Njema
    Huduma Yetu ya Ufalme—2012
  • Neno la Mungu Liko Hai!—Ulitumie
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Trakte Mupya Zenye kuvutia Sana!
    Huduma Yetu ya Ufalme—2014
  • Uitumie Kila Wakati Unapopata Nafasi
    Huduma Yetu ya Ufalme—2010
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2000
km 1/00 uku. 4

Tumieni trakti ili kuanzisha mazungumzo

1 Je! unakubali kwamba kutoa ushahidi wenye matokeo kunategemea kwa kiasi kikubwa kuchukua kwako hatua ya kwanza ili kuanzisha mazungumzo? Mwito wa kushindania ni kusema jambo fulani lenye kuvuta kupendezwa kwa mtu na kumfanya ahusike. Lakini hilo linawezaje kufanywa kwa matokeo?

2 Wahubiri wengi wametambua kwamba kwa kutumia maneno machache yenye kuchaguliwa vizuri, kutolea watu moja ya trakti zetu zenye msingi juu ya Biblia kunaweza kuanzisha mazungumzo. Vichwa vya habari ni vyenye kuvutia, na picha ni zenye rangi na zenye kupendeza macho. Trakti haimlemei mtu, kumfanya afikiri kwamba kuna habari nyingi sana ya kusoma. Hata hivyo, ujumbe mfupi katika trakti ni wenye kuvutia na unaweza kutumiwa ili kuongoza kwenye funzo la Biblia.

3 Hivyo ndivyo Shahidi mmoja alivyohisi binafsi: “Katika ulimwengu huu wenye pirikapirika, mara nyingi watu hawapendi kuchukua wakati mwingi ili kusoma, lakini trakti ni ndefu vya kutosha ili kutoa ujumbe wa maana, lakini hizo si ndefu sana; haziwezi kukatisha watu tamaa kabla hata ya kutazama ujumbe huo. Mimi nilisoma nyingi za trakti hizo, na mwishowe nikajifunza kweli.” Usidharau kamwe nguvu ya Neno la Mungu kama linavyofasiriwa katika ujumbe huo mfupi na wenye kuchapishwa.—Ebr. 4:12.

4 Hatua nne rahisi: Wengi wamepata mafanikio kwa kutumia utangulizi mwepesi. (1) Onyesha mtu trakti chache na umwulize ile inayompendeza. (2) Baada ya mtu kuchagua moja, uliza ulizo lililotayarishwa vizuri ambalo linatia mkazo juu ya nukta kubwa katika trakti. (3) Ili kujibu ulizo, soma kutoka katika trakti fungu au andiko lenye kupatana na ulizo hilo. (4) Ikiwa unapata jibu lenye kufaa, endelea kuzungumzia yaliyomo katika trakti na ujielekeze kwa somo fulani katika broshua Anataka au sura fulani katika kitabu Ujuzi, sura ambayo inatoa maelezo zaidi. Katika njia hiyo, unaweza kuanza moja kwa moja funzo la Biblia. Madokezo yafuatayo yatakusaidia utayarishe mambo ya kusema kwa kutumia nne kati ya zile trakti.

5 Kichwa cha trakti “Ni Nani Hasa Anayeutawala Ulimwengu?” kinaweza kutokezwa kama vile ulizo.

◼ Ikiwa kwa kulijibu, mtu unayezungumza naye anasema “Mungu” au “Sijui,” soma sentensi mbili za kwanza kwenye ukurasa 2 na fungu la kwanza kwenye ukurasa 3. Tia mkazo juu ya 1 Yohana 5:19 na Ufunuo 12:9. Iwe kwamba mtu anashakia au hashakii kuwako kwa Shetani Ibilisi au kwamba anatambua uvutano wake juu ya ulimwengu, unaweza kuendelea na namna ya kufikiri inayopatikana chini ya kichwa kidogo “Dalili Katika Hali za Ulimwengu” ili kuendeleza mazungumzo. Ikiwa kupendezwa kunaonyeshwa, pendekeza kufasiria Shetani alitoka wapi, ukitumia nukta kwenye kurasa 3 na 4 za ile trakti.

6 Trakti “Kuna Tumaini Gani kwa Wapendwa Waliokufa” inaweza kuamsha kupendezwa kwa mara moja. Unaweza kuanzisha mazungumzo kwa kuuliza:

◼ “Je! unafikiri kwamba wakati wowote tutaona tena wapendwa wetu waliokufa?” Baada ya mtu kujibu, onyesha fungu la pili kwenye ukurasa 4 wa ile trakti na usome Yohana 5:28, 29. Kisha, fasiria kwamba hiyo inasaidia kuelewa habari chini ya kichwa kidogo cha kwanza katika trakti hiyo. Pendekeza kuizungumzia pamoja.

7 Trakti “Furahia Maisha ya Familia” hupendeza familia mahali pote. Kwa kuitumia, ungeweza kusema:

◼ “Bila shaka unakubali kwamba familia ni yenye kushambuliwa leo. Ni nini unafikiri kinaweza kufanywa ili kutia nguvu vifungo vya familia?” Baada ya mtu kujibu, ongoza uangalifu wake kwenye nukta mbalimbali katika fungu la kwanza kwenye ukurasa 6. Chagua moja la maandiko yanayotajwa kwenye kurasa 4 na 5 za trakti, na ufasirie kile linachomaanisha. Kisha, mtolee mtu funzo la Biblia la nyumbani bila kuomba malipo.

8 Trakti “Sababu kwa Nini Wewe Unaweza Kuitumaini Biblia” inaweza kutumiwa kwa utoaji ufuatao:

◼ “Watu wengi wamesikia hadithi kuhusu Kaini na Abeli, ambayo inapatikana katika kitabu cha kwanza cha Biblia. Simulizi katika Mwanzo linasema pia kuhusu mke wa Kaini. Je! umepata kujiuliza yeye alitoka wapi?” Tumia fungu la mwisho kwenye ukurasa 2 wa ile trakti ili kutoa jibu. Fasiria kwamba trakti hiyo inazungumzia pia maelezo ya maana ya Biblia kuhusu jinsi wakati ujao utakavyokuwa. Kwa kuanza na fungu la tatu kwenye ukurasa 5, endelea na mazungumzo, ukitumia maandiko yenye kutegemeza mawazo hayo.

9 Kugawa trakti za kibiblia ni njia yenye matokeo yaliyohakikishwa kwa muda mrefu ya kutoa habari njema. Kwa kuwa hizo ni rahisi kuchukua mahali popote unapokwenda, unaweza kuzitumia kwa matokeo katika utendaji wako wa nyumba kwa nyumba na wakati wa kutoa ushahidi wa vivi hivi. Trakti hutimiza fungu la maana katika kutimiza huduma yetu. Hakikisheni kwamba mnachukua trakti mbalimbali, na tumieni hizo kwa ukarimu ili kuanzisha mazungumzo.—Kol. 4:17.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine