Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 2/01 uku. 3-4
  • Julisheni Jina na matendo ya Yehova

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Julisheni Jina na matendo ya Yehova
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2001
  • Habari za Kufanana na Zile
  • ‘Hubiri Neno la Mungu Kikamili’
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • ‘Toa Ushahidi Kamili Kuhusu Habari Njema’
    Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Endeleeni Kutangaza Kazi za Ajabu za Yehova
    Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Tangazeni Mahali Pote Sifa Bora za Yehova
    Huduma Yetu ya Ufalme—2007
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2001
km 2/01 uku. 3-4

Julisheni Jina na matendo ya Yehova

1 “Ee shukuruni BWANA, itieni jina lake; julisheni watu matendo yake. . . . Moyo wao wanaotafuta BWANA ufurahi.” (Zab. 105:1, 3) Mtunga-zaburi aliyeandika maneno hayo alipata furaha kubwa ya kibinafsi katika kuambia wengine kuhusu Yehova na “matendo” yake. Matendo gani? Bila shaka, ni yale yanayohusiana na ufalme mtukufu wa Mungu na habari njema ya “wokovu wake.”—Zab. 96:2, 3; 145:11, 12.

2 Kadiri tunavyokaribia majira ya Ukumbusho wa mwaka wa 2001, tunazo sababu nyingi za kushangilia kuhusu matendo ya Yehova kutuelekea sisi. Namna gani hivyo? Kwa Wakristo wa kweli, Chakula cha Jioni cha Bwana, bila shaka, ndio mwadhimisho mkubwa zaidi katika mwaka. Hakuna tukio lingine lililo kama hilo kuhusiana na umaana, kusudi, au namna ya kuliendesha. Huo ni wakati kwa ajili yetu sote kukumbuka yale ambayo Yehova na Yesu walifanya ili kutayarisha njia kwa ajili ya wokovu wetu. Hakuna shaka kwamba mnamo majira ya Ukumbusho tunatazamia kwa kawaida kuona ongezeko la utendaji katika utumishi wa shambani, tukijulisha habari njema ya “wokovu”!

3 Je, utakuwa painia msaidizi? Mnamo mwezi wa Aprili uliopita, wahubiri 7,644 katika Congo-Kinshasa na 556 katika Congo-Brazzaville walijiandikisha kuwa mapainia wasaidizi; hiyo ndiyo ilikuwa hesabu ya juu kupita zote. Mwaka huu, je, tunaweza kufanya Machi na Aprili kuwa miezi ya pekee ya utendaji wenye kuongezeka katika huduma? Mwezi wa Machi una Siku za Posho tano, na mwezi wa Aprili una Siku za Yenga tano. Kwa kupanga siku nzima za utumishi kwenye miisho-juma, wahubiri wengi wanaofanya kazi ya wakati wote wametambua kwamba wanaweza kuwa mapainia wasaidizi. Ili kutimiza kiwango cha saa 50 kwa mwezi, painia msaidizi anahitaji kufanya wastani wa karibu saa 12 kwa juma. Fikiria kwa uangalifu programu zinazopendekezwa katika kisanduku kwenye ukurasa 4. Je, moja ya hizo itapatana na hali zako? Ikiwa sivyo, labda unaweza kutengeneza programu yako mwenyewe ili uwe painia msaidizi mnamo miezi ijayo ya Machi na Aprili.

4 Wazee wanapaswa sasa kuanza kujenga uthamini na tegemezo kwa ajili ya utendaji wenye kuongezeka katika utumishi. Mwaka uliopita, katika kutaniko moja ambako wazee na watumishi wa huduma wote walijiandikisha kuwa mapainia wasaidizi, 64 kati ya wale wahubiri 121 walipainia mnamo Aprili! Walifurahi pia kuona wahubiri wasiobatizwa sita wakianza kutoa ripoti mnamo Machi na Aprili. Kwa kweli, huu ndio wakati bora kwa ajili ya watoto na wapya kuuliza wazee ikiwa wanatimiza matakwa ili kuanza kushiriki katika utendaji wa peupe wa kutoa ushahidi.

5 Jitihada ya ziada huleta baraka: Makutaniko yanayojiwekea miradi ya pekee na kufanya jitihada ya pekee hufurahia baraka nyingi. Makutaniko fulani yanaweza kutia mkazo juu ya kutembelea eneo lisilotumikwa kwa ukawaida, yakikaza fikira juu ya aina za vivi-hivi za kutoa ushahidi, au yakitia mkazo juu ya kutoa ushahidi kwa njia ya simu—njia yenye matokeo ya kukutana na wale wasiokuwa nyumbani na wakaaji wasioweza kufikiwa.

6 Je, afya mbaya au uzee unapaswa kuvunja yeyote moyo asihusike zaidi iwezekanavyo katika utumishi? Hayo si maoni ya dada mmoja mwenye umri wa miaka 86 aliye na kansa. Ijapokuwa miguu yake yenye kuvimba, yeye alikuwa painia msaidizi mnamo mwezi wa Aprili uliopita. Kutoa ushahidi kwa njia ya simu kulifanya iwezekane kwake kushiriki kikamili katika utumishi, akiongeza sifa yake kwa Yehova. Jambo hilo lilikuwa na matokeo ambayo yalimchochea yeye na kutaniko.

7 Jitayarishe vizuri kwa ajili ya ukumbusho: Mwaka huu, Ukumbusho utakuwa mnamo Aprili 8. Kwa kuwa hiyo ni Siku ya Yenga, inapaswa iwezekane kwa wengi zaidi kuhudhuria. Tunaweza kuwa na hudhurio kubwa kupita wakati mwingine wowote ikiwa tunatimiza fungu letu kwa (1) kuhudhuria sisi wenyewe na (2) kualika wengine waungane nasi kwenye Ukumbusho. Ni nani tunaopaswa kualika?

8 Chunguza maandishi yako binafsi kwa ajili ya utumishi wa shambani ili kupata majina ya wale ambao kwa kiasi fulani walionyesha kupendezwa na kweli, hata kama huenda ikawa hauwatembelei kwa ukawaida. Majuma mawili au matatu kabla ya Ukumbusho, kaza fikira juu ya kutembelea hao wote na kuwatolea mwaliko kwa ajili ya Ukumbusho. Ikiwa hali zako zinaruhusu, pendekeza kutayarisha usafirishaji kwa ajili ya wale wanaotaka kuhudhuria.

9 Katika makutaniko fulani, vikaratasi vya mwaliko vilivyochapishwa kwa ajili ya Ukumbusho havitumiwi vyote. Waandishi wa makutaniko wanapaswa kuwa hakika kwamba wanafanya vikaratasi vya mwaliko vipatikane pa wakati wenye kufaa kusudi vyote vifanyiwe ugawaji. Huenda ukataka kuandika kwa mashini au kuchapa vizuri wakati na mahali pa Ukumbusho kwenye sehemu ya chini ya kikaratasi cha mwaliko. Au huenda ukatia ndani kikaratasi cha mwaliko kinachoonyesha anwani ya Jumba la Ufalme ikiwa hapo ndipo mtakapofanyia Ukumbusho. Acheni tukumbushe kwamba, katika hali zilizo nyingi, vikaratasi vya mwaliko kwa ajili ya Ukumbusho vinapaswa kutolewa kwa mwenye-nyumba kibinafsi.

10 Kumbukeni wale wasiotenda: Ni jambo la kufurahisha wakati mwanafunzi wa Biblia anapojiweka wakfu kwa Yehova na kuonyesha hilo kwa kuzamishwa majini. Hata hivyo, kila mwaka, wengine kati yetu huacha kushirikiana nasi, nao huacha kuambia wengine kuhusu jina na matendo ya Yehova. Tunayo sababu nzuri ya kuhangaishwa. Ingawa walio wengi kati ya wale wasiotenda hawakuacha kweli, huenda wakawa wameacha kuhubiri kwa sababu ya kuvunjika moyo, matatizo ya kibinafsi, au mahangaiko mengine ya maisha. (Mt. 13:20-22) Wengine walio katika hali dhaifu ya kiroho wanahitaji msaada ili kurudi katika kutaniko kabla ya kumezwa na mfumo wa Shetani. (1 Pet. 5:8) Mnamo majira haya ya Ukumbusho, tunataka kufanya jitihada ya pekee ili kusaidia wasiotenda ambao wanatimiza matakwa ili kushiriki tena katika kutangaza habari njema.

11 Mwandishi wa kutaniko anapaswa kujulisha viongozi wa funzo la kitabu kuhusu yeyote ambaye amekuwa asiyetenda katika kikundi chao. Halmashauri ya Utumishi ya Kutaniko itachukua uongozi katika kufanya mipango ili ziara za uchungaji zifanywe kwa wale wasiotenda. Ikiwa inaamuliwa kwamba mtu asiyetenda anaweza kufaidika na funzo la Biblia la kibinafsi, halmashauri ya utumishi inapaswa kuamua ni nani anayestahili zaidi kuongoza funzo hilo. Ingawa huenda funzo lisihitaji kuendeshwa kwa muda mrefu, yule anayepewa mgawo wa kuliongoza anaweza kuripoti wakati, ziara za kurudia, na funzo la Biblia.

12 Mnamo mwezi wa Aprili uliopita, dada mmoja ambaye alikuwa akifanya kazi ya nyumba kwa nyumba alipendekeza magazeti kwa mwanamume mmoja kijana barabarani. Mwanamume huyo akamfunulia kwamba mke wake ni Shahidi asiyetenda. Akauliza mahali ambapo Jumba la Ufalme lilipatikana na akaalika dada huyo awatembelee, yeye na mke wake. Kama tokeo, wenzi hao wa ndoa wakahudhuria mkutano uliofuata, nao wakakubali funzo la Biblia.

13 Jitayarishe kwa ajili ya utendaji wenye kuongezeka! Mtunga-zaburi aliyesema kwamba tunapaswa kujulisha jina na matendo ya Yehova aliongeza: “Mumwimbie, mumwimbie sifa; fikilini kazi zake zote za ajabu. Mujisifu kwa jina lake takatifu.” (Zab. 105:2, 3) Acheni tuonyeshe kwamba tunahangaikia jina kuu la Yehova na “kazi zake za ajabu” kwa kuongeza jitihada zetu katika huduma, tukifanya majira haya kuwa majira makubwa zaidi ya Ukumbusho!

[Box on page 4]

Njia Mbalimbali za Kupanga Saa 12 kwa Juma ili Kuwa Painia Msaidizi

Siku Saa

Siku ya Kwanza 1 2 − −

Siku ya Pili 1 − 3 −

Siku ya Tatu 1 2 − 5

Siku ya Nne 1 − 3 −

Siku ya Tano 1 2 − −

Siku ya Posho 5 4 3 5

Siku ya Yenga 2 2 3 2

Jumla: 12 12 12 12

Je, moja ya programu hizi itatumika kwa ajili yako? Ikiwa sivyo, kwa nini usifanye programu yako mwenyewe?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine