‘Weka Kando Kitu Fulani’
Katika kutaniko la Kikristo la mapema, kulikuwa mahitaji ya kimwili yaliyoomba kutolewa uangalifu. Kulingana na jinsi kila mtu alivyofanikiwa, aliombwa “aweke kando kitu fulani” kuwa mchango ili kutimiza mahitaji hayo. (1 Kor. 16:1-3) Kama tokeo la ukarimu wao, wote walishangilia kwa kutoa “maonyesho mengi ya shukrani kwa Mungu.”—2 Kor. 9:11, 12.
Leo, kazi ya ulimwenguni pote ya watu wa Yehova inaendelea kupanuka, nayo inaomba utegemezo mwingi zaidi wa kifedha. Ni jambo lenye kufaa kwamba sisi pia ‘tuweke kando kitu fulani’ kwa ukawaida ili kusaidia kutimiza uhitaji huo. (2 Kor. 8:3, 4) Utoaji wa kimwili unaweza kufanywa kwa njia mbalimbali. (Ona Mnara wa Mlinzi wa Novemba 1, 2001, ukurasa wa 28-9.) Kwa njia yenye kufaa, tunaona hilo kuwa pendeleo linaloleta furaha ya kweli.—Mdo. 20:35.