Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 5/02 uku. 5
  • Tosheleza Uhitaji Wako wa Kiroho

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Tosheleza Uhitaji Wako wa Kiroho
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Habari za Kufanana na Zile
  • ‘Sikilizeni na Mwongezewe Elimu’
    Huduma Yetu ya Ufalme—2001
  • Sikiliza na Ujifunze
    Huduma Yetu ya Ufalme—2013
  • Makusanyiko ya Wilaya 1999 “Neno la Unabii la Mungu”
    Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • “Wajumbe wa Amani ya Kimungu”—Kusanyiko la Wilaya 1996
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2002
km 5/02 uku. 5

Tosheleza Uhitaji Wako wa Kiroho

1 Mkusanyiko wetu wa Wilaya unaokuja wenye kichwa “Watangazaji Wenye Bidii wa Ufalme” unatutolea nafasi nzuri ajabu ya kutosheleza uhitaji wetu wa kiroho. Kama vile chakula cha kimwili chenye kufaa, programu ya mkusanyiko itatulisha kiroho “maneno ya imani.” (1 Tim. 4:6) Itatuwezesha kumkaribia Yehova zaidi. Na tunaweza kutazamia kupokea shauri na kitia-moyo ili kutusaidia kukabiliana na majaribu maishani mwetu. Yehova anatuhakikishia: “Nitakufundisha na kukuonyesha njia utakayokwenda; nitakushauri na jicho langu likikutazama.” (Zab. 32:8) Tunabarikiwa kama nini kuwa na mwongozo wake wenye upendo maishani mwetu! Fikiria hatua zenye kufaa tunazoweza kuchukua ili kufaidika zaidi na programu ya mkusanyiko.

2 Tunahitaji Kutayarisha Moyo Wetu: Kila mmoja wetu ana daraka la kulinda moyo wake wa mfano. (Mez. 4:​23) Hilo linaomba tujitie adabu na kuwa wanyofu kuhusu hisia zetu wenyewe. Mkusanyiko ni wakati wa kutafakari kuhusu uhusiano wetu pamoja na Yehova, wakati wa ‘kuchungua ndani ya sheria kamilifu iliyo ya uhuru.’ Ili kutayarisha moyo wetu kusudi ‘upokee kupandwa kwa neno,’ tunapaswa kumwomba sana Yehova atuchunguze, aone ndani yetu “njia yo yote ya uovu” inayohitaji kusahihishwa, na atuongoze “katika njia ya milele.”​—Yak. 1:​21, 25; Zab. 139:​23, 24.

3 Sikiliza na Utafakari: Yesu alimsifu Maria kwa kusikiliza kwa ukaribu maneno yake; alisema: “Maria alichagua fungu jema, nalo halitaondolewa mbali naye.” (Luka 10:​39, 42) Ikiwa tuna mwelekeo huohuo wa kiakili, hatutaruhusu mambo ya ovyoovyo yatukengeushe. Tutahakikisha kwamba tunakaa na tunasikiliza muda wa programu nzima. Tutaepuka kuongea-ongea na kutembea-tembea isivyohitajiwa, na tutakuwa waangalifu ili tusikengeushe wengine kupitia simu ndogo, kamera za kupiga picha, na kamera za kurekodi kwenye vidio-kaseti.

4 Tunaposikiliza hotuba, ni vizuri tuchukue maandishi mafupi ili kutusaidia tuchanganue jinsi habari inavyozungumziwa. Tunapaswa kuunganisha yale tunayosikia na yale tunayojua tayari. Hilo litatusaidia kuelewa na kushikilia habari. Tunaporudilia maandishi yetu, tunapaswa kufanya hivyo tukiwa na mradi wa kutumikisha habari yenyewe. Kila mmoja wetu anaweza kujiuliza: ‘Jambo hili lina matokeo gani juu ya uhusiano wangu pamoja na Yehova? Ni mabadiliko gani ninayohitaji kufanya maishani mwangu? Ninaweza kutumiaje habari hii kuhusiana na jinsi ninavyoshughulika na wengine? Ninaweza kuitumiaje katika huduma yangu?’ Zungumza na wengine kuhusu nukta unazofurahia kipekee. Kufanya mambo hayo kutatusaidia katika kulinda maneno ya Yehova ‘ndani ya moyo wetu.’​—Mez. 4:​20, 21.

5 Acheni Tutumikishe Yale Tunayojifunza: Baada ya kuhudhuria mkusanyiko wa wilaya, mjumbe mmoja alisema: “Programu ilihusu kila mtu binafsi, ikimchochea achunguze hali ya moyo wake na ile ya washiriki wa familia yake, na kutoa msaada wenye upendo na wa Kimaandiko unaohitajiwa. Imenifanya nitambue zaidi wajibu wangu wa kusaidia kutaniko zaidi.” Yaelekea wengi wetu tumehisi hivyohivyo. Lakini haitoshi tu kutoka kwenye mkusanyiko tukiwa wenye kutiwa moyo na wenye kuburudishwa. Yesu alisema: “Ikiwa mwajua mambo haya, wenye furaha ni nyinyi ikiwa mwayafanya.” (Yn. 13:​17) Tunapaswa kwa bidii kutumikisha nukta zinazotuhusu kibinafsi. (Flp. 4:9) Huo ndio ufunguo wa kutosheleza kikamili uhitaji wetu wa kiroho.

[Picture on page 5]

Tafakari Yale

Unayosikia:

[Picture on page 5]

■ Hilo lina matokeo gani juu ya uhusiano wangu pamoja na Yehova?

■ Lina uvutano gani juu ya jinsi ninavyoshughulika na wengine?

■ Ninawezaje kulitumikisha katika maisha yangu na huduma yangu?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine