Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Julai 15
“Ikiwa tukio kama hili [linaloonyeshwa kwenye kifuniko cha gazeti hili] liliripotiwa katika vyombo vya habari vya siku zetu, huenda watu wengi zaidi wangetilia shaka. Unafikiri nini? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Marko 4:39.] Tuna uhakikisho gani wa kwamba miujiza ambayo Yesu alifanya ilikuwa ya kweli? Toleo hili la Mnara wa Mlinzi linazungumzia jambo hilo.”
Amkeni! Julai 22
“Katika ulimwengu wa leo, wahalifu ni wenye kutunga kila wakati mipango mipya yenye njama ili kuwadanganya watu wasio waangalifu. Je, jambo hilo linakutia wasiwasi? [Acha mtu ajibu.] Toleo hili la Amkeni! linazungumzia mambo machache ya msingi yanayohusu uangalifu, mambo yanayoweza kutusaidia kujilinda na mambo ya udanganyifu.” Soma Methali 22:3.
Mnara wa Mlinzi Ago. 1
“Kwa kuwa wanadamu wanagawanyika sana, watu wengine wanafikiri kwamba njia moja tu ili kuleta amani ulimwenguni ni kupitia serikali moja ya ulimwenguni. Je, unafikiri kwamba jambo hilo linawezekana? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Danieli 2:44.] Gazeti hili linazungumzia yale ambayo Ufalme wa Mungu unatimiza sasa na jinsi utaleta amani ulimwenguni hivi karibuni.”
Amkeni! Ago. 8
“Sisi wote tunahuzunika tunaposikia kuhusu kutumia watoto vibaya. Huenda umewahi kujiuliza, ‘Je, kweli Mungu anajali?’ [Acha mtu ajibu. Kisha soma Zaburi 72:12-14.] Makala hii inazungumzia jinsi Mungu anavyojisikia kuhusu watoto na jinsi atakavyoleta hivi karibuni kitulizo chenye kudumu kwa wote wanaotendewa vibaya.”