Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi 01/01/08
“Je, unaweza kukubaliana na maneno yanayosemwa katika andiko hili? [Soma Yakobo 3:2.] Habari hii inatoa mapendekezo fulani ya Biblia yenye kufaa ili kutusaidia tuepuke kuumiza washiriki wa familia kupitia usemi wetu.” Onyesha habari inayoanzia kwenye ukurasa wa 10.
Amkeni! Mwezi wa 1
“Kila ndoa ina magumu. Unafikiri mume na mke wanaweza kupata wapi mashauri yenye kutumainika? [Acha mtu ajibu.] Ona mwongozo huu wenye kufaa. [Soma Waefeso 5:22, 25.] Habari hii inafasiria jinsi mke anavyoweza kujitiisha kwa mume wake.” Onyesha habari inayoanzia kwenye ukurasa wa 28.
Mnara wa Mlinzi 01/02/08
“Kwa kuwa tunapatwa na magumu mengi leo, je, unafikiri kwamba inawezekana kupata amani ya kweli ya akilini? [Acha mtu ajibu.] Kufikiria tumaini la Biblia kuhusu wakati ujao kumesaidia watu wengi. [Soma andiko moja kati ya yale yaliyotajwa ao yaliyorudiliwa moja kwa moja katika habari unayotaka kukazia.] Gazeti hili linaonyesha yale ambayo Biblia inasema kuhusu mahali ambapo tulitoka, kusudi la maisha, na tumaini la wakati ujao.”
Amkeni! Mwezi wa 2
“Kwa kuwa uovu umeongezeka, watu wengi wanakosa usalama. Je, unafikiri kwamba hali zitakuwa nzuri wakati fulani? [Acha mtu ajibu.] Ona unabii huu wa Biblia wenye kupendeza. [Soma Zaburi 37:10.] Gazeti hili linazungumzia sababu kubwa ya uovu na yale Biblia inasema kuhusu jinsi ambavyo tatizo hilo litamalizwa.”