Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi 01/02/08
“Unafikiri familia zinaweza kufaidika namna gani ikiwa zinafuata shauri lililo katika andiko hili? [Soma Waefeso 4:31. Kisha acha mtu ajibu.] Habari hii inatoa mapendekezo fulani ya Biblia yanayofaa ili kuepuka ugomvi na kuendelea kuwa na furaha katika ndoa.” Onyesha habari inayoanzia kwenye ukurasa wa 18.
Amkeni! Mwezi wa 2
“Watu fulani wanafikiri kwamba Mungu anaandika kila kosa tunalofanya. Wengine wanafikiri kwamba anasamehe zambi zote, hata ziwe nzito kadiri gani. Wewe unafikiri nini? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Matendo 3:19.] Habari hii inazungumzia hatua tatu zinazoonyeshwa katika Biblia ili kusamehewa na Mungu.” Onyesha habari inayoanzia kwenye ukurasa wa 10.
Mnara wa Mlinzi 01/03/08
“Ningependa nijue maoni yako kuhusu andiko hili lenye kujulikana sana. [Soma Yohana 3:16.] Je, umepata kujiuliza namna gani kifo cha mtu mmoja kiliweza kuletea wengine uzima wa milele? [Acha mtu ajibu.] Gazeti hili linatoa maelezo yaliyo wazi na yenye kutosheleza kuhusu jinsi tunavyoweza kufaidika kutokana na kifo cha Yesu.”
Amkeni! Mwezi wa 3
“Je, unafikiri kwamba dini zote ni nzuri? [Acha mtu ajibu.] Ona yale ambayo Biblia inasema kuhusu ibada ya watu fulani. [Soma Marko 7:7.] Namna gani mtu anaweza kujua ikiwa dini fulani inafundisha kweli wala si ‘amri za wanadamu’? Je, tunaweza kupata dini inayofundisha kweli? Gazeti hili linajibu maulizo hayo.”