Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Feb. 15
“Ikiwa ungeweza kuchagua mtu fulani ili atawale ulimwengu, ungechagua nani? [Acha mtu ajibu.] Toleo hili la Mnara wa Mlinzi linazungumzia mambo yanayomtambulisha Masihi, yeye ambaye Mungu amechagua ili kutawala dunia. Linaeleza pia yale ambayo utawala wake utamaanisha kwa wanadamu.” Soma Isaya 9:6, 7.
Amkeni! Feb.
“Kuna miungu mingi ambayo watu wanaabudu leo. Hata hivyo, ona yale ambayo Yesu alisema katika sala kuhusu Baba yake aliye mbinguni. [Soma Yohana 17:3.] Ikiwa kuna Mungu wa pekee wa kweli mmoja tu, tuseme nini kuhusu miungu mingine yote? [Acha mtu ajibu.] Habari hii inatoa maoni ya Biblia.” Onyesha habari kwenye ukurasa wa 28-29.
Mnara wa Mlinzi Mac. 1
“Watu walio wengi wanakubali kwamba tunapaswa kupendana, kama vile Yesu alivyoamuru katika andiko hili. [Soma Yohana 13:34, 35.] Lakini, ni wapi tunakoweza kupata watu wanaotii mafundisho ya Yesu katika maisha zao? [Acha mtu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia jinsi tunavyoweza kutambua Wakristo wa kweli leo.”
Amkeni! Mac.
“Upendo ni wa maana sana ili kuwa wenye furaha na wenye hali njema. Lakini, watu wengi wanafikiri kwamba ni vigumu kupata upendo wa kweli. Kwa nini unafikiri kwamba ni hivyo? [Acha mtu ajibu.] Siri moja ya kupata upendo wa kweli ni kujifunza kuonyesha wengine upendo usio wa kibinafsi. Gazeti hili linazungumzia yale ambayo hilo linahusisha.” Soma 1 Wakorintho 13:4-7.