Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
MNARA WA MLINZI Feb. 15
“Watu fulani hujiuliza ikiwa kuna Mungu ambaye ni mtu halisi. Wengine wanasema kwamba yuko lakini wanafikiri kwamba yuko mbali nao. Je, umetambua hilo? [Acha mtu ajibu.] Ona kwa nini kupata kumjua Mungu kibinafsi ni jambo la maana sana. [Soma Yohana 17:3.] Kuhusiana na habari hii, utaona makala za utangulizi katika toleo hili kuwa zenye kupendeza.”
Amkeni! Feb. 22
“Je, unafikiri kwamba Mungu alikusudia kwamba wanadamu, kutia na watoto, wateseke kutokana na utapiamlo? [Acha mtu ajibu.] Ona ahadi hii yenye kufariji inayopatikana katika Biblia. [Soma Zaburi 72:16.] Toleo hili la Amkeni! linazungumzia sababu zinazoleta utapiamlo na, jambo la maana zaidi, ahadi ya Mungu ya kuumaliza karibuni.”
MNARA WA MLINZI Machi 1
“Tungependa kujua maoni yako kuhusu andiko hili lenye kupendeza. [Soma Mathayo 5:10.] Mtu anawezaje kuwa mwenye furaha wakati anapokuwa mwenye kunyanyaswa? [Acha mtu ajibu.] Makala mbili za kwanza katika gazeti hili zinazungumzia watu fulani waliodumisha furaha ijapokuwa mateso yao. Utapendezwa kusoma jinsi walivyofanya hivyo.”
Amkeni! Machi 8
“Je, hautakubali kwamba ijapokuwa matatizo ya maisha bado tuna sababu ya kuwa wenye shukrani? [Acha mtu ajibu.] Sababu moja ya kuwa wenye shukrani ni namna tulivyoumbwa. [Soma Zaburi 139:14.] Tunaweza kuwa wenye shukrani kama nini kwa kuwa na hisi tunazohitaji ili kuthamini maisha, kama toleo hili la Amkeni! linavyoeleza!”