Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Feb. 15
“Watu wengi ni wenye kuvurugwa na yale mambo mabaya ambayo yametendwa kwa jina la dini. Watu fulani wanafikiri kwamba dini ndiyo inasababisha matatizo ya wanadamu. Je, umepata kujiuliza kuhusu jambo hilo? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Ufunuo 18:24.] Gazeti hili linazungumzia yale Biblia inasema kuhusu habari hiyo.”
Amkeni! Feb. 22
“Watu wengi wanafurahia kujifunza kuhusu maisha ya wanyama, na wengine wanafurahia kuwafuga nyumbani. [Acha mtu atoe maelezo.] Gazeti hili linazungumzia matatizo ya kufuga mnyama. Linaeleza pia ahadi ya Mungu kuhusu wakati ambapo wanyama wote wataishi kwa amani pamoja na wanadamu na pia wao kwa wao.” Soma Isaya 11:6-9.
Mnara wa Mlinzi Mac. 1
“Pindi fulani, Yesu Kristo aliulizwa: ‘Ni amri gani iliyo ya kwanza kati ya zote?’ Sikiliza jibu lake. [Soma Marko 12:29, 30.] Je, umewahi kujiuliza kile ambacho Yesu alimaanisha? [Acha mtu ajibu.] Makala ‘Jinsi Tunavyoonyesha Upendo Wetu kwa Mungu’ inazungumzia maana ya maneno hayo yenye kujulikana sana.”
Amkeni! Mac. 8
“Wakati fulani, watu wengi waliishi katika woga wa vita ya kinyukilia. Je, unafikiri kwamba vita ya kinyukilia inawezekana leo? [Acha mtu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia maendeleo ya kisasa yanayotutia sisi wote wasiwasi. Linaeleza pia ahadi ya Biblia kuhusu ulimwengu ambamo woga hautakuwa tena.” Soma Sefania 3:13.