Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Feb. 15
“Mara kwa mara tunasikia ripoti zinazodai kwamba muujiza fulani umetendeka. [Taja mfano mmoja.] Watu wengine wanaamini ripoti hizo. Wengine wanatilia shaka. Gazeti hili linazungumzia ikiwa miujiza inayoripotiwa katika Biblia ilitokea kweli na ikiwa mambo kama hayo yanatendeka leo.” Soma Yeremia 32:21.
Amkeni! Feb. 22
“Wakati wa zamani, Mungu aliamuru watoto kuheshimu mama zao na baba zao pia. [Soma Kutoka 20:12.] Je, unawaza kwamba mama ni wenye kuheshimiwa ifaavyo leo? [Acha mtu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia matatizo ambayo mama katika nchi mbalimbali wanapambana nayo na jinsi wanavyoshughulikia matatizo hayo.”
Mnara wa Mlinzi Mac. 1
“Je, unafikiri kwamba dunia ingekuwa mahali bora ikiwa kila mmoja angetumia shauri hili? [Soma Waroma 12:17, 18. Kisha acha mtu ajibu.] Kwa kusikitisha, tofauti za kiutu mara kwa mara zinatokea. Gazeti hili linaonyesha jinsi kutumia shauri la Biblia kunavyoweza kutusaidia kutatua magomvi na kufanya amani.”
Amkeni! Mac. 8
“Kila mwaka, ombi la nishati (énergie) linaongezeka. Je, unaweza kuwazia jambo linaloweza kutokea ikiwa siku moja nishati tunayohitaji inakwisha? [Acha mtu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia maendeleo ambayo yamefanywa katika kusitawisha vyanzo vya nishati visivyochafua. Inatambulisha pia Chanzo cha nishati yote.” Soma Isaya 40:26.