Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi 15/02/07
“Watu fulani wanafikiri kwamba mwanadamu ni mwenye kuiharibu dunia. Je, jambo hilo linakuogopesha? [Acha mtu ajibu.] Ona ahadi hii yenye kutuliza moyo. [Soma Ufunuo 11:18.] Gazeti hili linatoa habari kuhusu mambo yanayofanya dunia iwe sayari (planeti) ya pekee. Linaonyesha pia yale ambayo Biblia inasema kuhusu jinsi dunia hii itakavyokuwa wakati ujao.”
Amkeni! Mwezi wa 2
“Je, unafikiri kwamba sababu hii ndio inayofanya kuwe na matatizo mengi katika ulimwengu? [Soma 1 Yohana 5:19. Kisha acha mtu ajibu.] Habari hii inazungumzia yale ambayo Biblia inasema kuhusu ‘yule mwovu’ na jinsi ambavyo tunaweza kuepuka uvutano wake wenye nguvu.” Onyesha habari inayoanzia kwenye ukurasa wa 12.
Mnara wa Mlinzi 01/03/07
“Watu wengi wanafikiri kwamba dini zote zinaongoza watu kwa Mungu. Je, unafikiri kwamba mtu anaweza kuchagua dini yoyote anayopenda? [Acha mtu ajibu.] Ona pendekezo hili. [Soma 1 Yohana 4:1.] Gazeti hili linazungumzia jinsi tunaweza kuchunguza mafundisho ili kuona kwamba yanatoka kwa Mungu. Linazungumzia pia jinsi dini fulani zilivyoanzishwa.”
Amkeni! Mwezi wa 3
“Kulingana na maoni yako, ni matatizo gani yanayowapata vijana leo? [Acha mtu ajibu.] Andiko hili linaonyesha moja kati ya matatizo hayo—yaani, jinsi ya kupata marafiki wazuri. [Soma Methali 13:20.] Gazeti hili linazungumzia hatari za kutumia internet ili kupata marafiki na jinsi vijana wanavyoweza kujilinda na hatari hizo.”