‘Hii Habari Njema Itahubiriwa’!
1. Tunajua namna gani kwamba hakuna jambo lolote linaloweza kuzuia kazi ya kuhubiri isitimizwe?
1 Kwa kweli, hakuna jambo lolote linaloweza kumzuia Yehova asitimize mapenzi yake. (Isa. 14:24) Hata ikiwa lilionekana kuwa jambo lisilowezekana Mwamuzi Gideoni na wanaume wake 300 kushinda jeshi la Wamidiani la wanaume 135,000, Yehova alimwambia hivi: “Hakika utawaokoa Israeli kutoka mkono wa Midiani. Je, si mimi ninayekutuma?” (Amu. 6:14) Ni kazi gani inayotegemezwa na Yehova leo? Yesu alisema hivi: “Hii habari njema ya ufalme itahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa.” (Mt. 24:14) Hakuna mutu yeyote anayeweza kuzuia kazi hiyo isitimizwe!
2. Kwa nini tunaweza kutazamia kwamba Yehova atamsaidia kila mmoja wetu anapohubiri?
2 Yehova Anasaidia Kila Mmoja Wetu: Ijapokuwa tunaweza kuwa hakika kwamba Yehova atasaidia Mashahidi wake wakiwa kikundi, je, tunaweza kutazamia kwamba atasaidia kila mutu kipekee? Alipokuwa katika uhitaji, mtume Paulo aliona kwamba Yehova alimtegemeza kupitia Mwana wake, Yesu. (2 Tim. 4:17) Sisi pia tunaweza kuwa hakika kwamba Yehova atambariki kila mmoja wetu anapojikaza kutimiza mapenzi yake.—1 Yoh. 5:14.
3. Yehova anatusaidia katika hali gani?
3 Je, shuguli za maisha za kila siku zinakuchokesha hivi kwamba unakosa nguvu ya kuhubiri? “Anampa nguvu mtu aliyechoka.” (Isa. 40:29-31) Je, wewe ni mwenye kuvumilia mateso ao upinzani? “Mtupie Yehova mzigo wako, naye mwenyewe atakutegemeza.” (Zab. 55:22) Je, nyakati fulani unajiona haustahili kuhubiri? “Nenda, nami nitakuwa pamoja na kinywa chako.” (Kut. 4:11, 12) Je, una matatizo ya afya yanayokufanya usishiriki zaidi katika mahubiri? Yehova anapendezwa na kazi unayofanya kwa nafsi yote na anaweza kuitumia, hata iwe ndogo kadiri gani.—1 Kor. 3:6, 9.
4. Kumtegemea Yehova kutatusaidia namna gani?
4 Mkono wa Yehova “umenyooshwa, na ni nani anayeweza kuurudisha nyuma?” (Isa. 14:27) Kwa kuwa tuna uhakika kwamba Yehova anabariki kazi yetu, acheni basi tuendelee kuhubiri bila kuacha “kwa ujasiri kwa mamlaka ya Yehova.”—Mdo. 14:3.