Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi 01/06/10
“Watu wengi wanafanya uaguzi kwa kutumia nyota mbele ya kufanya maamuzi. Je, unafikiri kwamba nyota zinaweza kuongoza maisha yetu? [Acha msikilizaji ajibu.] Jambo la kujua ni kwamba Biblia inazungumzia elimu ya nyota. [Soma 2 Wafalme 23:5.] Habari hii inatoa maoni ya Biblia.” Onyesha habari inayoanzia kwenye ukurasa wa 18.
Amkeni! Mwezi wa 6
“Mara nyingi makanisa yanaomba feza ili mutu abatizwe, wakati mutu anapenda kufanya ndoa na pia sherehe ya mazishi. Unawaza kwamba ni vizuri kufanya hivyo? [Acha mutu ajibu.] Angalia maagizo haya ambayo Yesu alitolea wanafunzi wake. [Soma Mathayo 10:7, 8b.] Habari hii inaonyesha kile Biblia inasema kuhusu kuomba feza kwa ajili ya mambo ya kidini.” Onyesha habari iliyo kwenye ukurasa wa 22.
Mnara wa Mlinzi 01/07/10
“Watu wengi wanawaza kwamba Mungu anaitwa tu Mweza-Yote. Lakini, ulijua kwamba Biblia inatujulisha jina la Mungu? [Acha mutu ajibu. Kisha soma Isaya 42:8a.] Gazeti hili linaeleza kwa nini jina la Mungu limeondolewa katika Biblia fulani na inamaanisha nini kumjua Mungu kwa jina lake.”
Amkeni! Mwezi wa 7
“Uchumi (économie) umehangaisha watu sana. Wale wasio na kazi wanasumbuliwa sana, na wale wanaofanya kazi wanaogopa wasipoteze kazi yao. Je, unawaza kwamba shauri hili linaweza kutusaidia tupambane na hali hiyo? [Soma Mathayo 6:34. Kisha acha mutu ajibu.] Gazeti hili linatoa mashauri fulani ili kujua jinsi ya kupambana na mambo ya feza na kujua jinsi ya kuwa wenye kutulia kiakili.”