Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 1/11 uku. 1
  • Kazi Yenye Kufurahisha Zaidi

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kazi Yenye Kufurahisha Zaidi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Unaweza Kusaidia mu Kazi ya Kufanya Wanafunzi?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2021
  • Namna ya Kusaidia Wanafunzi wa Biblia Wafikie Kubatizwa—Sehemu ya Pili
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
  • Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo
    Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo
    Huduma Yetu ya Ufalme—2005
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2011
km 1/11 uku. 1

Kazi Yenye Kufurahisha Zaidi

1. Ni kazi gani ya kuwaponya watu kiroho inayofanywa katika siku zetu?

1 Katika karne ya kwanza, wale walioona jinsi watu walivyokuwa wakiponyeshwa kimwili walifurahi sana. (Luka 5:24-26) Katika siku zetu, tunafurahi sana tunaposhiriki katika kazi ya kuwaponya watu kiroho. (Ufu. 22:1, 2, 17) Inafurahisha kabisa kusoma mambo yaliyoonwa kuhusu jinsi Neno la Yehova na roho takatifu yake vinavyobadili maisha ya watu! Hata hivyo, kushiriki katika kazi hiyo kwa kuongoza mafunzo ya Biblia yenye kufanya maendeleo ndilo jambo lenye kufurahisha zaidi.

2. Ni furaha gani tunayoweza kupata tunapomfundisha mutu kweli?

2 Jina la Mungu ni nani? Kwa nini Mungu anaruhusu watu wateseke? Ufalme wa Mungu utawafanyia wanadamu nini? Tunapata furaha tunapojibu maulizo hayo na tunapoona jinsi mwanafunzi anavyofurahi anapojifunza ile kweli. (Met. 15:23; Luka 24:32) Mwanafunzi anapofanya maendeleo, anaweza kuanza kutumia jina la Yehova, kuanza kufanya mabadiliko katika namna yake ya kuvaa na kujipamba, kuacha mazoea mabaya, na kutolea wengine ushahidi. Ikiwa anafikia kujiweka wakfu na kubatizwa, atakuwa ndugu yetu na mfanyakazi mwenzetu. Mwanafunzi anapofanya maendeleo hayo hatua kwa hatua, jambo hilo linatufurahisha kabisa.​—1 The. 2:19, 20.

3. Ni hatua gani zenye kufaa tunazoweza kufanya ili kuanzisha funzo la Biblia?

3 Je, Unaweza Kushiriki Katika Kazi Hiyo? Ikiwa unapenda kushiriki katika kazi hiyo yenye kufurahisha zaidi, umwombe Yehova akusaidie kupata funzo la Biblia, na kisha utende kulingana na sala yako. (1 Yoh. 5:14) Hubiri wakati na mahali unapoweza kupata watu. Anzisha funzo la Biblia kila wakati unapopata nafasi inayofaa. (Mhu. 11:6) Unapopata mutu mwenye kupendezwa na unapopanda mbegu ya kweli, urudi ili kuitilia maji.​—1 Kor. 3:6-9.

4. Kwa nini tutambue uhitaji wa kutenda kwa haraka tunapoanzisha mafunzo ya Biblia?

4 Kuna watu wengi sana ambao bado wana njaa na kiu cha uadilifu. Ni nani atajifunza nao Biblia ili kuwasaidia kutosheleza mahitaji yao ya kiroho? (Mt. 5:3, 6) Acheni tujitolee kabisa ili kusaidia kumalizia kazi ya kuhubiri na kufanya wanafunzi mbele mavuno yafikie mwisho.​—Isa. 6:8.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine