Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 3/11 uku. 3
  • Je, Ulikuwa Painia wa Kawaida Hapo Mbele?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Je, Ulikuwa Painia wa Kawaida Hapo Mbele?
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Je, Unaweza Kuingia Katika “Mlango Mkubwa Unaoongoza Kwenye Utendaji”?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2007
  • “Unaweza Kuwa Painia Kabisa!”
    Huduma Yetu ya Ufalme—2010
  • Utumishi Wa Painia: Je! Ni Wako?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Sasa Ndio Wakati wa Kuhubiri!
    Huduma Yetu ya Ufalme—2005
Huduma Yetu ya Ufalme—2011
km 3/11 uku. 3

Je, Ulikuwa Painia wa Kawaida Hapo Mbele?

1. Ni pendeleo gani ambalo wengi wamekuwa nalo, lakini wengine wamelazimika kufanya nini?

1 Ndugu na dada wengi wamefurahia kwa miaka mingi pendeleo la “kufundisha na kutangaza habari njema” kama watumishi wa wakati wote. (Mdo. 5:42) Hata hivyo, wengine wamelazimika kusimamisha utumishi wao wa upainia kwa sababu mbalimbali. Ikiwa ulikuwa painia wa kawaida hapo mbele, je, umechunguza hali zako ili kuona ikiwa unaweza kuwa tena painia?

2. Kwa nini ingekuwa vizuri wale waliokuwa mapainia hapo mbele wachunguze hali zao za sasa?

2 Hali Zinabadilika: Labda hali iliyofanya usimamishe kazi yako ya upainia imebadilika. Kwa mfano, ikiwa ulisimamisha kazi yako ya upainia kwa kuwa ilikuwa vigumu kwako kufanya saa 90 kwa mwezi, je, unaweza kurudilia kazi yako ya upainia kwa kuwa sasa ni saa 70 zinazoombwa? Ikiwa ulisimamisha kazi yako ya upainia kwa sababu ulilazimika kuwa na kazi ya kimwili ili kutimiza mahitaji yako fulani ao kwa sababu ya madaraka ya familia, je, mahitaji hayo na madaraka hayo yamepunguka? Dada mmoja aliyesimamisha kazi ya upainia kwa sababu ya afya mbaya alirudilia kazi hiyo alipokuwa na miaka 89. Alifanya mwaka mzima bila kuingia hospitalini, kwa hiyo aliona kwamba afya yake ingemwezesha kuwa tena painia!

3. Namna gani washiriki wa familia wanaweza kuungana mkono ili mmoja wao afanye kazi ya upainia?

3 Labda haukuwa painia hapo mbele, lakini mutu mmoja katika familia yenu alisimamisha kazi yake ya upainia ili kumutunza mshiriki fulani wa familia, kwa mfano mzazi aliyezeeka. (1 Tim. 5:4, 8) Ikiwa ni hivyo, je, wewe ao wengine katika familia munaweza kusaidia yule aliyeacha kazi ya upainia ili apate wakati wa kurudilia kazi ya upainia? Kwa nini musizungumzie jambo hilo pamoja? (Met. 15:22) Wakati washiriki wa familia wanaungana mkono ili mmoja wao awe painia, wote watajisikia kuwa wanashiriki katika kazi hiyo.

4. Utafanya nini ikiwa hauwezi kurudilia kazi ya upainia kwa sasa?

4 Usivunjike moyo ikiwa hali zako za sasa hazikuruhusu kurudilia kazi ya upainia. Nia yako ya kufanya hivyo inampendeza Yehova. (2 Kor. 8:12) Tumia uzoefu uliopata ulipokuwa painia katika kazi ya kuhubiri unayofanya sasa. Katika sala zungumzia tamaa yako ya kupenda kurudilia kazi ya upainia, na uwe macho ili kuona nafasi zinazoweza kufanya ubadili hali zako. (1 Yoh. 5:14) Labda, kwa wakati wake, Yehova atakufungulia “mlango mkubwa unaoongoza kwenye utendaji” ili upate tena furaha uliokuwa nayo ulipokuwa painia wa kawaida!—1 Kor. 16:9.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine