Siku Tatu za Kuburudishwa Kiroho
1. Tunatazamia nini kupitia mkusanyiko wa wilaya wa mwaka huu?
1 Katika inchi hii yenye kukauka kiroho, yaani ulimwengu wa Shetani, Yehova anaendelea kuwaburudisha watumishi wake. (Isa. 58:11) Mkusanyiko wa wilaya unaofanywa kila mwaka ni njia moja kati ya njia anazotumia ili kututia nguvu. Mkusanyiko wa mwaka huu unapokaribia, namna gani tunaweza kujitayarisha ili tutiwe nguvu kiroho na kuwasaidia wengine?—Met. 21:5.
2. Ni matayarisho gani ambayo unahitaji kufanya?
2 Ikiwa haujajitayarisha, anza sasa kufanya mipango ili kutengeneza programu yako na kazi yako ya kimwili ili uwe hapo muda wa siku zote tatu za mkusanyiko. Je, umekwisha kufikiria ikiwa itakuchukua saa ngapi ili kufika kila siku mahali ambapo mkusanyiko utafanywa na kuchukua nafasi ya kukaa mbele programu ianze? Hatupendi kabisa kukosa sehemu yoyote ya chakula cha kiroho chenye kututia nguvu ambacho Yehova ametayarisha kwa ajili yetu! (Isa. 65:13, 14) Je, umekwisha kufanya mipango kuhusu mahali pa kupangia na kuhusu usafirishaji?
3. Ni mapendekezo gani yanayoweza kukusaidia wewe na familia yako ili mufaidike kabisa na mkusanyiko?
3 Ni nini kitakachokusaidia ili ufuate programu yote kwa uangalifu bila kukengeushwa? Ikiwezekana, upumzike vya kutosha kila usiku muda wote wa mkusanyiko. Kwenye mkusanyiko, kazia msemaji macho. Tafuta kila andiko katika Biblia yako. Andika mambo ya lazima. Ni vizuri watu wa kila familia wakae pamoja ili wazazi wasaidie watoto wao wafuate kwa uangalifu. (Met. 29:15) Labda munaweza kuzungumzia katika familia mambo makuu ya programu kila mangaribi. Ili familia yenu iendelee kuburudishwa kiroho hata kisha mkusanyiko, wakati wa Ibada ya Familia ya mangaribi, munaweza kuchukua wakati ili kuzungumzia mambo fulani ya lazima ambayo munaweza kutumia katika familia yenu.
4. Namna gani tunaweza kuwasaidia wengine katika kutaniko letu waburudishwe kiroho?
4 Tuwasaidie Wengine Waburudishwe Kiroho: Tunataka wengine pia waburudishwe kiroho. Katika kutaniko lenu, je, kuna wahubiri wenye kuzeeka ao wengine wanaohitaji msaada ili wahuzurie mkusanyiko? Je, unaweza kuwasaidia? (1 Yoh. 3:17, 18) Wazee, zaidi sana waangalizi wa vikundi, watashugulikia jambo hilo ili kuona kwamba wahubiri kama hao wamepata msaada wanaohitaji.
5. Namna gani tutatolea watu mialiko tunapoenda kwenye mkusanyiko? (Ona pia kisanduku kilicho hapo juu.)
5 Kama tulivyofanya wakati uliopita, majuma matatu mbele mkusanyiko uanze, tutafanya kampanye ya kualika watu waje kuhuzuria mkusanyiko. Makutaniko yanapaswa kujiwekea mradi wa kugawa mialiko yao na kuigawia watu wengi katika eneo lao kadiri iwezekanavyo. Ikiwa familia yako inabaki na mialiko fulani mwishoni mwa kampanye, muje na mialiko hiyo kwenye mkusanyiko ili muitumie kualika watu munapohubiri munapokwenda kwenye mkusanyiko. Mutapewa maagizo mengine Siku ya Tano kwenye mkusanyiko kuhusu jinsi ya kutumia mialiko hiyo. Ikiwa bado familia yako ina mialiko mingine ya zaidi ambayo haitawezekana kutolea watu wakati mutakapopatikana katika muji ambamo mkusanyiko utafanywa, munaweza kuwapatia wakaribishaji mialiko hiyo munapofika mahali ambapo mkusanyiko utafanywa. Tafazali, uchunge mwaliko mmoja kwa ajili yako kwa kuwa utauhitaji wakati wa hotuba ya mwisho ya Siku ya Yenga.
6. Namna gani tunaweza kujiendesha kwa adabu kwenye mkusanyiko?
6 Kujiendesha kwa Adabu Kunaburudisha: Wakati ambapo watu wengi ni “wenye kujipenda wenyewe” na hawafikirie hali ya wengine, inaburudisha kabisa kuwa pamoja na Wakristo wenzetu wanaojikaza kujiendesha kwa adabu! (2 Tim. 3:2) Tunajiendesha kwa adabu kwa kuingia mahali pa mkusanyiko kwa utulivu na kwa utaratibu milango inapofunguliwa na kwa kuchungia viti wale tu tunaoishi nao nyumba moja, ao wale tunaosafiri nao katika gari moja, ao wale tunaojifunza nao Biblia sasa. Tunajiendesha kwa adabu kwa kufuata maagizo yanayotolewa na mwenyekiti wa kipindi cha mkusanyiko anapotuomba tuketi na kusikiliza kipindi cha muziki unaofungua kila kipindi cha mkusanyiko. Tunaonyesha adabu kwa kutia telefone zetu katika hali ambayo haitakengeusha wengine wakati wa programu. Tunaonyesha pia adabu kwa kutozungumza-zungumza, kutoandika-andika ujumbe kwa njia ya telefone, kutokula, na kutotembea-tembea wakati wa programu.
7. Namna gani tunaweza kuburudishwa na kuwaburudisha wengine kiroho tunapokuwa na ndugu zetu?
7 Kuzungumza na Wengine Kunaburudisha: Mikusanyiko inatutolea nafasi nyingi za kufurahia umoja wetu wa Kikristo wenye kuburudisha na upendo wa kindugu. (Zab. 133:1-3) Kwa nini usichukue hatua ya ‘kupanuka’ na kukutana na ndugu na dada wa makutaniko mengine walio kwenye mkusanyiko? (2 Kor. 6:13) Unaweza kujiwekea mradi wa kufahamiana na mutu mmoja ao familia moja kila siku. Mapumuziko ya midi yanatutolea nafasi nzuri ya kufanya hivyo. Kwa hiyo, ulete chakula chepesi na ule mahali pa mkusanyiko na kuzungumza na ndugu na dada zetu kuliko kwenda kununua chakula ao kula kwenye restora iliyo karibu na mahali pa mkusanyiko. Kwa kufanya hivyo utapata nafasi ya kuunda urafiki mpya na wenye kudumu.
8. Kwa nini ni lazima tujitolee kufanya kazi kwenye mkusanyiko, na tunaweza kufanya hivyo namna gani?
8 Ni jambo lenye kuburudisha sana kutumika pamoja na waabudu wenzetu katika utumishi mtakatifu! Je, unaweza kujitolea ili kufanya kazi katika Biro fulani ao kushiriki katika mgawo wa usafishaji ambao kutaniko lenu litapewa? (Zab. 110:3) Ikiwa haujakuwa na mgawo wowote, tafazali uende kwenye Biro ya Wafanyakazi Wanaojitolea ili upewe kazi kwenye mkusanyiko. Kutumika watu wengi kunafanya kazi iwe yenye kufurahisha na rahisi.
9. Kwa nini tunapaswa kuhangaikia zaidi mwenendo na mvalio wetu siku zote tatu za mkusanyiko?
9 Mwenendo Wetu Unawafurahisha Wale Wanaotutazama: Tutaonyesha mwenendo safi muda wa siku zote tatu za mkusanyiko mahali popote tutakapopatikana, si tu wakati wa programu. Wale wanaotutazama tunapokuwa katika muji ambamo mkusanyiko unafanywa wanapaswa kufurahi kuona kwamba sisi ni tofauti kabisa na wale wasio Mashahidi. (1 Pet. 2:12) Mvalio wetu na namna yetu ya kujipamba vinapaswa kumletea Yehova sifa tunapokuwa kwenye mkusanyiko, mahali ambapo tunapangishwa, na kwenye restora tukienda kula huko. (1 Tim. 2:9, 10) Ikiwa tunavaa kadi zetu za utambulisho, wale wanaotutazama watatambua kwamba sisi ni Mashahidi wa Yehova. Hilo linaweza kututolea nafasi ya kuwaelezea kuhusu mkusanyiko wetu na kuwatolea ushahidi wa zaidi.
10. Ni mambo gani yaliyoonwa yanayoonyesha kwamba mwenendo wetu wa Kikristo unatoa ushahidi mzuri?
10 Mwenendo wetu mzuri wakati wa mkusanyiko unawavutia wengine namna gani? Kulingana na gazeti moja, msimamizi wa jengo fulani lililotumiwa kwa ajili ya mkusanyiko alisema hivi: “Watu hao ni wenye adabu kabisa. Tunafurahi kuwakaribisha hapa kila mwaka.” Mwaka uliopita mutu fulani asiye Shahidi alipoteza mfuko wake mdogo wa kubebea feza kwenye hoteli iliyopangisha ndugu na dada waliokuja kwenye mkusanyiko. Mfuko huo uliporudishwa kwa msimamizi wa hoteli pamoja na vyote vilivyokuwa ndani, msimamizi wa hoteli alimwambia mwenye mfuko hivi: “Ufurahi kwamba Mashahidi wa Yehova walihuzuria mkusanyiko wao katika muji, na kwamba walijaa katika hoteli. Haingekuwa hivyo, labda haungepata tena mfuko wako.”
11. Kwa kuwa mkusanyiko unakaribia, tunapaswa kuwa na mradi gani, na kwa nini?
11 Mkusanyiko wa mwaka huu unakaribia. Wakati mwingi umetumiwa ili kutayarisha programu na nguvu nyingi zimefanywa ili mambo yawe yenye kuburudisha kwenye mkusanyiko. Basi, ujiwekee mradi wa kuhuzuria mkusanyiko siku zote tatu, na ujitayarishe kupokea yale ambayo Yehova na tengenezo lake wametayarisha kwa ajili yako. Ukusudie kuwaburudisha wengine kwa kujiendesha kwa adabu, kuzungumza nao kwa furaha, na kupitia mwenendo wako mzuri. Kwa kufanya hivyo, wewe na wengine munaweza kujisikia kama alivyojisikia mwanamuke fulani aliyehuzuria mkusanyiko mwaka uliopita, ambaye aliandika hivi: “Sijapata kuona kipindi chenye kufurahisha zaidi kama hicho!”
[Wazo la fungu kwenye ukurasa wa 4]
Kama tulivyofanya wakati uliopita, majuma matatu mbele mkusanyiko uanze, tutafanya kampanye ya kualika watu waje kuhuzuria mkusanyiko
[Wazo la fungu kwenye ukurasa wa 6]
Mvalio wetu na namna yetu ya kujipamba vinapaswa kumletea Yehova sifa tunapokuwa kwenye mkusanyiko, mahali ambapo tunapangishwa, na kwenye restora
[Wazo la fungu kwenye ukurasa wa 7]
Ukusudie kuwaburudisha wengine kwa kujiendesha kwa adabu, kuzungumza nao kwa furaha, na kupitia mwenendo wako mzuri
[Sanduku katika ukurasa wa 4]
Mambo ya Kukumbuka Kuhusu Mkusanyiko wa Wilaya wa 2011
◼ Saa: Siku zote tatu programu itaanza pa saa 2:20 asubuhi (8h20). Lakini, mikusanyiko itakayofanywa katika miji mikubwa ifuatayo: Brazzaville, Goma, Kananga, Kikwit, Kinshasa, Kisangani, Kolwezi, Likasi, Lodja, Lubumbashi, Matadi, Mbandaka, Mbuji-Mayi, Mwene Ditu, Pointe Noire na Tshikapa, programu itaanza kila siku pa saa 3:20 asubuhi (9h20). Milango itafunguliwa pa saa 1:00 asubuhi (7h00) ao saa 2:00 asubuhi (8h00), kulingana na mahali. Wakati muziki wa kufungua utakapoanza, sisi wote tunapaswa kukaa ili programu iweze kuanza kwa utaratibu.
◼ Kuchungia Wengine Viti: Munaweza kuchungia viti wale tu munaoishi nao katika nyumba moja, wale munaosafiri nao katika gari moja ao wale munaojifunza nao Biblia kwa sasa.—1 Kor. 13:5.
◼ Chakula Wakati wa Midi: Inapendekezwa kwamba kila mutu alete kitu fulani cha kula kisicho kizito lakini cha kujenga mwili, kwa mfano: sandwichi (mikate ao keki), matunda (ndizi), kalanga, vitumbua ao ndazi. Vinywaji kama vile maji, kahawa ao chai vinapaswa kutiwa katika vyombo visivyoweza kuvunjika ili kuepuka aksida. Hairuhusiwi kuleta pombe kwenye mkusanyiko. Ikiwa tunaleta chakula na kinywaji chetu, hatutahitaji kununua vyakula kwa wale wanaouzisha chakula inje. Kuepuka kununua vyakula kwa wale wanaouzisha chakula inje kunasaidia kuonyesha kwamba sisi ni watu safi. (Tafazali, jueni kwamba wale wanaouzisha chakula inje hawataruhusiwa kuingia katika eneo la mkusanyiko wakati wowote.—Yoh. 2:13-17.)
◼ Michango: Tunaweza kuonyesha shukrani yetu kwa ajili ya mipango ya mkusanyiko kwa kutoa michango ya kujipendea kwenye Jumba la Ufalme ao mahali pa mkusanyiko, ili kutegemeza kazi ya ulimwenguni pote. Sheke zote zinazotolewa kwenye mkusanyiko zinapaswa kuandikwa kwa jina Association “Les Témoins de Jehovah.”
◼ Aksida na Mambo Yanayoomba Kutenda Haraka: Ndugu wanaohusika na mambo yanayoomba kutenda haraka wanaitwa sana kwa sababu ya mambo madogo-madogo. Ikiwa kunatokea jambo linaloomba kutenda haraka kwenye mkusanyiko, tafazali unaweza kumwelezea ndugu mkaribishaji aliye karibu ambaye atajulisha bila kuchelewa ndugu wanaoshugulika na Matunzo ya Haraka ili waamue ikiwa hali inaomba kutoa msaada unaohitajiwa.
◼ Kukamata Picha: Ukikamata picha kwenye mkusanyiko, tafazali usitumie mwangaza (flash). Tafazali, usiite mahali pa mkusanyiko wale wanaofanya kazi ya kukamata picha. Ikiwa unawaona wakitafuta mutu wa kukamata picha, usikubali wakukamate picha.—Yoh. 2:13-17.
◼ Telefone za Mkononi: Zinapaswa kutiwa katika hali ambayo haitakengeusha wasikilizaji.
◼ Usafi: Imeonekana mara nyingi kwamba wale wanaonunua vyakula kutoka kwa wale wanaouzisha chakula inje wanatupa chini makaratasi ya kufungia vyakula. Hivyo, eneo lote linajaa makaratasi, vifuko vya plastiki, na vifuniko vya machupa ya vinywaji-sukari, nk. Ikiwa mutu anachagua kununua chakula kwa wale wanaouzisha chakula inje (kwa mfano: bonbons, biskwiti, ndazi ao vitumbua, vipande vya samaki ao chakula kingine) anapaswa kutupa makaratasi ya kufungia vyakula katika chombo cha kutupia uchafu kuliko kutupa chini. Tukiona mutu fulani ametupa kipande cha karatasi ao cha plastiki chini, tunapaswa kukiokota na kukitia katika chombo cha kutupia uchafu. Tafazali ndugu, acheni tujikaze sana kuhusu jambo hilo ili kulinda mahali petu pa mkusanyiko na eneo la kandokando vikiwa safi. Kila mutu anayehuzuria anapaswa kuhangaikia jambo hilo la usafi. Ikiwa kila mutu anatimiza sehemu yake, mwishoni mwa siku, mahali pa mkusanyiko pataachwa pakiwa safi. Tunapenda kuonyesha katika maisha yetu sifa za Mungu mtakatifu ambaye tunaabudu.—1 Pet. 1:15, 16; Kut. 19:10; Kum. 23:14.
◼ Mahali Ambapo Tunapangishwa: (1) Usiwe na watu wengi zaidi katika chumba ao nyumba isivyoruhusiwa ao isivyokubaliwa na mutu aliyekukaribisha. (2) Ikiwa utavunja ombi lako la kupangishwa, fanya hivyo bila kukawia. (3) Mbele ya kupika chakula, uliza mwenye nyumba ao ndugu wanaoshugulika na upangishaji kwenye Jumba la Ufalme ili ujue kile kinachohitajiwa ili kuepuka hatari. (4) Usitumie ovyoovyo vitu vyovyote vinavyotolewa kwa ajili ya wageni. Kanuni ya mwenendo ni kuwa mwenye kiasi na mwenye usawaziko. (5) Ili kumwogopa Mungu inafaa kuwa safi. Kila siku, acha mahali ulipopangishwa pakiwa na utaratibu, pakiwa safi. Hilo linahusu pia Jumba la Ufalme, ambalo linaweza kutumiwa kuwa mahali pa upangishaji kwa ajili ya ndugu waliotoka katika makutaniko ya mbali. (6) Onyesha tunda la roho katika kushugulika na wengine, iwe ni mwenye nyumba ao ndugu wengine Wakristo ambao labda munapangishwa pamoja nao.—Gal. 5:22, 23.
◼ Kazi ya Kujipendea: Furaha tunayopata kwa kuhuzuria mkusanyiko itaongezeka ikiwa tunajitolea kufanya kazi. (Mdo. 20:35) Yeyote anayetaka kufanya kazi anapaswa kujulisha Biro ya Wafanyakazi Wanaojitolea Kufanya Kazi kwenye mkusanyiko. Mtoto aliye na miaka chini ya 16 anaweza pia kusaidia kwa kutumika chini ya uongozi wa mzazi wake ao mutu aliyemleta ao mutu mwingine mwenye kukomaa aliyekabiziwa mtoto huyo na wazazi wake.
[Sanduku katika ukurasa wa 5]
Jinsi ya Kumtolea Mutu Mwaliko
Ili kumaliza eneo letu, tunapaswa kusema kwa kifupi. Tunaweza kusema hivi: “Jambo. Ulimwenguni pote tunajikaza kutolea watu mwaliko huu. Chukua mwaliko wako. Utapata maelezo mengine kwenye mwaliko huo.” Ukurasa wa mbele wa mwaliko ni wenye kuvutia, kwa hiyo umtolee mutu mwaliko huo kwa namna inayomfanya auone mara moja ukurasa huo. Sema kwa uchangamfu. Tunapotolea watu mwaliko Siku ya Posho na Siku ya Yenga, tunaweza kuwatolea pia magazeti inapofaa.