Njia Mbalimbali za Kuanzisha Mazungumuzo
Jinsi ya Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Siku ya Posho ya Kwanza Katika Mwezi wa 11
“Je, unafikiri kwamba watu wanaojikaza kumutii Mungu ni wenye furaha kuliko wengine? [Acha mutu ajibu.] Habari hii ina mambo fulani yenye kupendeza.” Umwonyeshe musikilizaji Mnara wa Mlinzi wa tarehe 1 mwezi wa 11 na musome na kuzungumuzia habari ya kichwa kidogo kimoja kati ya vichwa vidogo vilivyo kwenye ukurasa wa 16-17. Musome andiko moja kati ya maandiko yanayoonyeshwa. Umutolee mutu magazeti, na ufanye mupango wa kumurudilia ili kujibu ulizo linalofuata.
Mnara wa Mlinzi 01/11/11
“Watu fulani wanafikiri kwamba mafundisho ya Biblia kuhusu ngono ni ya zamani na kwamba Biblia ina vizuizi visivyohitajiwa kuhusu ngono. Wengine wanakubaliana na Biblia. Wewe unafikiri nini? [Acha mutu ajibu.] Ona yale ambayo andiko hili linasema ili kutuonyesha ikiwa kanuni za Biblia zimetoka wapi. [Soma 2 Timotheo 3:16.] Gazeti hili linaonyesha jinsi Biblia inavyojibu maulizo kumi ambayo watu wanauliza kwa ukawaida kuhusu ngono. Linaeleza pia jinsi kanuni za Biblia zinavyotufaidi.”
Amkeni! Mwezi wa 11
“Ikiwa tunachunguza kwa uangalifu vitu vinavyotuzunguka, hilo linaweza kutufanya tujiulize ikiwa kuna Muumbaji ao ikiwa kila kitu kilijitokeza chenyewe. Wewe unafikiri nini? [Acha mutu ajibu.] Ona yale ambayo mwandikaji fulani wa Biblia alisema alipotazama vitu vilivyo katika ulimwengu. [Soma Waroma 1:20.] Gazeti hili linaeleza yale ambayo wanasayansi wamevumbua kuhusu chembe (cellule) ya mwanadamu; jambo hilo linatusaidia tuelewe kwamba kuna Muumbaji.”