Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 1/12 uku. 1
  • Unatumia Broshua Hizi?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Unatumia Broshua Hizi?
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2012
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Biblia Ina Ujumbe Gani?
  • Maswali Matano Muhimu Kuhusu Chanzo cha Uhai
  • Wewe Unaweza Kuwa Rafiki ya Mungu!
  • Broshua Mpya ya Kutolea Watu!
    Huduma Yetu ya Ufalme—2010
  • Namna ya Kutumia Broshua Habari Njema Inayotoka kwa Mungu!
    Huduma Yetu ya Ufalme—2013
  • Tumwige Yehova Kwa Kuhangaikia Kwelikweli Wengine
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Tutumie Broshua Mbalimbali Katika Mahubiri
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2012
km 1/12 uku. 1

Ichungwe

Unatumia Broshua Hizi?

Biblia Ina Ujumbe Gani?

Broshua hii imetayarishwa ili kuvutia watu ambao hawajui mengi kuhusu Biblia, zaidi sana wale walio katika dini zisizo za Kikristo

Jinsi ya kuitolea watu: “Tungependa kujua mawazo yako juu ya mambo yanayosemwa hapa katika Maandiko (ao katika kitabu hiki kitakatifu). [Soma andiko la Zaburi 37:11, linalozungumuziwa katika sehemu ya 11.] Unawaza dunia itakuwa namna gani wakati unabii huu utatimia? [Acha mutu ajibu.] Huo ni mufano mumoja unaoonyesha kwamba Biblia inaweza kuwatolea watu wa mahali pote na dini zote tumaini na faraja.” Soma fungu la kwanza-kwanza lililo kwenye sehemu ya juu ya ukurasa wa 3, na umutolee mutu broshua.

Namna nyingine ya kuitumia: Ikiwa unajifunza Biblia na mutu aliye katika dini isiyo ya Kikristo kupitia kitabu Biblia Inafundisha, chukua kila mara dakika chache mbele ya funzo ao kisha funzo ili kuzungumuzia sehemu moja ya broshua hii. Kufanya hivyo kutamusaidia mutu aelewe Biblia kwa kifupi.

Maswali Matano Muhimu Kuhusu Chanzo cha Uhai

Broshua hii imetayarishwa kwa ajili ya vijana Wakristo wanaofundishwa mageuzi kwenye masomo na inaweza kutusaidia tunapozungumuza na wale wanaoamini mambo ya mageuzi, wale wanaoshakia kuwapo kwa Mungu, na wale wasioamini kuwapo kwa Mungu (Broshua hii si ya kutolea watu tunapohubiri nyumba kwa nyumba.)

Jinsi ya kuitumia tunapozungumuza na mutu anayeamini mambo ya mageuzi ao mutu asiyeamini kuwapo kwa Mungu: “Leo, karibu kila kitabu cha sayansi kinafundisha mageuzi. Mageuzi ni mambo ya kuwazia-wazia tu ao ni mambo ya hakika? Wewe unawaza namna gani? [Acha mutu ajibu.] Ili kufanya uamuzi muzuri kuhusu jambo hilo, inaomba kuchunguza upande wote, yaani, ikiwa ni mambo ya kuwazia-wazia tu ao ni mambo ya hakika, sivyo? Broshua hii inaonyesha mambo fulani ambayo yamesadikisha watu wengi kwamba kuna Muumbaji.”

Namna nyingine ya kuitumia: Ikiwa wewe ni mwanafunzi, tia broshua hii kwenye meza yako ili kuona ikiwa itachochea wanafunzi fulani wakuulize maulizo kuhusu broshua hiyo.

Wewe Unaweza Kuwa Rafiki ya Mungu!

Broshua hii imetayarishwa ili kuvutia watu wasio na elimu nyingi ao wale wasiojua kusoma vizuri

Jinsi yakuitolea watu: “Unawazia kwamba inawezekana sisi kuwa marafiki wa Mungu? [Acha mutu ajibu. Kisha soma Yakobo 2:23.] Broshua hii imetayarishwa ili kutusaidia tuwe marafiki wa Mungu kama Abrahamu.”

Namna nyingine ya kuitumia: Iwe unazungumuza na mutu kwa mara ya kwanza ao unamurudilia, umuonyeshe jinsi funzo la Biblia linavyofanywa kwa kuzungumuzia pamoja sura ya 1 yote ao sehemu ya sura hiyo.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine