Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 3/12 uku. 2
  • Usiogope Kuhubiria Watu Nafasi za Biashara

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Usiogope Kuhubiria Watu Nafasi za Biashara
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2012
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Tukomalishe Ufundi Wetu wa Kuhubiri—Kutoa Ushahidi Katika Eneo la Biashara
    Huduma Yetu ya Ufalme—2015
  • Jinsi ya Kuhubiri Katika Eneo la Biashara
    Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Tuhubiri Habari Njema Mahali Pote
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Onyesha Kupendezwa Kibinafsi na Wengine—Kwa Kuwa Mwenye Kujitayarisha
    Huduma Yetu ya Ufalme—2006
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2012
km 3/12 uku. 2

Usiogope Kuhubiria Watu Nafasi za Biashara

1. Sababu gani hatupaswi kuvunjika moyo ikiwa tunaogopa kuhubiria watu nafasi za biashara?

1 Unaogopa kuhubiria watu nafasi za biashara? Ikiwa jibu ni ndiyo, usivunjike moyo, kwa sababu hata mutume Paulo, aliyekuwa muhubiri mwenye bidii na asiye na woga, alilazimika ‘kujipatia ujasiri’ ili kuhubiri. (1 The. 2:2) Tutazungumuzia hali fulani zinazotuhangaisha na mapendekezo yenye kufaa yanayoweza kutusaidia kushinda mahangaiko hayo.

2. Sababu gani hatupaswi kuogopa kwa kuwaza kama tutawauzi wafanyabiashara?

2 Nikiwakatiza Wafanyabiashara, Sitawauzi? Kwa kawaida mufanyabiashara yeyote anatazamia tu kukatizwa. Mara nyingi wafanyabiashara ni wenye adabu, kwa sababu wanapomuona mutu anawakaribia wanawazia kama anakuja kununua vitu. Ikiwa unavaa kwa heshima na ikiwa unaonyesha hali ya uchangamufu na ya urafiki, watakuheshimu.

3. Namna gani tunaweza kuepuka kuwauzi watu wanaonunua vitu?

3 Nikitoa Ushahidi Katika Magazini Wakati Watu Wananunua Vitu, Sitawauzi? Ikiwezekana, ingia katika magazini wakati hakuna wetu wengi, kwa mufano wakati wanapofungua. Zungumuza na mwenye magazini ao mutu anayeuzisha humo wakati yuko yeye mwenyewe. Usiseme maneno mengi.

4. Tunaweza kusema nini tunapohubiria watu nafasi za biashara?

4 Nitasema Nini? Ikiwa kuna wafanyakazi wengi, zungumuza na musimamizi wa biashara. Unaweza kusema hivi: “Ni vigumu kuwakuta wafanyabiashara nyumbani, ndiyo sababu tunakutembelea nafasi yako ya kazi. Ninajua kama uko kwenye kazi, na kwa hiyo nitasema kwa kifupi.” Ili watu wasituwazie kuwa wachuuzi wa vitabu, kwa kawaida ni vizuri tusizungumuzie muchango wa kujipendea isipokuwa tu mutu anatuuliza namna kazi yetu inavyoendeshwa. Ikiwezekana, unaweza kumuomba musimamizi wa biashara ruhusa ili kuzungumuza kwa kifupi na wafanyakazi. Unapozungumuza nao, rudilia maneno uliyomuambia musimamizi. Ukiona kama mufanyakazi ana kazi nyingi, sema tu maneno machache na umuachie trakti. Ikiwa haiwezekani kuzungumuza na wafanyakazi, labda utaruhusiwa kuacha vichapo mahali wanapopumuzikia ao mahali pengine ambapo wote wanaweza kuingia.

5. Sababu gani hatupaswi kuogopa kuhubiria watu nafasi za biashara?

5 Paulo na Yesu hawakuogopa kuhubiria watu nafasi za biashara, na wewe unaweza kufanya hivyo. (Math. 4:18-21; 9:9; Mdo. 17:17) Umuombe Yehova akusaidie uwe na moyo mutulivu na pia moyo wa ujasiri ao moyo usioogopa. (Mdo. 4:29) Kwa sababu watu hawakosekani nafasi za biashara, sababu gani usijaribu aina hii ya mahubiri yenye kuzaa matunda?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine