Les jeunes s’interrogent... Comment se faire de vrais amis ?
Yehova aliwaumba watu ili watumike pamoja na kufanya urafiki na wengine. (Met. 17:17; 18:1, 24) Ili urafiki huo uwe wenye faida, ni lazima kila mutu achague marafiki kwa uangalifu. (Met. 13:20) Kisha kutazama video Les jeunes s’interrogent... Comment se faire de vrais amis ? (Vijana Wanauliza—Namna Gani Ninaweza Kujifanyia Marafiki wa Kweli?) je, unaweza kujibu maulizo yafuatayo?
Utangulizi:
(1) Rafiki wa kweli ni nani?
Des obstacles à l’amitié (Mambo Yanayoweza Kutuzuia Kupata Marafiki):
(2) Namna gani tunaweza kushinda hali ya kujisikia kama wengine hawatujali? (Flp. 2:4) (3) Sababu gani tunapaswa kuwa tayari kufanya utu wetu uwe muzuri zaidi, na ni nani anayeweza kutusaidia kufanya hivyo? (2 Kor. 13:11) (4) Nafasi za kupata marafiki wengi zaidi zinaweza kupatikana namna gani?—2 Kor. 6:13.
L’amitié avec Dieu (Urafiki Pamoja na Mungu):
(5) Namna gani tunaweza kuwa na urafiki wa karibu pamoja na Yehova, na sababu gani inaomba kujikaza sana? (Zab. 34:8) (6) Tunapomufanya Yehova kuwa rafiki wetu wa karibu, tunaweza kuwa na urafiki wa namna gani na watu wengine?
Des amis peu recommandables (Marafiki Wabaya):
(7) Marafiki wabaya ni nani? (1 Kor. 15:33) (8) Namna gani marafiki wabaya wanaweza kuharibu hali ya kiroho ya mutu?
Une fiction contemporaine (Drama ya Kisasa):
(9) Hadisi ya Biblia kuhusu Dina inatufundisha nini? (Mwa. 34:1, 2, 7, 19) (10) Namna gani Tara aliutetea urafiki wake pamoja na vijana wa ulimwengu? (11) Marafiki wake kwenye masomo walimuingiza katika hatari gani? (12) Sababu gani wazazi wake hawakutambua hatari aliyokuwa ndani, lakini walipotambua tatizo lake walimusaidia namna gani ili atengeneze hali yake ya kiroho? (13) Namna gani dada mumoja painia alijionyesha kuwa rafiki wa kweli wa Tara? (14) Tara alifikia kuona mambo namna gani?
Umalizio:
(15) Wewe umejifunza mambo gani kutokana na video hii? (16) Namna gani unaweza kuitumia ili kuwasaidia wengine?
Acheni basi tuwachague marafiki ambao watatusaidia tulinde urafiki wetu pamoja na Mungu—urafiki ulio bora zaidi!—Zab. 15:1, 4; Isa. 41:8.