Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 10/12 uku. 7
  • Njia Tano za Kupata Funzo la Biblia

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Njia Tano za Kupata Funzo la Biblia
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2012
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Je, Unauliza ili Ujulishwe Kuhusu Wale Wanaoweza Kukubali Kujifunza Biblia?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2006
  • Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo
    Huduma Yetu ya Ufalme—2005
  • Namna ya Kusaidia Wanafunzi wa Biblia Wafikie Kubatizwa—Sehemu ya Kwanza
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
  • Namna Kutaniko Linaweza Kusaidia Wanafunzi wa Biblia Wafikie Kubatizwa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2021
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2012
km 10/12 uku. 7

Njia Tano za Kupata Funzo la Biblia

1. Ikiwa ni vigumu kwetu kupata funzo la Biblia katika eneo letu, tunapaswa kufanya nini, na sababu gani?

1 Je, imekuwa vigumu kwako kupata funzo la Biblia? Endelea kutafuta. Yehova anawabariki wale ambao hawachoke kufanya mapenzi yake. (Gal. 6:9) Hapa chini tunapendekeza njia tano ili kukusaidia kupata funzo la Biblia.

2. Namna gani tunaweza kuanzisha funzo la Biblia mara tu tunapotembelea watu?

2 Kuuliza Watu Ikiwa Wangependa Kujifunza Biblia: Watu wengi wanajua kama tunatolea watu Munara wa Mulinzi na Amkeni!, lakini inawezekana hawajue kama tunafundisha watu Biblia. Unapohubiri nyumba kwa nyumba, unaweza kuwauliza watu mara tu unapowatembelea ikiwa wangependa kujifunza Biblia. Unaweza pia kuwauliza watu wanaopendezwa ikiwa wanataka kujifunza Biblia. Ikiwa wanakataa, unaweza kuendelea kuwaachia vichapo na kuwasaidia waendelee kupendezwa. Kwa muda wa miaka mingi, ndugu mumoja alitolea bwana mumoja na bibi yake magazeti kwa kawaida. Siku moja kisha kuwaachia magazeti ya karibuni, alitaka kuenda, lakini akakumbuka kuwauliza ikiwa wangependa kujifunza Biblia. Alishangaa kuona kwamba walikubali. Kwa sasa, wote wawili ni wenye kubatizwa.

3. Je, ni vizuri kuwaza kama kila mutu anayehuzuria mikutano ana mutu anayemufundisha Biblia? Eleza.

3 Kuuliza Watu Wenye Kupendezwa Wanaohuzuria Mikutano: Usiwaze kama kila mutu anayependezwa ambaye anahuzuria mikutano ana mutu anayemufundisha Biblia. Ndugu mumoja alieleza hivi: “Zaidi ya nusu ya mafunzo ya Biblia niliyopata yalianzishwa kwa kuzungumuza na watu waliohuzuria mikutano.” Dada mumoja aliamua kumukaribia mwanamuke fulani mwenye haya ambaye mabinti wake wenye kubatizwa walikuwa washiriki wa kutaniko lake. Mwanamuke huyo alikuwa amehuzuria mikutano kwa muda wa miaka 15 hivi na alikuwa akifika kwenye Jumba la Ufalme mara tu mikutano ilipoanza na aliondoka mara tu mikutano ilipokwisha. Mwanamuke huyo alikubali funzo na mwishowe akaikubali kweli. Dada huyo aliandika hivi: “Ninasikitika kwa sababu nilingojea miaka 15 mbele ya kumuuliza ikiwa anataka kujifunza Biblia!”

4. Namna gani tunaweza kupata funzo kupitia wanafunzi wa Biblia na wahubiri wengine?

4 Kuuliza Ikiwa Kuna Watu Wanaoweza Kukubali Funzo La Biblia: Dada mumoja anajikaza kuwasindikiza wengine wanapoenda kuongoza mafunzo ya Biblia. Kwa ruhusa ya mwalimu, kisha funzo, dada huyo anamuuliza mwanafunzi ikiwa anajua mutu mwengine ambaye angetaka kujifunza Biblia. Unapomutolea mutu ambaye umetembelea kwa muda fulani kitabu Biblia Inafundisha, unaweza kumuuliza hivi: “Je, unamujua mutu mwengine ambaye angependa kupata kitabu hiki?” Wakati fulani, kuna hali zinazoweza kuzuia muhubiri ao painia kujifunza na mutu fulani aliyekutana naye katika eneo. Kwa hiyo, ni vizuri kuwajulisha wahubiri wengine kama uko tayari kuongoza funzo la Biblia.

5. Sababu gani tunaweza kumuuliza mwenzi wa ndoa asiyeamini wa ndugu ao dada ikiwa angetaka kujifunza Biblia?

5 Kumuuliza Mwenzi wa Ndoa Asiye Shahidi: Je, katika kutaniko lenu kuna muhubiri ambaye bibi yake ao bwana yake si Shahidi? Watu fulani wanakataa kujifunza Biblia pamoja na wenzi wao wa ndoa ambao ni Mashahidi lakini wanaweza kukubali kujifunza na mutu asiye mushiriki wa familia yao. Kwa kawaida, ni vizuri zaidi kuzungumuza kwanza na ndugu ao dada mbele ya kumuuliza mwenzi wake asiye Shahidi ikiwa angetaka kujifunza Biblia. Hilo linasaidia kujua njia nzuri zaidi ya kutumia ili kumuhubiria.

6. Sababu gani sala ni ya lazima ili kupata funzo la Biblia?

6 Sala: Usizarau nguvu ya sala. (Yak. 5:16) Yehova anaahidi kusikiliza sala zetu ikiwa zinapatana na mapenzi yake. (1 Yoh. 5:14) Ndugu fulani ambaye alikuwa na kazi nyingi alianza kusali ili apate funzo la Biblia. Bibi yake alijiuliza ikiwa bwana yake atapata wakati wa kushugulikia mwanafunzi, zaidi sana ikiwa mwanafunzi huyo ana matatizo mengi. Kwa hiyo, alimujulisha Yehova hangaiko hilo aliposali ili bwana yake apate funzo. Kisha majuma mawili hivi sala zao zilijibiwa; painia mumoja katika kutaniko alipata mutu aliyetaka kujifunza Biblia na hivyo akamupatia ndugu huyo funzo hilo. Bibi ya ndugu huyo aliandika hivi: “Kwa watu ambao wanawaza ni vigumu kupata funzo la Biblia, ninawaambia: Mumuambie Yehova waziwazi katika sala tatizo lenu, na musichoke kufanya hivyo. Tumepata furaha nyingi kuliko jinsi nilivyowaza.” Ukivumilia, wewe pia unaweza kupata funzo la Biblia na kupata furaha ya kumusaidia mutu atembee katika “barabara inayoongoza kwenye uzima.”​—Mt. 7:13, 14.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine