Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 11/12 uku. 3
  • Usijizuie Kuanzisha Funzo kwa Sababu Una Kazi Nyingi

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Usijizuie Kuanzisha Funzo kwa Sababu Una Kazi Nyingi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2012
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Usisite Kuongoza Funzo la Biblia!
    Huduma Yetu ya Ufalme—2007
  • Fanyeni Programu ya Familia Yenye Kufaa
    Huduma Yetu ya Ufalme—2005
  • Namna ya Kusaidia Wanafunzi wa Biblia Wafikie Kubatizwa—Sehemu ya Kwanza
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
  • Mambo Yenye Itakusaidia Kujifunza kwa Ukawaida
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2012
km 11/12 uku. 3

Usijizuie Kuanzisha Funzo kwa Sababu Una Kazi Nyingi

1. Sababu gani watu fulani wanasita kuanzisha funzo la Biblia?

1 Watu fulani wanasita kuanzisha funzo kwa sababu wana kazi nyingi. Ni kweli kwamba kushugulikia mwanafunzi wa Biblia kunachukua wakati. Inaomba wakati ili kutayarisha funzo, kuliongoza, na kumusaidia mwanafunzi ashinde vizuizi fulani. Mutume Paulo alisema kama alitoa nafsi yake ili kuwasaidia Wathesalonike wafikie kumujua Yehova. (1 Thes. 2:7, 8) Namna gani tunaweza kuongoza funzo la Biblia hata kama tuna kazi nyingi?

2. Kwa kuwa tunamupenda Yehova, tutatumia wakati wetu namna gani?

2 Inaomba Wakati ili Kumuabudu Yehova: Ukweli ni kwamba ibada inaomba wakati. Kwa mufano, kwa ukawaida tunachukua wakati ili kuhuzuria mikutano, kuhubiri, kusoma Biblia, na kusali. Mutu aliyefunga ndoa anafurahia kupitisha wakati pamoja na mwenzi wake, hata kama ana kazi nyingi. Kwa kuwa tunamupenda Yehova, tunapaswa ‘kujinunulia’ kwa furaha wakati mwingi hata zaidi ili kumuabudu, sivyo? (Efe. 5:15-17; 1 Yoh. 5:3) Yesu alionyesha kama kazi ya kufanya wanafunzi ni sehemu ya maana sana ya ibada yetu. (Mt. 28:19, 20) Kufikiria jambo hilo kutatusaidia tusisite kukubali daraka la kuongoza mafunzo ya Biblia.

3. Namna gani tunaweza kushugulikia mwanafunzi wa Biblia hata ikiwa mambo fulani yanazuia programu yetu?

3 Tuseme nini ikiwa tunazuiwa mara kwa mara kwa sababu ya kazi, magonjwa yasiyopona, ao madaraka ya kiteokrasi? Wahubiri fulani wanaosafiri mara kwa mara wanaongoza mafunzo yao ya Biblia kwa njia ya telefone ao kupitia internete. Wale wanaozuiwa mara kwa mara kwa sababu ya magonjwa yasiyopona wamefanya mipango ili wanafunzi waje kwenye nyumba zao ili kujifunza. Wengine wamefanya mipango ili muhubiri mwengine awasaidie kuongoza funzo ikiwa hawana wakati.

4. Ni baraka gani zinazotokana na kuongoza mafunzo ya Biblia?

4 Paulo alipata furaha nyingi kwa kutumia wakati wake na nguvu zake ili kuwasaidia wengine waijue kweli. (Mdo. 20:35) Alipofikiria watu wote ambao alisaidia huko Thesalonike, alichochewa kumushukuru Yehova. (1 Thes. 1:2) Tunaweza kupata furaha na kutosheka zaidi katika mahubiri ikiwa haturuhusu kazi zetu nyingi zituzuie kuongoza mafunzo ya Biblia.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine