“Toa Ushahidi Kamili”
1. Mutume Paulo aliweka mufano muzuri gani katika mahubiri?
1 “Timiza kwa ukamili huduma yako.” (2 Tim. 4:5) Mutume Paulo alikuwa na zamiri safi alipomutolea Timotheo shauri hilo. Kuanzia mwaka wa 47 mupaka wa 56 kisha kuzaliwa kwa Yesu, Paulo alifanya safari tatu ya umisionere. Kitabu cha Matendo kinazungumuzia mara nyingi Paulo akitoa “ushahidi kamili.” (Mdo. 23:11; 28:23) Tunaweza kumuiga namna gani leo?
2. Namna gani tunaweza kutoa ushahidi kamili tunapohubiri nyumba kwa nyumba?
2 Nyumba kwa Nyumba: Ili kuwapata watu ambao hawajasikia habari njema, ni lazima tuwatembelee watu wakati tofauti. Inaweza kuwa vizuri kuhubiri wakati wa mangaribi ili tumukute Baba wa familia. Tunapaswa kujikaza kuzungumuza hata na mutu moja katika kila nyumba na kuwatembelea mara kwa mara wale ambao hatukukuta nyumbani. Unaweza kufanya nini ikiwa unamutembelea mutu mara nyingi lakini haumukute nyumbani? Labda kuandika barua ao kumuita kwa njia ya telefone kunaweza kuwa na matokeo mazuri.
3. Una nafasi gani za kutoa ushahidi mahali pa watu wengi na wakati haukupanga kufanya hivyo?
3 Mahali pa Watu Wengi na Wakati Hatukupanga Kufanya Hivyo: Leo, watumishi wa Yehova wanajulisha watu wote wanaowasikiliza “hekima ya kweli.” Wakati fulani, wanafanya hivyo “barabarani” ao “katika viwanja vya watu wote.” (Met. 1:20, 21) Tunapokuwa katika shuguli zetu za kila siku, je, tunakumbuka kutoa ushahidi? Watu wanaweza kusema kutuhusu kama ‘tunashugulika sana na lile neno’? (Mdo. 18:5) Ikiwa tunajibu ndiyo, basi tunatimiza daraka letu la “kutoa ushahidi kamili.”—Mdo. 10:42; 17:17; 20:20, 21, 24.
4. Namna gani kusali na kutafakari kunaweza kutusaidia kutoa ushahidi kamili?
4 Wakati fulani, kwa sababu ya uzaifu tulio nao ao kwa sababu ya haya, tunaweza kusita kutoa ushahidi. Kwa kweli, Yehova anajua uwezo wetu. (Zab. 103:14) Lakini, ikiwa tunakuwa katika hali kama hizo, tunaweza kumuomba Yehova atupe ujasiri wa kusema. (Mdo. 4:29, 31) Pia, tunapofanya funzo letu la pekee na kutafakari juu ya Neno la Mungu, tunaweza kukaza uangalifu juu ya namna tunavyoweza kupendezwa na habari njema ambayo ni ya maana sana. (Flp. 3:8) Kufanya hivyo kutatuchochea tuitangaze kwa bidii!
5. Tunaweza namna gani kushiriki katika utimizo wa unabii wa Yoeli?
5 Unabii wa Yoeli ulitabiri kama mbele ya kuja kwa ile siku kubwa ya Yehova na yenye kuogopesha, watu wa Mungu ‘wangesonga mbele’ na hawangeruhusu kitu chochote kiwazuie kuhubiri. (Yoe. 2:2, 7-9) Acheni basi tufanye yote tuwezayo ili kushiriki kwa ukamili katika kazi hiyo ya kutoa ushahidi ambayo haitarudiliwa tena!