Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 2/03 uku. 3-4
  • Tuhubiri na Kutoa Ushahidi Kamili

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Tuhubiri na Kutoa Ushahidi Kamili
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Tutafute Mapainia Wasaidizi 100,000
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Je! Tutafanya Hilo Tena?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Tangazeni Mahali Pote Sifa Bora za Yehova
    Huduma Yetu ya Ufalme—2007
  • Mradi Unaofaa kwa Ajili ya Mwaka Mpya wa Utumishi
    Huduma Yetu ya Ufalme—2007
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2003
km 2/03 uku. 3-4

Tuhubiri na Kutoa Ushahidi Kamili

1 Akiwa “mukubwa na jemadari,” Yesu alizoeza wanafunzi wake kwa ajili ya kazi kubwa ya kuhubiri iliyokuwa mbele yao. (Isa. 55:4; Luka 10:1-12; Mdo. 1:8) Mtume Petro alifafanua utume ambao Yesu aliwapa kwa maneno haya: “Alituagiza sisi tuwahubiri watu na kutoa ushahidi kamili kwamba Huyu ndiye aliyeagizwa na Mungu kuwa hakimu wa walio hai na wafu.” (Mdo. 10:42) Kutoa ushahidi kamili kunahusisha nini?

2 Tunaweza kujifunza mengi kwa kufikiria mfano wa mtume Paulo. Alipokutana na wanaume wazee kutoka kutaniko la Efeso, aliwakumbusha: “Sikuepuka kuwaambia nyinyi lolote kati ya mambo yaliyokuwa yenye kuleta faida wala kuwafundisha nyinyi hadharani na kutoka nyumba hadi nyumba. Lakini nilitoa ushahidi kikamili kwa Wayahudi na Wagiriki pia juu ya toba kuelekea Mungu na imani katika Bwana wetu Yesu.” Ijapokuwa alivumilia majaribu yeye mwenyewe, Paulo alitumika kwa nguvu ili kufikisha habari njema kwa watu wengi zaidi iwezekanavyo. Hakutosheka tu na kushiriki kweli za msingi na wasikilizaji wake, bali alitumika kwa nguvu ili kuambia wasikilizaji wake “shauri lote la Mungu.” Ili kutimiza hilo, alikuwa tayari kufanya jitihada na kujinyima. Aliendelea kusema: “Sifanyi nafsi yangu kuwa kitu chenye thamani sana kwangu, kama tu ningepata kumaliza mwendo wangu na huduma niliyopokea ya Bwana Yesu, kutoa ushahidi kamili kuhusu habari njema ya fadhili isiyostahiliwa ya Mungu.”—Mdo. 20:20, 21, 24, 27.

3 Tunawezaje kuiga mfano wa Paulo leo? (1 Kor. 11:1) Kwa kutafuta watu mmojammoja na familia zinazostahili, hata wakati sisi wenyewe tunapopambana na majaribu; kwa kujitahidi kufikisha habari njema kwa vikundi vyote vya kikabila na lugha; na kwa kusitawisha kwa bidii kupendezwa kulikopatikana. (Mt. 10:12, 13) Hilo linaomba wakati, jitihada, na upendo kuelekea watu.

4 Je, Unaweza Kutumika Ukiwa Painia Msaidizi? Miezi ya Machi na Aprili ingekuwa wakati mzuri kwako kutoa ushahidi kamili kwa kuwa painia msaidizi. Lilikuwa jambo lenye kutia moyo kama nini mwaka uliopita kuona wahubiri wengi sana wakifanya jitihada ya pekee ili kuwa mapainia wasaidizi!

5 Dada mmoja mwenye umri wa miaka 80 na mwenye matatizo mengi ya afya alichochewa na kitia-moyo kilichotolewa na tengenezo la Yehova. Aliandika: “Kiliwasha tena tamaa iliyokuwa katika moyo wangu kwa muda mrefu, na kilinifanya nihisi kwamba nilipaswa kabisa kuwa painia msaidizi tena hata mara moja.” Akaamua kufanya hivyo mnamo Machi. “Jambo la kwanza nililofanya,” akasema, “lilikuwa kukaa na kuhesabu gharama. Mimi na binti yangu tulizungumzia jambo hilo tena na tena kwa kuwa ningehitaji msaada wake. Alinishangaza kwa kutwaa ombi kwa ajili yake mwenyewe.” Muda wa mwezi, dada huyo mzee-mzee alipitisha saa 52 katika huduma. “Mara nyingi niliomba Yehova afanye upya nguvu zangu nilipohisi kwamba zilikuwa zikiisha. Kwenye mwisho wa mwezi, nilikuwa mwenye furaha sana na mwenye kutosheka, na nimemshukuru Yehova mara nyingi kwa kunisaidia. Ningependa kujaribu tena.” Furaha aliyoipata inaweza kutia moyo wengine ambao wanataka kwelikweli kuwa mapainia wasaidizi ijapokuwa matatizo makubwa ya afya.

6 Ndugu mmoja aliyeachishwa kazi ya kimwili bila kutazamia alitumia hali hiyo ili kuwa painia msaidizi. Mnamo mwezi aliotumia ili kupainia, alijaa bidii kwa ajili ya kazi ya kuhubiri, na kufikia mwisho wa mwezi, alikuwa ameanzisha funzo jipya la Biblia. Akifikiria jambo hilo, alisema: “Ni mwezi wenye kuthawabisha kama nini!” Alikuwa mwenye furaha kama nini kuwa na mwongozo na msaada wa Yehova! Ndiyo, Yehova alimmwagia baraka tele kwa sababu ya jitihada ya ziada ambayo ndugu huyo alifanya katika huduma, na atafanya hivyohivyo kwa ajili yako.—Mal. 3:10.

7 Kwa wengi, kuwa painia msaidizi si jambo jepesi. Hata hivyo, ijapokuwa madaraka ya kimwili na ya kifamilia na vilevile matatizo ya kibinafsi, ndugu na dada wengi wameweza kufanya hivyo. Kutoa ushahidi kamili mara nyingi kunaomba kujinyima wakati wa thamani na nguvu, lakini baraka zinazotokana na jambo hilo haziwezi kulinganishwa na jambo lingine lolote.—Mez. 10:22.

8 Machi na Aprili ni miezi bora ya kuwa painia msaidizi. Kuna miisho-juma mitano katika mwezi wa Machi. Kutumia vizuri miisho-juma hiyo na saa za jioni kutawezesha watu fulani wanaofanya kazi ya wakati wote kuwa mapainia wasaidizi. Zaidi ya hilo, unaweza kutumia sikukuu ili kuhubiri mnamo mwezi wa Aprili. Wengine wanaweza kuwa na siku za mapumziko shuleni au kazini, jambo linaloweza kuwasaidia kutimiza saa 50 zinazoombwa. Ili kupanga kupitisha saa 50 katika huduma mnamo Machi na Aprili, je,unaweza kutumia moja ya programu za kielelezo za painia msaidizi zinazotiwa ndani ya makala hii? Zungumzia programu yako na wengine; bila shaka wengine watatiwa moyo wajiunge nawe katika huduma. Ikiwa hauwezi kuwa painia msaidizi, jiwekee mradi kamili wa kutimiza mnamo miezi hiyo, na utegemeze wale wanaoweza kupainia. Fanya mipango yako sasa ili kuhubiri zaidi mnamo Machi na Aprili.

9 Onyesha Kwamba Unathamini Ukumbusho: Kila mwaka katika majira ya Ukumbusho, shukrani kwa ukombozi zinachochea wengi ‘kununua kabisa wakati’ ili kuwa mapainia wasaidizi. (Efe. 5:15, 16) Katika Congo-Kinshasa mwaka uliopita, kulikuwa na mapainia wasaidizi 5,879 mnamo Machi na 6,507 mnamo Aprili. Hilo linatoa wastani wa mapainia wasaidizi 6,193 kwa kila mmoja wa miezi hiyo miwili. Linganisha hiyo na hesabu ya wastani ya wahubiri 3,298 waliokuwa mapainia wasaidizi mnamo kila mmoja wa miezi iliyotangulia ya mwaka wa utumishi. Katika Congo-Brazzaville mwaka uliopita, kulikuwa mapainia wasaidizi 424 mnamo Machi na 199 mnamo Aprili. Hilo linatoa wastani ya mapainia wasaidizi 312 kwa kila mmoja wa miezi hiyo miwili. Linganisha hiyo na hesabu ya wastani ya wahubiri 129 waliokuwa mapainia wasaidizi mnamo kila mmoja wa miezi iliyotangulia ya mwaka wa utumishi. Majira haya ya Ukumbusho ni nafasi nyingine ya kuonyesha kwamba tunathamini kwa unyofu dhabihu ya ukombozi ya Kristo kwa kuongeza utendaji wetu katika huduma ya shambani.

10 Aprili 16 inapokaribia, fikiria lile ambalo Ukumbusho unamaanisha kwako. Fikiria matukio yaliyoongoza kwenye kifo cha Kristo na mawazo yaliyolemea akili na moyo wake. Tafakari pia juu ya shangwe iliyowekwa mbele ya Yesu na jinsi ilivyomsaidia kuvumilia kutendewa vibaya kwa namna hiyo. Fikiria kwa uzito cheo chake sasa akiwa Kichwa cha kutaniko, akisimamia kazi ya kuhubiri na kufanya wanafunzi. (1 Kor. 11:3; Ebr. 12:2; Ufu. 14:14-16) Kisha, onyesha shukrani zako kwa yote ambayo Kristo amefanya kwa kushiriki kikamili zaidi iwezekanavyo katika kazi ya kuhubiri kadiri hali zako zinavyoruhusu.

11 Tieni Wengine Moyo Watoe Ushahidi Kamili: Kwa kushiriki katika utumishi wa upainia msaidizi, wazee na watumishi wa huduma wana nafasi nzuri ya kutia wengine moyo. Wanapotumika na wahubiri katika huduma ya shambani na wanapofanya ziara za uchungaji, wana nafasi nzuri ya kusaidia kibinafsi wengine washiriki kikamili katika utendaji huo wa pekee. Sisi sote na tusali kuhusu jambo hilo, hivyo tukitia nguvu jitihada zetu zenye umoja za kutoa ushahidi kamili.

12 Wazee wote na watumishi wa huduma watafanya kazi kulingana na mipango ya kutaniko kwa ajili ya utendaji zaidi mnamo miezi ya Machi na Aprili, lakini mwangalizi wa utumishi hasa anapaswa kufanya mipango ya pekee kwa ajili ya kazi ya kueneza evanjeli. Anapaswa kupanga mahali pa kufanyia mikutano kwa ajili ya utumishi wa shambani, siku, na wakati unaofaa kwa wahubiri walio wengi na kufanya mipango hiyo itangazwe kikawaida. Mipango inaweza kuchukuliwa ili mikutano ifanywe pa saa tofauti-tofauti za mchana ili kutolea wote katika kutaniko nafasi ya kushiriki aina mbalimbali za kazi ya kutoa ushahidi. Hilo linaweza kutia ndani kutumika katika eneo la biashara, kutoa ushahidi barabarani, kuhubiri nyumba kwa nyumba, kufanya ziara za kurudia, na kutoa ushahidi kwa njia ya simu. Zaidi ya hayo, anapaswa kufanya mipango ili kuwe na kiasi cha kutosha cha vichapo, magazeti, na eneo mnamo miezi hiyo.

13 Mnamo Machi tutatolea watu kitabu Ujuzi, tukiwa na mradi wa kuanzisha mafunzo ya Biblia. Mapendekezo mazuri ili kutolea watu kitabu Ujuzi yalitangazwa katika nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Januari 2002. Toleo la vichapo la Aprili litakuwa magazeti Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Jaribu kutumikisha utoaji mbalimbali unaopendekezwa katika habari “Tuseme Nini Kuhusu Magazeti.” Sote tunapaswa kuchukua wakati wa kujitayarisha vizuri ili kutoa ushahidi kamili.

14 Sisi ni wenye kubarikiwa kama nini kutumika chini ya uongozi wa Kichwa cha kutaniko, Kristo Yesu, na kuwa na pendeleo la kushiriki habari njema na wengine! Miezi ya Machi na Aprili inapokaribia, na tujitahidi tena kuifanya kuwa miezi yetu bora zaidi huku tukitii amri ya Kristo ya kuhubiri na kutoa ushahidi kamili.

[Picture on page 4]

Njia Mbalimbali za Kuwa Painia Msaidizi

Mnamo Machi na Aprili 2003

[Picture on page 4]

SikuSaa

Siku ya Kwanza12——2—

Siku ya Pili1—3———

Siku ya Tatu12—5——

Siku ya Nne1—3———

Siku ya Tano12————

Siku ya Posho543567

Siku ya Yenga223223

Machi565654555050

Aprili50505153——

[Picture on page 4]

Je, moja ya programu hizi itafaa kwako?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine