Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 3/13 uku. 2
  • Tuwakaribishe!

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Tuwakaribishe!
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2013
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Ushahidi Mkubwa Utatolewa
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Tuwakaribishe Wageni Wetu
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2016
  • Namna Gani Tutasaidia Wale Watakaohuzuria Ukumbusho?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Mtolee Yehova Shukrani kwa Ajili ya Fadhili Zake Zenye Upendo
    Huduma Yetu ya Ufalme—2005
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2013
km 3/13 uku. 2

Tuwakaribishe!

1. Ni tukio gani linalotutolea nafasi nzuri zaidi ya kutoa ushahidi, na kwa sababu gani?

1 Ukumbusho tunaoazimisha kila mwaka unatutolea nafasi nzuri zaidi ya kutoa ushahidi kuliko wakati mwengine wowote. Fikiria jambo hili: Mwaka huu tunatazamia zaidi ya watu milioni 10 kuhuzuria Ukumbusho na kusikia namna gani Yehova na Yesu Kristo wametuonyesha upendo mukubwa kwa kutoa zabihu ya ukombozi. (Yoh. 3:16; 15:13) Watajifunza kuhusu baraka zinazotokana na zawadi hiyo ya Yehova. (Isa. 65:21-23) Lakini, wakati huo, si musemaji tu ndiye atatoa ushahidi. Wahuzuriaji wote watapata nafasi ya kutoa ushahidi wenye nguvu kwa kuwakaribisha kwa uchangamfu wageni wetu.—Rom. 15:7.

2. Namna gani tunaweza kuwakaribisha kwa uchangamfu wageni kwenye Ukumbusho?

2 Kuliko tu kutafuta nafasi ya kukaa na kungojea kwa ukimya programe ianze, itakuwa vizuri kujitambulisha kwa wale walio karibu nawe. Wageni wanaweza kuwa na wasiwasi kwa sababu hawajui namna mambo yatakavyofanyika. Kuwaonyesha sura ya kicheko na kuwasalimia kwa njia ya kirafiki kutawafanya wajisikie vizuri na wenye kukaribishwa. Ili kujua ikiwa mutu fulani anakuja kwa sababu alialikwa, unaweza kumuuliza kama ni mara yake ya kwanza kuhuzuria mikutano yetu ao kama anamujua mutu fulani katika kutaniko. Labda unaweza kumualika akae pamoja nawe ili uchangie pamoja naye Biblia na kitabu chako cha nyimbo. Ikiwa kutaniko lingine lingali linatumia Jumba la Ufalme, unaweza kumutembeza kidogo. Kisha hotuba, umuambie kwamba ikiwa ana maulizo, uko tayari kuyajibu. Ikiwa kutaniko lenu linapaswa kuacha haraka Jumba la Ufalme kwa ajili ya kutaniko lingine, unaweza kusema: “Ningependa kujua maoni yako juu ya programe hii. Naweza kukupata namna gani?” Kisha upange kumuona siku ingine. Wazee hasa watakuwa waangalifu ili kutia moyo wahubiri wasiotenda wanaohuzuria Ukumbusho.

3. Sababu gani ni jambo la maana tujikaze kuwakaribisha wageni wetu kwenye Ukumbusho?

3 Itakuwa mara ya kwanza kwa wageni wengi kuona furaha, amani na umoja ambao watumishi wa Yehova wanapata katika paradiso ya kiroho. (Zab. 29:11; Isa. 11:6-9; 65:13, 14) Wageni watakumbuka jambo gani kisha kuhuzuria Ukumbusho? Jibu litategemea sana mambo tutakayofanya ili kuwakaribisha.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine