Programu ya Juma Tokea Tarehe 28 Mwezi wa 10
JUMA TOKEA TAREHE 28 MWEZI WA 10
Wimbo 31 na Sala
□ Funzo la Biblia la Kutaniko:
jl uku. 3 na Somo 1-2 (Dak. 30)
□ Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi:
Usomaji wa Biblia: 1 Timotheo 1-6–2 Timotheo 1-4 (Dak. 10)
Kujikumbusha Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi (Dak. 20)
□ Mukutano wa Utumishi:
Wimbo 61
Dak. 5: “Utafanya Nini Wakati wa Sikukuu?” Hotuba.
Dak. 10: Onyesha Faida ya Habari Njema Katika Maisha. Mazungumuzo yanayotegemea kitabu Shule ya Huduma, ukurasa wa 159. Mufanye onyesho kuhusu namna ya kutolea watu kitabu Biblia Inafundisha kwa kutumia habari inayopendeza watu wa eneo lenu.
Dak. 15: Ulazima wa Kufika kwa Wakati. Mazungumuzo. (1) Yehova anatuwekea mufano gani kuhusu kuchunga wakati? (Hab. 2:3) (2) Namna gani kufika kwa wakati kwenye mikutano ya kutaniko na mikutano kwa ajili ya mahubiri kunaonyesha kwamba tunamuheshimu Yehova na tunawafikiria wengine? (3) Ikiwa tunachelewa mukutano kwa ajili ya mahubiri, hilo linakuwa na matokeo gani juu ya ndugu anayeongoza na wengine? (4) Ikiwa tunamuahidi mutu aliyependezwa ao funzo la Biblia kwamba tutamurudilia wakati fulani, sababu gani ni jambo la lazima tufike kwa wakati? (Mt. 5:37) (5) Tunaweza kufanya nini ili kufika kwa wakati kwenye mikutano ya kutaniko ao mikutano kwa ajili ya mahubiri?
Wimbo 69 na Sala