Kujikumbusha Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi
Maulizo yanayofuata yatatumiwa kwenye Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi katika juma tokea tarehe 24 Mwezi wa 2, 2014.
1. Shetani alimuchochea Eva afikirie nini, na Eva alionyesha nini kwa kula tunda la muti uliokatazwa? (Mwa. 3:6) [Juma tokea tarehe 6 Mwezi wa 1, w11 15/5 uku. 16-17 fu. 5]
2. Inawezekana Abeli alifikia kuwa na imani yenye nguvu namna gani, na imani hiyo ilimuletea faida gani? (Mwa. 4:4, 5; Ebr. 11:4) [Juma tokea tarehe 6 Mwezi wa 1, w13 1/1 uku. 12 fu. 3; uku. 14 fu. 4-5]
3. Namna gani wazazi wanaweza kuwalinda watoto wao ili wasishangazwe na kuvutiwa na “watu wenye nguvu” na “wanaume wenye sifa”? (Mwa. 6:4) [Juma tokea tarehe 13 Mwezi wa 1, w13 1/4 uku. 13 fu. 2]
4. Tunaweza kujifunza nini juu ya habari ya Loti na bibi yake, kama inavyozungumuziwa katika andiko la Mwanzo 19:14-17, 26? [Juma tokea tarehe 27 Mwezi wa 1, w03 1/1 uku. 16-17 fu. 20]
5. Namna gani Abrahamu alionyesha imani katika ufufuo na katika ahadi ya Yehova ya kutokeza uzao ulioahidiwa katika kizazi cha Isaka? (Mwa. 22:1-18) [Juma tokea tarehe 3 Mwezi wa 2, w09 1/2 uku. 18 fu. 4]
6. Tunaweza kujifunza kweli gani za lazima kutokana na unabii ulio katika andiko la Mwanzo 25:23, unaosema kama ‘mukubwa atamutumikia mudogo’? [Juma tokea tarehe 10 Mwezi wa 2, w03 15/10 uku. 29 fu. 1]
7. Yakobo aliona katika ndoto kitu chenye tafsiri fulani za Biblia zinaita “ngazi,” ao “kipandio”; ngazi hiyo ilimaanisha nini? (Mwa. 28:12, 13) [Juma tokea tarehe 10 Mwezi wa 2, w04 15/1 uku. 28 fu. 6]
8. Sababu gani Labani alihangaishwa sana wakati miungu yake iliibwa, na sababu gani alitamani sana kuipata? (Mwa. 31:30-35) [Juma tokea tarehe 17 Mwezi wa 2, it-2-F uku. 100 fu. 1]
9. Jibu lenye malaika alimupatia Yakobo katika andiko la Mwanzo 32:29, linatufundisha nini? [Juma tokea tarehe 24 Mwezi wa 2, w13 1/8 uku. 10]
10. Namna gani tunaweza kuepuka matokeo mabaya kama yale yaliyomupata Dina? (Mwa. 34:1, 2) [Juma tokea tarehe 24 Mwezi wa 2, w01 1/8 uku. 20-21]