Kampanye ya Kuwaalika Watu Kwenye Ukumbusho
Mwaka huu kampanye ya kuwaalika watu kwenye Ukumbusho itaanza Siku ya Posho tarehe 22 Mwezi wa 3. Sisi wote tunatiwa moyo kushiriki katika kampanye hiyo kwa bidii. Ikiwa hali inaruhusu, tutawaachia pia watu magazeti Siku ya Posho na Siku ya Yenga. Siku ya Posho ya kwanza ya Mwezi wa 4, kuliko kuanzisha mafunzo ya Biblia, tutawaachia watu mialiko. Hata hivyo, mutu akipendezwa, tunaweza kuanzisha funzo la Biblia. Mwangalizi wa utumishi ataamua ikiwa wahubiri wanaweza kuwatolea watu mialiko mahali pa watu wengi, ikiwa kufanya hivyo kutasaidia wahubiri wafikie watu wengi zaidi. Tuanze sasa kuandika kwenye karatasi majina ya watu wa jamaa yetu, wafanya-kazi wenzetu, wanafunzi wenzetu, watu tunaorudilia, na wengine ambao tunataka kualika ili wahuzurie ukumbusho, na tupange kuwaachia mialiko wakati kampanye itaanza. Tunatumaini kwamba watu wengi watajiunga na sisi tutakapokumbuka namna Yehova na Yesu walituonyesha upendo mukubwa.—Yoh 3:16; 15:13.