Programu ya Juma la Tarehe 15 Mwezi wa 12
JUMA LA TAREHE 15 MWEZI WA 12
Wimbo 1 na Sala
Funzo la Biblia la Kutaniko:
cl sura ya 17 fu. 9-16 (Dak. 30)
Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi:
Usomaji wa Biblia: Yoshua 6-8 (Dak. 10)
Na. 1: Yoshua 8:18-29 (Isipite dak. 4)
Na. 2: Ni Nini Kinachoonyesha Kwamba Mutu Ana Roho Takatifu?—rs uku. 243 fu. 3–uku. 244 fu. 2 (Dak. 5)
Na. 3: Adui (Adversaire)— Shetani Ibilisi Ndiye Adui Yetu Mukubwa Zaidi— it-1-F uku. 52 (Dak. 5)
Mukutano wa Utumishi:
Tungo la Mwezi: Tutoe “mambo mema [mazuri]” kutoka katika hazina nzuri ambayo tumepewa.—Mt. 12:35a.
Wimbo 101
Dak. 15: “Tuongoze Mafunzo ya Biblia Yenye Kufanya Maendeleo.” Maulizo na majibu. Kisha kuzungumuzia fungu la 3, mufanye onyesho lenye sehemu mbili la muhubiri ambaye anaongoza funzo la Biblia kwenye sura ya 15, fungu la 8 la kitabu Biblia Inafundisha. Katika onyesho la kwanza, muhubiri anasema mingi. Lakini katika onyesho la pili, muhubiri anauliza maulizo ambayo yanamusaidia mwanafunzi atoe mawazo yake.
Dak. 15: Chombo cha Kutusaidia Kujitayarisha ili Kuongoza Mafunzo ya Biblia. Mazungumuzo. Vuta uangalifu wa wasikilizaji kwenye sehemu yenye kichwa “Biblia Inafundisha Nini?” iliyo kwenye jw.org (Fungua Sehemu MAFUNDISHO YA BIBLIA > VIJANA.) Eleza namna sehemu hiyo inaweza kutumiwa ili kutusaidia kuongoza mafunzo ya Biblia pamoja na watu wa miaka tofauti tofauti, vijana na wazee. Namna gani maulizo yaliyo kwenye karatasi hizo za maulizo yanaweza kutusaidia tujue mambo yaliyo katika moyo wa mwanafunzi? Mufanye onyesho la mutu mwenye kujisemesha anayetumia sehemu hiyo ili imusaidie kufikiri juu ya mahitaji ya mwanafunzi na kutayarisha maulizo ambayo yatamusaidia kujua mawazo ya mwanafunzi. Ikiwa wahubiri wa kutaniko lenu hawatumie Internete, mazungumuzo yenu yatategemea sura ya 1 ya kitabu Biblia Inafundisha. Kichwa cha habari kitakuwa “Ujitayarishe Kuongoza Mafunzo ya Biblia.” Tumia Maulizo haya: (1) Namna gani unaweza kujibu mutu mwenye anasema kwamba Mungu anawapatia watu wabaya malipizi kwa kuwatesa? Unaweza kutumia andiko gani ili kumujibu? Sababu gani utatumia zaidi sana andiko hilo? (2) Unaweza kujibu namna gani kama mutu fulani anauliza hivi: Ikiwa Mungu anatuhangaikia kweli kweli, juu ya nini yeye aliye na nguvu zote hazuie mambo mabaya? Unaweza kutumia andiko gani ili kumujibu? Sababu gani utatumia zaidi sana andiko hilo? Malizia kwa kuwatia moyo wasikilizaji wakuwe wafundishaji wazuri, wajikaze kugusa mioyo ya wanafunzi wao kwa kutumia mambo mazuri ambayo tuko nayo ili kuwasaidia wengine.—Met. 20:5.
Wimbo 99 na Sala