Tuongoze Mafunzo ya Biblia Yenye Kufanya Maendeleo
1. Wahubiri wenye kuongoza mafunzo ya Biblia wana daraka gani?
1 Ili mutu afikie kumutumikia Yehova, ni lazima Yehova ‘amuvute’ kwanza. (Yoh. 6:44) Hata hivyo, wahubiri ambao wanaongoza mafunzo ya Biblia wanapaswa kufanya sehemu yao kwa kuwasaidia wanafunzi wamukaribie Baba yao wa mbinguni. (Yak. 4:8) Hilo linaomba kujitayarisha. Kusoma tu kila fungu na kuuliza ulizo lililo katika kitabu hakutoshe ili kumusaidia mwanafunzi aelewe kabisa ujumbe na kufanya maendeleo.
2. Mwanafunzi wa Biblia mwenye kufanya maendeleo atafikia hatua gani?
2 Ili kuongoza mafunzo ya Biblia yenye kufanya maendeleo, wahubiri wanapaswa kuwasaidia wanafunzi wao (1) waelewe mafundisho ya Biblia, (2) wakubali mafundisho hayo, na (3) wayatumikishe katika maisha yao. (Yoh. 3:16; 17:3; Yak. 2:26) Inaweza kuchukua miezi ili kusaidia mwanafunzi afikie hatua hizo. Hata hivyo, kila hatua inamusaidia kufanya urafiki wake pamoja na Yehova uwe nguvu na kufikia kujitoa katika sala ili kumutumikia.
3. Sababu gani walimu wazuri wanauliza maulizo ambayo yanamuchochea mwanafunzi atoe mawazo yake?
3 Mwanafunzi Ana Mawazo Gani?: Ili kutambua ikiwa mwanafunzi wa Biblia anaelewa na kukubali mambo ambayo anajifunza, epuka kusema mingi, na umutie moyo atoe mawazo yake. (Yak. 1:19) Je, anaelewa mafundisho ya Biblia juu ya habari ambayo munajifunza? Anaweza kueleza habari hiyo kwa maneno yake mwenyewe? Ana mawazo gani juu ya mambo yenye anajifunza? Anaamini kwamba mafundisho ya Biblia ni yenye kusaidia katika maisha? (1 Thes. 2:13) Anaelewa kwamba mambo ambayo anajifunza yanapaswa kumuchochea kufanya mabadiliko katika maisha yake? (Kol. 3:10) Ili kupata majibu kwa maulizo kama hayo, ni vizuri umuulize kwa hekima maulizo ambayo yatamufanya atoe mawazo yake, na kisha umusikilize.—Mt. 16:13-16.
4. Tutafanya nini ikiwa mwanafunzi ana magumu ya kuelewa ao ya kutumikisha mambo ambayo anajifunza?
4 Mara nyingi ni vigumu mutu kuacha tabia na namna yake ya kufikiri ya zamani, na inaomba wakati ili kufanya hivyo. (2 Kor. 10:5) Tutafanya nini ikiwa mwanafunzi hakubali ao hatumikishe mambo ambayo anajifunza? Inaomba kuvumilia na kuacha wakati wa kutosha upite ili Neno la Mungu na roho takatifu viguse moyo wa mwanafunzi. (1 Kor. 3:6, 7; Ebr. 4:12) Ikiwa mwanafunzi ana magumu ya kuelewa ao ya kutumikisha mafundisho ya Biblia, kuliko kumukaza, mara nyingi ni muzuri zaidi kuacha habari hiyo na kuzungumuzia habari ingine. Ikiwa tunaendelea kumufundisha kwa uvumilivu na kwa upendo, baada ya muda anaweza kuchochewa kufanya mabadiliko yanayohitajiwa.