Tukomalishe Ufundi Wetu wa Kuhubiri—Kuonyesha Namna Funzo la Biblia Linafanywa kwa Kutumia Kitabu Biblia Inafundisha
Sababu Gani Ni Lazima Kufanya Hivyo: Pengine watu wengi hawataelewa wakati tunawaambia kwamba tunajifunza na watu Biblia bila malipo. Wanaweza kufikiri kwamba watajiunga na kikundi fulani ili kujifunza pamoja ao watajifunza kupitia barua ao Internete. Kuliko kusema tu kwamba tunajifunza na watu Biblia, ni vizuri zaidi kuwaonyesha namna funzo hilo linafanywa. Kwa dakika kidogo tu, hata kwenye mulango, unaweza kumuonyesha mutu namna kujifunza Biblia ni jambo rahisi na linafanya ajue mambo mengi kabisa.
Tumikisha Shauri Hili Katika Mwezi:
Muombe Yehova abariki bidii yako ya kujikaza kuanzisha funzo la Biblia.—Flp. 2:13.
Jaribu kuonyesha mutu namna funzo la Biblia linafanywa kwa kutumia kitabu Biblia Inafundisha ao onyesha video yenye kichwa Funzo la Biblia Linafanywa Namna Gani? hata mara moja wakati uko katika mahubiri.